Hoja binafsi: Nawapa changamoto BAVICHA, muda wa kuiua CCM ni huu chukueni hatua

Albedo

JF-Expert Member
Feb 24, 2008
5,559
1,452
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni Chama Kilichofanikiwa kwa kiasi kikubwa kujipambanua kama Chama kinachopigania Maslahi ya Uma, na Kwa Bahati nzuri Kimeeleweka hivyo machoni mwa uma, na ikumbukwe namna Nguvu ya Uma ilivyofanikisha kwa Wabunge zaidi ya Ishirini (2) wa CHADEMA katika Uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2010. Ni Chama ambacho kimeonekana kujizolea Uungwaji Mkono Mkubwa katika Kada Mbali Mbali, Kuanzia Watoto wa Shule za Msingi mpaka wazee!
Ni Chama ambacho kinazidi kukua ( Kwa maana ya Kuvutia zaidi Vijana) tofauti na CCM ambacho kinaelekea kufa kutokana na Kuchukiwa na Vijana wengi ( Chama kisipoungwa na mkono na Vijana Mwisho wake ni Kifo tu)
Toka kuanzishwa kwake kimefanya Jitihada nyingi sana katika Kuhakikisha kinapata Wanachama wengi kila pembe ya Nchi. Mifano ya Kampeni ilizowahi kufanya ni pamoja na Operesheni Sangara ambayo kwa Kiasi Kikubwa Ilisaidia kukitambulisha chama hicho hata kuweza kuipa JambaJamba CCM katika uchaguzi uliopita!

Je Wakati wa CHADEMA kuiua CCM Umefika? Na kama Umefika Silaha gani CHADEMA iitumie? Majibu ni Rahisi sana
1: Ndiyo Muda wa CHADEMA kuiadhibu na kuiua CCM umefika, CHADEMA wamepewa Fursa ya Buren a Wananchi na CCM yenyewe, CCM imejipeleka machinjioni na kuweka Kichwa chake kwenye Gogo la kuchinjia na CHADEMA wameshika shoka. Swali ni Je nani kwa Mtazamo wako asushe Shoka hilo kwenye Kisusio kiitwacho CCM?
Naamini wanaopaswa kufanya Hivyo si Mbowe, si Slaa, Si Baregu wala si Arfi, Bali Wanaopaswa Kufanya Hivyo ni Jeshi la BAVICHA likiongozwa na Makamanda kama Halima Mdee, Zitto Kabwe, John Mnnyika, John Mrema, David Silinde, Godbless Lema, MsandoAlberto na Wengine.
Nashauri CHADEMA Waanzishe “Operesheni Mavuno”, na Main Objective ya Operesheni hiyo iwe ni “Maziko ya CCM”. Waitangaze na Waikabaidhi kazi hiyo kwa BAVICHA. Naamini BAVICHA iliyo na Nguvu itaweza kuwavutia zaidi vijana Wengi Zaidi kujiunga na kuwa Wanachama wa CHADEMA
Naomba CHADEMA wasiipoteze Fursa hii Adhimu Kabisa, CCM wanakaribia Kufa na Hawapaswi waachwe wafe Natural Death, wanapaswa kufa kifo cha Aibu, Kifo cha Kukataliwa. Kazi Hiyo BAVICHA wanaiweza wakabidhini.
 
Well said mkuu, Bavicha ichaguwe uongozi wenye vision ili wasije kuharibu taswira ya chama iliyojijengea na kuaminiwa na umma, mpaka sasa watu wanaipenda CHADEMA kutoka mioyoni mwao lakini sio kwa kupewa Tshirt na kanga au posho, na hapa Dar es salaam ndio mkoa unoongoza Tanzania kwa wajinga, kwahiyo inabidi ifanyike kazi ya ziada kwa sababu CCM bado mtandao ni mkubwa licha ya kutokupendwa lakini bado wana miradi ile ya kulaza magari na ndio inayowafanya ukifika uchaguzi wao wa ndani waanze kutoana roho. halafu mimi bahati mzuri uchaguzi uliopita nilishiriki vilivyo, bado organisation ya chama sio nzuri sana, maofisa wa kuzungukia maeneo wakati wauchaguzi kwa upande wa jimbo na kata yangu walifeli, pili hakukuwa na mtu alikyekuwa anapita kuchukuwa matokeo ya urais, wote tulikuwa tumeyatolea macho matokeo ya udiwani na ubunge, ili eneo ndilo CCM wanajuwa kulicheza vizuri kuliko eneo lingine lolote. nina mengi ya kueleza hapa lakini nitawachosha wasomaji. yangu machache ni hayo tu.
 
