Gari ya spika wa bunge hailali nyumbani kwa spika wa bunge je dereva wakati anaenda kumchukua spika wa bunge aweke plate no za spika au anapokuwa hayupo na spika ni sahihi kuweka plate no za spika?
Fatilia kwanza taratibu za protocol then ndo uje uongee
Lakini bado haujajibu swali la msingi.
Hoja haikuwa gari la spika linalala wapi, wala dereva anamchukua nani.
Hoja ni matumizi ya namba za usajili zisizoendana na mwaka wa gari.
Protocol haisimamii usajili wa magari.
Usajili unasimamiwa na sheria za nchi, si hisia wala mazingira ya kazi ya dereva.
Kama gari lina plate number ya mtu fulani au ofisi fulani, basi hilo gari liwe limesajiliwa kihalali kwa plate hiyo bila kujali spika yupo au hayupo ndani ya gari.
Huwezi kubadilisha mantiki ya usajili kwa sababu “dereva anaenda kumchukua mtu”.
Na kama kuna utaratibu maalum wa kiserikali unaoruhusu magari mapya kubeba namba za zamani, basi uelezwe wazi.
Kusema tu “fuata protocol” bila kuonyesha kifungu cha sheria au utaratibu rasmi si jibu, ni kukwepa hoja.
Kwa hiyo swali bado lipo pale pale. Je, haya ni matumizi halali yanayoruhusiwa kisheria, au ni upendeleo unaovumiliwa kimya kimya?
Kama una taarifa sahihi za kisheria au waraka unaoeleza hilo, uweke wazi.
Hoja haimalizwi kwa kauli, inamalizwa kwa ushahidi.