Relief
JF-Expert Member
- Aug 6, 2010
- 254
- 47
Wabunge wa Chama cha NCCR Mageuzi wamegawanyika bungeni jioni ya leo baada ya hoja ya Mh.Tundu Lissu.
Baada ya hoja hiyo, wabunge David Kafulila wa Kigoma Kusini na Felix Mkosamali wa Muhambwe wameungana na wabunge wa CHADEMA kutoka nje huku wabunge Agripina Buyogela na Mosses Machali wamebaki ndani kushirikiana na CCM (MAGAMBA) katika mjadala unaoendelea.
Ni wazi ya kuwa kubaki kwa wabunge hao wawili wa NCCR Mageuzi ndani ya Bunge kujadili jambo ambalo wabunge wenzao wa Upinzani wanalipinga kunadhihirishia Umma jinsi gani wao ni CCM-B na huenda uamuzi wao huo ni maelekezo ya Bw. James Mbatia ambaye huyu ndugu yetu Machali anamtetea muda wote na kuwalaani wenzie kuwa wanakosea kumwondoa madarakani.
Mgawanyiko huu unaleta maswali juu ya wabunge hawa wa upinzani hususan NCCR Mageuzi;
Baada ya hoja hiyo, wabunge David Kafulila wa Kigoma Kusini na Felix Mkosamali wa Muhambwe wameungana na wabunge wa CHADEMA kutoka nje huku wabunge Agripina Buyogela na Mosses Machali wamebaki ndani kushirikiana na CCM (MAGAMBA) katika mjadala unaoendelea.
Ni wazi ya kuwa kubaki kwa wabunge hao wawili wa NCCR Mageuzi ndani ya Bunge kujadili jambo ambalo wabunge wenzao wa Upinzani wanalipinga kunadhihirishia Umma jinsi gani wao ni CCM-B na huenda uamuzi wao huo ni maelekezo ya Bw. James Mbatia ambaye huyu ndugu yetu Machali anamtetea muda wote na kuwalaani wenzie kuwa wanakosea kumwondoa madarakani.
Mgawanyiko huu unaleta maswali juu ya wabunge hawa wa upinzani hususan NCCR Mageuzi;
- Je inawezekana kweli upinzani unatumiwa na MAGAMBA kuleta mpasuko Bungeni kwa faida yao na si ya Umma?
- Je, hali hii iliyojionyesha mapema ya kufarakana kwa NCCR katikati ya mchakato wa kuelekea Katiba Mpya na vyama vingine vya upinzani (TLP na CUF) kukubaliana na CCM juu ya MUSWADA wa Katiba ambao hauonyeshi dhamira ya dhati ya upatikanaji wa TUME adilifu kusimamia uundwaji wa KATIBA MPYA utatupatia KATIBA tunayoitazamia?
- Tutarajie Tanzania gani baada ya mchakato huu kuisha?