"Kila mtoto atakayeanza darasa la kwanza 2017 ataripoti na mche wa mti, ataupanda na kuutunza kwa miaka yote atakayosoma - Waziri Makamba"
View attachment 420974
Mimi ningeshauri elimu ianze ili wanafunzi pamoja na wazazi wapende kupata na kutunza miti. Rais Nyerere alikuwa akitumia hotuba zake kuwaelimisha wananchi kupenda na kupanda miti na watu walitokea kupenda kupanda na kutunza miti. Alizoea kusema: "Kabla ya kukata mti panda mitatu". Binafsi nili'implement' kauli mbiu hii hadi leo hii napanda na kutunza miti si kwa kulazimishwa, bali kwa kupenda mwenyewe kwa sababu nilielimika na pia kilichonisaidia nilisoma shule yenye mchipuo wa kilimo kwa miaka 6 na hadi sasa elimu ya kilimo na mazingira iko kwenye damu yangu. Bado naandaa mazingira ya sehemu nilipohamia na nataka uwe mfano kwa Watanzania wenzangu kujifunza kupenda na kutunza mazingira.
