Hongera mamlaka ya kivuko Kigamboni

Hongera mamlaka ya kivuko Kigamboni

nimechafukwa

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2013
Posts
290
Reaction score
237
Kufuatia sakata la kigaidi lililotokea Kenya apa kivukoni kuna upekuzi. Hii itatuweka salama sana ukizingatia kivuko kinabeba watu wengi alishababu wakiingia huko watatumaliza. Ningeomba uongozi utafute angalau wanajeshi 10 kwa kila kivuko tuwe tunavuka nao kwa usalama zaidi.
 
kufuatia sakata la kigaidi lililotokea Kenya apa kivukoni kuna upekuzi...hii itatuweka salama sana ukizingatia kivuko kinabeba watu wengi alishababu wakiingia huko watatumaliza ....ningeomba uongozi utafute angalau wanajeshi 10 kwa kila kivuko tuwe tunavuka nao kwa usalama zaidi....

Acha woga wewe! Hao wanajeshi kumi ndo wakumzuia mtoa roho?? Hata iwekwe brigade nzima kama mbwai mbwai tu
 
kufuatia sakata la kigaidi lililotokea Kenya apa kivukoni kuna upekuzi...hii itatuweka salama sana ukizingatia kivuko kinabeba watu wengi alishababu wakiingia huko watatumaliza ....ningeomba uongozi utafute angalau wanajeshi 10 kwa kila kivuko tuwe tunavuka nao kwa usalama zaidi....

Nashauri kwa wakristo wenzangu tunaoishi.mkoa wa Dar es Salaam, kwa siku ya leo tusijotokeze wala kutembelea maeneo yatakayokuwa na mkusanyiko ya watu, kama vile beaches, night clubs, shopping malls, hata pale katika ule uwanja wa taifa katika tamasha la pasaka, etc tahadhari imetolewa kuwa hawa jamaa watafanya maangamizi makubwa huko, pamoja na jijini Mwanza
 
ha ha ha bora kufa ukiwa una sifu uwanja wa taifa kuliko kujifungia ndani...
 
Huo ukaguzi unahusisha magari na waenda kwa miguu?? Bado nafikiri kuna mengi zaidi yanahitajika pale kivukoni.
 
Niliona kuanzia jmo kuna askari alikuw anakagua magari na baadhi ya abiria lakujiuliza jee ni zoezi endelevuu?
 
Lile suala la pantoni zote mbili kuondoka kwa pamoja husababisha kuwa na idadi kubwa mno ya watu pindi zinaporudi sijui kama zoezi hili litafanikiwa kuwa endelevu, kwani mtu anakua amesubiri mda mrefu anataka awahi na mkaguzi anataka kumkagua. Anyway acha tuone.
 
Niliona kuanzia jmo kuna askari alikuw anakagua magari na baadhi ya abiria lakujiuliza jee ni zoezi endelevuu?

Baada ya mashambulizi ya Western Gate, tuliona ukaguzi wa watu na magari ulianzishwa pale Mlimani City shopping mall; ajabu baada ya mwezi wakaacha. Sijui waliwasiliana na Al Shabab wakawaeleza tumeahirisha kuja!!! Hivyo basi, ninahofu hata hilo zoezi la hapo kivukoni si endelevu, Tanzania tunapenda sana kufanya mambo kwa matukio kukiandamana na kupiga pesa ndefu, mfuko tu ukikauka na zoezi linakwisha!!!
 
Hil zoezi kwa muda tu..utaniambia.ikipita miez mitatu najisahau maisha yanakua kama kawa no ulinzi no nn..!utaniambia
 
Ukaguzi mwingine wala hauna maana. Siku ya alhamisi tulikwenda hoteli moja mjini kati. Tukakuta mlinzi anakagua wanaoingia kwa zile metal detector. Cha ajabu tukaruhusiwa kuingia baada ya kuscaniwa na hiyo mashine lakini jamaa yangu akanionesha bastola yake tukiwa ndani. Nikabaki najiuliza, ile mashine ilikuwa mbovu au mkaguzi hajui kuitunia. Tuwe serious tunapoamua kukagua watu la hivyo tuache viini macho.
 
Back
Top Bottom