Hongera sana DC Jokate na atafika mbali sana katika uongozi wake

tatum

JF-Expert Member
Jan 16, 2018
5,786
4,490
DoHyBV9WsAAwxTb.jpg

Moja ya Wakuu wa Wilaya katika awamu hii ya tano ambaye kiukweli amekuwa mstari wa mbele kutembea nje ya ofisi na kuona ukweli wa miradi ya maendeleo ,huduma za jamii ktk sekta ya afya,elimu ,maji na huduma zingine kujua namna zinavyotolewa na mamlaka husika kwa kushirikiana na jamii husika naona kabisa Kisarawe mpya inakuja.

Kwa hakika huyu dada atafika mbali sana watumishi wengi wanampenda na huwezi kusikia akitoa matamko yenye utata wala kuwatumisha wananchi wake na viongozi wao maana amaeona jinsi wanavyokabiliwa na hali ngumu na umasikini uliokithiri na hasa ukichanganya na mila na desturi za mikoa ya pwani kwahiyo anakazi ngumu sana kuibadili jamii hiyo ambayo wao kwao umasikini ni kitu cha kawaida tu kwao kutoenda shule wao wanaona sawa tu.

Hongera sana DC Jokate kwa kiliona hilo na kuamua kuwa nao sambasamba ili kuwafanya wabadilike kiumtazama na kimaendeleo.Mungu na akupe nguvu na uweze kufikia malengo uliyojipangia.

wasahili wanasema ukienda kwa wenye chongo vunja lako jicho

DoH1TRfVAAA5kmo.jpg
 
Wengi wanafanya sana hivi vitu tofauti ni kwamba DC wa Kisarawe yupo karibu sana na media, ndiyo maana ni rahisi kuona kila anachofanya!
 
Hawa wa media hakuna lolote! Yaani hata akinywa kahawa nayo ni habari eti ni kazi. Wapo viongozi mikoani wanapiga kazi achana na hawa wapenda sifa akina dab na huyo unayemsifia. Juzi juzi rais kashuhudia mwenyewe.
 
Hawa wa media hakuna lolote! Yaani hata akinywa kahawa nayo ni habari eti ni kazi. Wapo viongozi mikoani wanapiga kazi achana na hawa wapenda sifa akina dab na huyo unayemsifia. Juzi juzi rais kashuhudia mwenyewe.
ok tuletee hao wa mikoani wanaopiga kazi....unafikiri kwanini kila siku Trump ana tweet
 
Unafikiri wote watakafuata watakuwa wapenda ...., wengine wana hofu ya Mungu hawapendelei hivyo vitu
 
Mtamuharibia mwenzenu kazi bure kazi haipimwi kwa mkuu wa wilaya kutembelea shule na kunywa gahawa.


Angalieni umaskini wa watu tazameni vipato vyao, chakula chao, wanapolala, matibabu yao, kazi zao na nyenzo wanazotumia kufanyia kazi, miundo mbinu, huduma za jamii na uhuru wao wa kutoa maoni na kuchagua.

Mkianza kutazama urembo mnatutoa kwenye reli.
 
Hivi yule jamaa aliyekuwaga Iringa aliyekuwa anapiga picha daily na kutupia mitandaoni. ile kasi iliishia wapi??

Au mukulu alishamtumbua??
 
Back
Top Bottom