BAVICHA Mungu awape nini tena? Gunia la Chawa?

UVCCM: Dk. Slaa chaguo la vijana
• Wafichua jinsi viongozi wao wa kitaifa wanavyotumiwa na mafisadi

na Grace Macha, Moshi


amka2.gif
UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kilimanjaro (UVCCM) umeushutumu uongozi wa kitaifa wa umoja huo kwa kuwa dhaifu kiasi cha kusababisha vijana wengi nchini kumpa kura zao aliyekuwa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa.
Viongozi wa kitaifa wa umoja huo wametakiwa kujiuzulu kwenye nafasi zao kwa sababu ya kile kilichoelezwa kuwa wameshindwa kuongoza na badala yake wamekuwa wakitumiwa na mafisadi kutoa matamko ya kuwashambulia wanaopambana na ufisadi nchini.
Pia uamuzi wa kumteua kada wa siku nyingi wa CCM, Kingunge Ngombale- Mwiru, kuwa kamanda wa umoja huo umepingwa kwa madai kuwa hana sifa, kwani ameshapoteza umashuhuri na hawezi kwenda na kasi ya changamoto, kwa madai kuwa atapinga kila wazo jipya la manufaa ndani ya jumuiya hiyo.
Hayo yalisemwa juzi na mjumbe wa mkutano wa mkoa wa UVCCM mkoani Kilimanjaro, Paul Makonda, alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kwenye Hoteli ya Crane mjini Moshi.
Alisema viongozi wa UVCCM taifa ndio waliosababisha vijana wengi kujiunga, kukishabikia na kukipigia kura nyingi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita baada ya kushindwa kutoa mwelekeo na tumaini kwa vijana, jambo alilosema kuwa ndilo limechangia kuinyima CCM kura za vijana.
“UVCCM waseme gharama kubwa waliyoitumia katika kampeni za uchaguzi wa mwaka jana kulipia watoto wa vigogo kuzunguka nchi nzima kwa kisingizio cha kupiga kampeni zimeleta manufaa yapi? Iweje watu wanazunguka nchi nzima na mwishowe kundi kubwa la vijana wanakimbia kutoka CCM na kutua CHADEMA? Je, huu si usaliti wa wazi kufukuza vijana chamani na kuwapeleka CHADEMA?” alihoji Makonda huku akishauri viongozi waachie ngazi kwa ustawi wa UVCCM.
Alisema uongozi wa kitaifa wa UVCCM umejipambanua kama mawakala wa ufisadi kwa tabia yake ya kutoa matamko ya mara kwa mara yasiyo na tija kwa taifa zaidi ya kuwashambulia viongozi waandamizi na wastaafu wanaopinga ufisadi nchini.
Kwamba, hatua ya viongozi wa kitaifa wa UVCCM kuitaka sekretarieti ya CCM itoke madarakani inaashiria kuwa ni mambumbu wasiojua vema majukumu ya jumuiya za CCM.
“Wanasema viongozi wa serikali na wastaafu ambao CCM inawaheshimu na kuwapa nafasi Sitta (Samuel, Waziri wa Afrika Mashariki ) na Waziri Mkuu mstaafu Sumaye (Frederick) kuwa wanakosea kuongea nje ya vikao huku nao UVCCM wakitumia vyombo vya habari kuwakosoa nje ya vikao, jambo linaloonyesha uwezo wao kiutendaji ni mdogo,” alisisitiza Makonda.
Alisema kuwa aliamua kujitoa mhanga kulizungumzia hilo baada ya kuona vijana wenzake kutoka Mkoa wa Kilimanjaro na maeneo mbalimbali nchini hawakubaliani na namna mambo yanavyokwenda ndani ya umoja huo lakini wanashindwa kupinga kutokana na hofu ya kushughulikiwa.
Makonda alisema kuwa anguko la UVCCM kwa sasa linaonekana dhahiri kutokana na namna uongozi ulio chini ya Kaimu Mwenyekiti wake, Benno Malisa na Katibu Mkuu wake, John Shigela, ulivyokosa dira na mwelekeo, hali inayoifanya UVCCM ikose sifa ya kuwa jumuiya ndani ya CCM.
Alisema UVCCM imekuwa kama chama cha upinzani ndani ya CCM, akitolea mfano wa hatua ya umoja huo kupinga maaamuzi ya sekretarieti ya kumrudishia uanachama wa jumuiya hiyo Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Nape Nnauye, jambo alilowashauri kama wanashindwa kukubaliana na maamuzi sahihi ya CCM ni vema wakaachia ngazi na kuanzisha chama chao cha siasa.
“Hata kama kutumiwa huku kwa UVCCM ni kwa kwanza kuonekana duniani na kwa style hii misingi ya amani na utulivu inatikiswa kutokea ndani, ni nani atazuia …wanasema watafanya maandamano nchi nzima endapo mtu wanayemtaka kwa nafasi ya urais 2015 hapitishwi na chama, hivi hawa watu wana lengo zuri kweli? Kwa nini wasifanye maandamano kupinga malipo ya shilingi bilioni 94 ya Kampuni ya Dowans Tanzania Limited?” alihoji Makonda.
Aidha, alipinga uteuzi wa Hussein Bashe aliyedai mpaka sasa bado hajatoa majibu ya msingi juu ya utata wa uraia wake, halafu anapewa jukumu la kufanya utafiti wa mabadiliko ya kimuundo ya umoja huo, kwa madai kuwa hiyo ni mbinu na mkakati maalumu wa kusaka uongozi wa UVCCM 2012 na kwamba wanajiwekea mazingira ya kumpata rais wanayemtaka ateuliwe na CCM kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa 2015.
“Mambo haya ndiyo yanasadifu uwezo mdogo wa kuamua mambo ya msingi ya vijana wa chama na taifa hili, badala yake unadhihirisha uwezo mkubwa wa kuamua mambo kwa maslahi ya mafisadi wachache ndani ya taifa hili.
“Na kwa vile viongozi wa UVCCM wanafanya kazi kwa maslahi ya mafisadi, basi hakuna dhambi nao wakijumuishwa kwenye kundi la mafisadi na waachie nafasi hizi ndani ya jumuiya na ndani ya CCM, waende wakaunde taasisi zao watakazofanya watakavyo,” alisema Makonda.
Mwanachama huyo wa UVCCM alishauri suala la kufanya utafiti wa kimuundo wa jumuiya hiyo lifanywe na wasomi au taasisi huru zenye wataalamu wasiofungwa na chama chochote, ambao watafanya utafiti kubaini walishindwa wapi na wafanye nini ili waweze kusonga mbele.


