Hongera Job Ndugai

Hongera Job Ndugai

Sasa naanza kuona mwanga kwa mbaali,kama muheshimiwa ameongea kutoka moyoni,basi tunaelekea kuzuri maana amelenga pale pale kwenye goli.
 
Niliwahi kusema CCM wataomba POO tu ktk huu mchakato wa Katiba. Naona huyu katumwa kuanza propaganda za kuwashawishi UKAWA wasizunguke nchi nzima.
 
Maswamediacentre hakika umepigilia msumari wa nchi tano.thumb up!
 
Sababu yoyote iliyofanya akasema hayo sio muhimi. Muhimu ni hayo mawazo aliyotoa. Sasa tunataraji mwanzo mpya. Ukawa kurudi, mijadala yenye upendo, hoja kutoegemea vyama, maamuzi ya pamoja, katiba inayokubalika kwa wote, mawazo ya wachache kupewa nafasi. Nk

Nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani lakini natofautiana kidogo pia.kama wanataka ukawa warudi wakubaliane kwenda kwa wananchi wao waamue wanataka muungano upi, serikali 2 au 3? Pili kifungu cha kura ya wazi kifutwe ibaki kura ya siri.
 
ccm huwa siwaamini kabisa , wana hila mbaya sana hawa watu. Ngoja tutaona mwisho wa hii movie.


Mkuu wanasiasa wote ni watu wa kuchukuliwa kwa tahadhari na kama ingewezekana wawe wanaongea chini ya viapo!!!!!!!!
 
Kinachonishangaza na hao CCM ni kwamba wana mashaka na takwimu za Judge Warioba, that is fine. Lakini kwa busara ya kawaida kama wana maahaka na takwimu, wangemuita Judge Warioba kwenye BMK ili kuzitolea ufafanuzi. Na kama angeshindwa kuwaondolea mashaka basi ndio wangekuwa na haki ya kuziponda. Lakini CCM hawataki kufanya hivyo! Guess why? Kuhusu misimamo ya makundi CCM v UKAWA, mimi ningeshauri kama CCM msimamo wao ni serikali 2 na UKAWA msimamo wao ni serikali 3, basi wengekubaliana NEUTRAL MUUNDO yaani SERIKALI 1. Hiyo ndiyo ingekuwa WIN WIN SITUATION for both CCM AND UKAWA

Hapo kwenye Serikali moja Zanzibar hawataki, wote walioko UKWA na walio CCM. Hapo piga ua HAWAKUBALI. Kwa kweli hata kama ningekuwa mimi. Umejaribu kufurukuta (mf. Jumbe 1984), hatimaye ukapata NCHI KAMILI, urudi tena Sirikali Moja?
 
Nnampongeza Job Ndugai. Namshauri, kama ni Mwanaume kweli na ametoa haya maoni kwa nia njema, akautoe huo ushauri na maoni yake ya kutaka Tanganyika Bungeni na kisha kwenye kikao cha wabunge wa CCM, watakao mwunga mkono waje nje hadharani tuwaone. Siyo waitake Tanganyika sirini kisha waikatae hadharani.
 
Kinachonishangaza na hao CCM ni kwamba wana mashaka na takwimu za Judge Warioba, that is fine. Lakini kwa busara ya kawaida kama wana maahaka na takwimu, wangemuita Judge Warioba kwenye BMK ili kuzitolea ufafanuzi. Na kama angeshindwa kuwaondolea mashaka basi ndio wangekuwa na haki ya kuziponda. Lakini CCM hawataki kufanya hivyo! Guess why? Kuhusu misimamo ya makundi CCM v UKAWA, mimi ningeshauri kama CCM msimamo wao ni serikali 2 na UKAWA msimamo wao ni serikali 3, basi wengekubaliana NEUTRAL MUUNDO yaani SERIKALI 1. Hiyo ndiyo ingekuwa WIN WIN SITUATION for both CCM AND UKAWA

Serikali moja haiwezekani. Wazanzibari utawabeba kwa mbeleko gani?
 
Kama ilivyo mila na desturi yetu mtu akifanya jambo jema katika jamii yake ni jambo la kawaida kumpongeza.wachangiaji wengi wamempongeza job kwa ujasiri mkubwa alioonesha kwa jamii yake kama kiongozi.

