Hongera chief mkuu wa kaya bwana JK

The Hunter

JF-Expert Member
Dec 25, 2010
1,049
305
Nakupongeza Chief, kwa kuwa kiongozi wa nchi hii iliyokaliwa na wanadamu hawa wasiojua wamekosa nini na wasio na udhubutu wakujua wanataka nini!

Hongera
kwa kuwa baba wa mfano unaowakilisha wazazi wasio na muda na familia zao kwani hata Bintio alipopata 4 hukutaka kuwalazimisha NECTA kubadili matokeo, ni wazi wangekuwa hao vilaza wengine kwenye serikali yako matokeo yangekuwa yameshafutwa na kutolewa upya.

Hongera mkuu maana hapa umemkopi mzee Madiba alipoitangazia dunia mwanae wa kiume kafa kwa UKIMWI.

Hongera kwa kutokujali wanamagamba wenzako wanasema nini juu ya mswada wa sheria, hukumjali hata yule kigeugeu Shelukindo.

Hongera Chief kwa kuwa kiongozi wa kwanza kuiround dunia kama huna akili zote huku watendaji wako wachini wakishindwa kumudu hata mlo ule unaoitwa Balance Diet.

Hongera mwana, japo afya ilionyesha mgogoro, ukapiga mtulia mara kibao lakini hukujali, nini bana,chezea misafari ya bwerere huku ukipiga picha na ma starz! saizi unapiga zako ndovu bariidiiiii mkuu kama nakuona vile.

Nini bana unakikwea pipa kila unapoimiss
Mc Donalds (Nikukumbushe wanakitu hii bado hujaonja DOUBLE QUARTER POUNDER WITH CHEESE)

Hongera tena na tena, mgomo, nani anadhurika? uliwaambia hutaki kura zao kwa kimbelembele chao wakakupigia saizi wanataka laki tisa! shwaini wakubwa zitoke wapi?! Eti mkuu zitoke wapi, wanataka usisafiri? ok! waambie una plan B' ya kufanya tujisafari 250 zaidi ili ukawaombee kwa cameroon na kwa mzee obama!

Hongera bana kwa ile kitu pale karibu na bandari ya zamani pale bagamoyo, naona baada ya mabanda ya wale wauza samaki kuteketea mkuu ukaamua kufanya kweli.

Haina kwere ntakucheki Bilila najua bia zao kwa dola tuu! Mpe hi Riz, naona umempiga mkwara aache fujo! alaa! asiigie fujo za Kinje!

NB:

Mkuu usisahau vijisafari vya hapa nchini na africa mkabidhi mzee wa kukata utepe, Injinia wa nuke, afanye maana najua kaafya kake hakamruhusu kutia maguu kwa mama lizabety after all siunajua kajamaa ni ka soshalist.
 
Umuomesha kuwa wewe sio kiongozi unayetumia mabavu kufanikisha unachokitaka.Kwa roho yako ungetamani mtoto afauli ila kutotaka kuingilia mamlaka tumeshuhudia wote.Kwa hili wafaa pongezi mkuu
 
Back
Top Bottom