Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Waziri Ngeleja aliyeachwa katika Wizara ya Nishati na Madini
Khoja ya Zitto Kabwe ya kukosa imani na Waziri Mkuu imepata matumaini makubwa baada ya JK kurudia makosa yaleyale ya kuipuzilia mbali taarifa ya CAG ambayo iliyoweka hadharani matatizo makubwa ya wizi na ubadhirifu katika Wizara (4) za kilimo, Nishati, Viwanda na Biashara na Serikali za mitaa lakini baadhi ya mawaziri au manaibu wao bado kurudishwa kwa maana ya uhamisho tu kwenye nyadhifa zao ikiashiria ya kuwa JK kaiponda taarifa tajwa.
Aidha uteuzi wa Prof. Maghembe kutoka wizara ya kilimo kwenda Maji unazua utata mkubwa na huku aliyekuwa naibu wake Chiza kupandishwa cheo katika wizara ileile kwa kazi chafu ya usimamizi wa wizara tajwa kulingana na taarifa ya CAG unaonyesha jinsi serikali ya JK inavyofanya kazi kwa upendeleo, mashinikizo na ya kuwa haijali maelekezo ya Bunge lake lenyewe.
Uteuzi wa Kighoma Malima aliyekuwa naibu wa Nishati chini ya Ngeleja unazua maswali mengi ambayo hayana majibu kwa sababu baadhi ya manaibu wamewajibishwa lakini huyu na Nyalandu wanaonekana kuwa ni "the untouchables" kwenye hii serikali ya wababaishaji................
Mkuchika na Mwanri nao walivurunda sana wizara ya serikali za mitaa kulingana na taarifa ya CAG lakini JK na Pinda wake wametia pamba masikioni na hivyo kutia dosari kubwa katika zoezi zima la kuwawajibisha watendaji wakuu ndani ya serikali.
Lakini hii siyo mara ya kwanza kwa JK kukaidi maelekezo ya Bunge ambalo wengi wa wabunge wake wanatoka ndani ya chama chake cha ccm. Katika sakata la Richmond/Dowans manaibu kama Ngeleja walinusurika na leo imeonekana kwa uwazi kabisa ya kuwa kuwapandisha manaibu siyo dawa ya matatizo yaliyopo. Hata akina Dr. Hosea hawakuondolewa kule Takukuru kwa kulipotosha Bunge juu ya sakata la Richmond hadi muda wao wa kustaafu ulipofika na watendaji wengine ilikuwa ni pata shika kuwang'oa ikiashiria JK na Pinda wanalidharau bunge kwa kugoma kutekeleza maagizo yake.
Kutokana na upembuzi huo, nionavyo khoja ya kumn'goa Pinda bado ina mashiko manene na inapaswa kuendelea kutiliwa mkazo ili kumshurutisha JK na Pinda wake waache na kukoma kabisa kuiendesha nchi kisanii-sanii hivi