Wataalam wengi wanatuambia tamko la kiongozi mmoja mmoja lina nguvu sana kuliko tamko la kikundi chake bila kujali nitamko baya au zuri.

Kwa siku ya leo tukijiandaa kwenda kwenye mkesha wa PASAKA hakika Job Ndugai amezikonga nyoyo za wengi na bila shaka watasherehekea ufufuko wa Yesu kwa furaha na Amani.namtakia pasaka njema mh.naibu spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania mh.Job Ndugai.
 
Mmemsikia prof. Kabudi leo akiwa zanzibar......? Msingi wa muungano, agenda, njozi, na matamanio ya mwalimu.....ameweka kila kitu hadharani na kwkaweli ameshukuru kuitumia kwaresma hii kuuweka ukweli na msingi wa rasimu ya katiba iliyopo mezani....amesema sote ni waja wa mungu, sote tutakufa, na wale wanaotuhukumu leo kwa kupuuza rasimu yao mbele ya umma wote tutahukumiwa kwa haki na kweli mbele ya mungu.

Ni huzuni tbc kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya kongamano muhimu ambalo makamu wa rais wa jamhuri ya muungano anashiriki kisa ni utayari wa prof. Kabudi kuweka bayana kilichochomo kwenye rasimu na msingi wake.....
 
Job Ndugai kwenye issue ya Katiba yuko fame
 
hakuna kitu kibaya ka unafiki....weng ccm wanataka sana Tanganyika irudi tuuu.....at least huyu katupatupa miguu kweny maji mengi kabla ya kufa
 
Mmemsikia prof. Kabudi leo akiwa zanzibar......? Msingi wa muungano, agenda, njozi, na matamanio ya mwalimu.....ameweka kila kitu hadharani na kwkaweli ameshukuru kuitumia kwaresma hii kuuweka ukweli na msingi wa rasimu ya katiba iliyopo mezani....amesema sote ni waja wa mungu, sote tutakufa, na wale wanaotuhukumu leo kwa kupuuza rasimu yao mbele ya umma wote tutahukumiwa kwa haki na kweli mbele ya mungu.

Ni huzuni tbc kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya kongamano muhimu ambalo makamu wa rais wa jamhuri ya muungano anashiriki kisa ni utayari wa prof. Kabudi kuweka bayana kilichochomo kwenye rasimu na msingi wake.....

Prof.kabudi anaudhihirishia ulimwengu kuwa yeye ni msomi na ameelimika.tume ya jaji warioba ilijaa wataalam wenye weredi wa hali ya juu sana!! Nataka nikwambie kuna kijana anaitwa Hamfrey Polepole alikuwa bunge la katiba hakika huyu kijana atakuwa prof wa ukweli.anachambua rasimu mpaka nashiba mwenyewe.

Kuhusu hao Tbc tunaandaa kesi yao baada ya kujilidhisha ili walipa kodi watoe hukumu ni hatua gani ichukuliwe kwa watendaji wakuu wa chombo hicho maana wanonekana nimakada wa ccm
 
Mmemsikia prof. Kabudi leo akiwa zanzibar......? Msingi wa muungano, agenda, njozi, na matamanio ya mwalimu.....ameweka kila kitu hadharani na kwkaweli ameshukuru kuitumia kwaresma hii kuuweka ukweli na msingi wa rasimu ya katiba iliyopo mezani....amesema sote ni waja wa mungu, sote tutakufa, na wale wanaotuhukumu leo kwa kupuuza rasimu yao mbele ya umma wote tutahukumiwa kwa haki na kweli mbele ya mungu.

Ni huzuni tbc kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya kongamano muhimu ambalo makamu wa rais wa jamhuri ya muungano anashiriki kisa ni utayari wa prof. Kabudi kuweka bayana kilichochomo kwenye rasimu na msingi wake.....

Tume ilifanya kazi yake vizuri , kwa weledi na juhudi kubwa. Tatizo ni ukigeugeu na unafiki wa viongozi wetu kuendekeza maslahi binafsi na ya vikundi vyao ndiyo walioharibu mchakato kwa ujumla.

hao tbc hawana maana yoyote kwa mustakabali wa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom