Watakuuliza, kwanini wewe kama mwana CCM unawapa hints CDM? ... watakwambia kuna jambo hapo!Kwa Kanuni ya ushindi: Mshindi ni Mshindi, CCM kupata 50.1% dhidi ya Chadema 49.9%, CCM ni mshindi. Membe au mgombea mwingine yeyote atakayesimamishwa na CCM, hasa wale wote ambao tayari wapo masikioni mwa Watanzania watapita kwa urahisi sana dhidi ya Chadema chini ya kanuni hii ambayo Chadema kwa sababu tusizojua hawaonekani kuwa na jitiada zozote za kuifanyia kazi. Vinginevyo katika siasa za Tanzania kuelekea 2015 zinazotawaliwa na "innocent until proven guilty, lakini muhimu zaidi, guilty only if you dont have money to buy justice, any publicity is good publicity, iwe ya ufisadi, kukamatwa ugoni n.k;
Nianze kwa kukiri kuwa mimi siipendi CCM na ni mpinzani mkubwa wa yeyote yule anayejaribu kwa njia moja ama nyingine kulitetea hili genge la wezi kwa sababu yoyote ile. Pasco, labda mimi niko gizani lakini unapodai kuwa ndani ya CCM kuna "spotless names" unaniacha hoi kwa sababu kwangu naamini kwa dhati kuwa kule kuhusishwa na CCM ni doa tayari.Mkuu Mkandara, alielala, usimwamshe!, ukimwamsha, utalala wewe!. Kama na wewe ni miongoni mwa wanaotaka ukombozi wa pili wa kweli wa Mtanzania ile 2015!, please dont bring to the sptlight these "spotless names", they are not good kwa ukombozi!.
Ndio maana siku zote, nimekuwa nayaepuka majina kama ya kina Dr. Shein, Nahodha, Prof. Tibaijuka, Dr. Asha Rose, and the like!, these names are not good at all!.P.
Kwa Kanuni ya ushindi: Mshindi ni Mshindi, CCM kupata 50.1% dhidi ya Chadema 49.9%, CCM ni mshindi. Membe au mgombea mwingine yeyote atakayesimamishwa na CCM, hasa wale wote ambao tayari wapo masikioni mwa Watanzania watapita kwa urahisi sana dhidi ya Chadema chini ya kanuni hii ambayo Chadema kwa sababu tusizojua hawaonekani kuwa na jitiada zozote za kuifanyia kazi. Vinginevyo katika siasa za Tanzania kuelekea 2015 zinazotawaliwa na "innocent until proven guilty, lakini muhimu zaidi, guilty only if you dont have money to buy justice, any publicity is good publicity, iwe ya ufisadi, kukamatwa ugoni n.k;
MM naomba nichakachue
thread yako kama inavyoendelea kuchakachuliwa.
Mara nyingi natatizika sana kila ninaposoma habari za fulani ni best
candidate.
Hapa ndipo nakubaliana na Mkandara kuwa elimu ya uraia bado ni tatizo
kubwa sana.
Wenzetu wanaojua kuchagua viongozi huangalia kigezo kimoja hadi kingine:
Maadili ya mtu, misimamo yake kisiasa, anasimamia nini, mahusiano na
wenzake, mahusiano na chama chake, ushiriki katikashughuli za kijamii,
maadili yake, mahusiano kati yake na wananchi, mtazamo wake kuhusu nchi,
historia ya utendaji wake, maamuzi aliyowahi kuayafanya huko nyuma,
uthubutu katika kusimamia anachokiamini n.k.
Tunatakiwa twende mbali zaidi ya hapa pa kusema fulani atatusaidia.
Labda nitoe mifano kidogo, ni Membe aliyetuambia kuwa tumeibiwa katika
Radar, ni Membe aliyekataa kutuambia nani ni wezi. Alichotaka ni
ku-score political point kuwa pesa zimerudi! Sasa huyu mtu kimaadili
unamweka kundi gani?
Nina nani miongoni mwetu anayejua misimamo ya Membe kuhusu masuala ya
kitaifa?
Mfano wa pili, ni Lowasa huyu aliyetuambia hakuna wizi Richmond, ni
Lowasa huyu aliyejiuzulu kwa dhambi anayosema hakuitenda, ni Lowasa huyu
anayesema alifanya hivyo kuilinda serikali, ni Lowasa huyo asiyetuambia
nani alibofoa Richmond hadi leo tunapata hasara. Ushujaa wa kusema huyu
ni best candidate unakuwa katika misingi gani?