 
Good CHADEMA, Jina Zuri cha Msingi mtekeleze

Vyuo vikuu Chadema waja na `washa taa mchana`




Na Gideon Mwakanosya
Chadema%2858%29.jpg

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)



Vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali nchini wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wamezindua kampeni waliyoipa jina la ‘washa taa mchana’, itakayoendeshwa nchi nzima, yenye lengo la kuleta ukombozi wa kifikra kwa wananchi.
Akizungumza kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika jana mjini hapa, Mratibu wa kampeni hiyo mkoa wa Ruvuma, Likapo Bakari, alieleza kuwa taa hiyo itawashwa rasmi Machi 26 mwaka huu, ikiwa na lengo la kumulika na kuangaza katika kila mkoa nchini ili kuleta ukombozi kwa Watanzania
Alisema kuwa, ukombozi huo utakuwa katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa na kwamba itaanzia mkoa wa Ruvuma kwa kufanya mikutano mbalimbali ya hadhara katika kata zote za Manispaa ya Songea, kwa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi wa eneo husika ili waweze kuzijua haki zao, kuzitetea na kuzidai.
Aliongeza kusema kuwa, kupitia mikutano hiyo pia watahamasisha jamii namna ya kutumia vizuri rasilimali za taifa katika kujiendeleza na kujiongezea kipato na kuwaelimisha maana ya katiba ya nchi na umuhimu wa kudai katiba mpya.
Akizindua kampeni hiyo, Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Ruvuma, Joseph Fuime, alisema maendeleo yoyote hayawezi kufikiwa bila ya kuwepo kwa siasa safi, hivyo wameanzisha kampeni hiyo itakayoendeleza, kukuza na kukitangaza chama kila kona ya nchi na kufungua matawi mapya.
 