Ni nani anayeweza kunishawishi kuhusu uadilifu wa Lowasa hadi apewe
ofisi kubwa kiasi hicho?Ni nani anayeweza kutumia vigezo ilivyoweka
kumpa pasi Lowasa japo 60%?
Kama ni suala la kusema tu fulani anafaa basi mimi nasema Sophia Simba
anafaa kama best candidate.
Msiniulize kwa vigezo gani kwasababu lengo ni kutaja tu.
Membe alivyo handle mambo ya Libya na Arab spring kwa ujumla, kauli zake ktk media Naye hafai.Kwani kama ni Kashfa tayari kumtetea Ghaddafi kipindi waLibya wakifa, kumtetea hadi kumfanya awe Mwenyekiti wa AU.Baadaye kujulikana kuwa hela ya Libya ilitumika sana kuwafanya viongozi wetu kuwa wapambe wa Ghaddafi.Atakuweje rais wetu huyu katk dunia inayohitaji umahiri na ujasiri katk kila maamuzi,ataishia kuwapa amri watu wa ndani kwa nguvu zote .Amri zilizotoka kwa watawala wa nchi nyingine.Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"
CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.
Ni kweli?
Watakuuliza, kwanini wewe kama mwana CCM unawapa hints CDM? ... watakwambia kuna jambo hapo!
Watakuuliza, kwanini wewe kama mwana CCM unawapa hints CDM? ... watakwambia kuna jambo hapo!
Hypothetical question: akisimama Zitto na Edward Lowassa utampa kura nani?Natoa hints za kuboresha demokrasia chini ya Dhana ya Tanzania Kwanza, Siasa baadae; Isitoshe, nionavyo mimi, katika siasa, hakuna kitu chenye kuleta faraja moyoni zaidi ya ufahamu kwamba umeshinda kihalali, umeshinda ndani ya mazingira yanayo heshimu sheria, umeshinda huku ukiwa unaheshimu haki za raia, na umeshinda bila ya kuitia doa demokrasia; Nitaiunga mkono CCM yenye mtazamo wa namna hii, vinginevyo iwapo Mwasisi wa CCM (Nyerere) aliwahi sema CCM sio mama yake, na anaweza kuachana nayo wakati wowote, kwa mtu mdogo kama mimi, nipo tayari kujiunga na chama chochote kinachokidhi hayo juu, Chadema ikiwa kimoja wapo, au CCM itakayojirekebisha kabla ya 2015;
Ila mimi kama jirani yako na unaniuliza kama ukileta wi-Fi litakuwa jambo la maana, mimi nitasema poa tu!Na kuna jambo kweli..CDM imefika hapo bila ushauri wa mwana CCM leo iweje CCM wajidai kutoa ushauri kwa CDM na si kwa NCCR,ADP na wengine?Yupo Jirani yangu kila siku ni mshauri wangu ila juhudi zake za kuniangusha kila mtu anaziona.Baada ya kutoka hatua chache.
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"
Mzee Mwanakijiji,
Umeshafanya mahojiano na mtu wako?
Amekwambia, amekuomba umpigie chapuo?
Kwa wale wanaofatilia mada zako za muungano wataelewa sera ipi ya muungano unaisimamia. Serikali moja.
Kutoka serikali mbili kuelekea moja.
Natumai umeanza kufunguka. Je utampatia kura yako Membe atakapochaguliwa kuwa mgombea wa chama unachokipigia debe?
Kuna thread ya zamani alianzisha, yaya au yoyo kuhusu wewe, bado naikumbuka vyema.
Hawa ndio wanaharakati wetu wa JF, wanatuhamasisha tutoe maoni ya kudai serikali moja na leo wanatwambia Membe atashinda uchaguzi mkuu 2015, CCM itashinda.
Nashindwa hata kushangaa.
Changuzi zilizopita je zilikidhi hivi vigezo ulivyojiekea? Au vigezo hivi utaanza kuvitumia 2015?Natoa hints za kuboresha demokrasia... katika siasa, hakuna kitu chenye kuleta faraja moyoni zaidi ya ufahamu kwamba umeshinda kihalali, umeshinda ndani ya mazingira yanayo heshimu sheria, umeshinda huku ukiwa unaheshimu haki za raia, na umeshinda bila ya kuitia doa demokrasia; Nitaiunga mkono CCM yenye mtazamo wa namna hii,..
Hypothetical question: akisimama Zitto na Edward Lowassa utampa kura nani?
Mind you, wewe bado upo CCM>