Well said mkuu, Bavicha ichaguwe uongozi wenye vision ili wasije kuharibu taswira ya chama iliyojijengea na kuaminiwa na umma, mpaka sasa watu wanaipenda CHADEMA kutoka mioyoni mwao lakini sio kwa kupewa Tshirt na kanga au posho, na hapa Dar es salaam ndio mkoa unoongoza Tanzania kwa wajinga, kwahiyo inabidi ifanyike kazi ya ziada kwa sababu CCM bado mtandao ni mkubwa licha ya kutokupendwa lakini bado wana miradi ile ya kulaza magari na ndio inayowafanya ukifika uchaguzi wao wa ndani waanze kutoana roho. halafu mimi bahati mzuri uchaguzi uliopita nilishiriki vilivyo, bado organisation ya chama sio nzuri sana, maofisa wa kuzungukia maeneo wakati wauchaguzi kwa upande wa jimbo na kata yangu walifeli, pili hakukuwa na mtu alikyekuwa anapita kuchukuwa matokeo ya urais, wote tulikuwa tumeyatolea macho matokeo ya udiwani na ubunge, ili eneo ndilo CCM wanajuwa kulicheza vizuri kuliko eneo lingine lolote. nina mengi ya kueleza hapa lakini nitawachosha wasomaji. yangu machache ni hayo tu.

Penye RED nilitaka kuwapa changamoto. kama kizazi kipya ni vizuri wawe na mtazamo chanya wa kukifanya Chadema iwe na muundo na sura ya kitaifa na sio kama ilivo sasa ina sura na muundo wa kikanda, kikabila na kidini.

Hiyo ni changamoto kubwa sana kwenu Baavicha.
 
Penye RED nilitaka kuwapa changamoto. kama kizazi kipya ni vizuri wawe na mtazamo chanya wa kukifanya Chadema iwe na muundo na sura ya kitaifa na sio kama ilivo sasa ina sura na muundo wa kikanda, kikabila na kidini.

Hiyo ni changamoto kubwa sana kwenu Baavicha.

Hapo kwenye RED hiyo ndio sifa ya CCM mwenyekiti JK MZARAMO ( MAANA MODS WAMESHALIHUJUMU HILI JUKWAA UKIANDIKA ****** WAO WANAWEKA NYOTA NA SIO ULICHOANDIKA ) ni mwislamu na anatoka ukanda wa pwani, katibu mkuu ni Yusuf Makamba, ni Mwislamu na anatoka ukanda wa pwani, kwahiyo CCM ndio chama cha kikanda na kidini na sasa hivi mmempata na yule Mufti Simba aliyeishia darasa la saba.
 
Well said mkuu, Bavicha ichaguwe uongozi wenye vision ili wasije kuharibu taswira ya chama iliyojijengea na kuaminiwa na umma, mpaka sasa watu wanaipenda CHADEMA kutoka mioyoni mwao lakini sio kwa kupewa Tshirt na kanga au posho, na hapa Dar es salaam ndio mkoa unoongoza Tanzania kwa wajinga, kwahiyo inabidi ifanyike kazi ya ziada kwa sababu CCM bado mtandao ni mkubwa licha ya kutokupendwa lakini bado wana miradi ile ya kulaza magari na ndio inayowafanya ukifika uchaguzi wao wa ndani waanze kutoana roho. halafu mimi bahati mzuri uchaguzi uliopita nilishiriki vilivyo, bado organisation ya chama sio nzuri sana, maofisa wa kuzungukia maeneo wakati wauchaguzi kwa upande wa jimbo na kata yangu walifeli, pili hakukuwa na mtu alikyekuwa anapita kuchukuwa matokeo ya urais, wote tulikuwa tumeyatolea macho matokeo ya udiwani na ubunge, ili eneo ndilo CCM wanajuwa kulicheza vizuri kuliko eneo lingine lolote. nina mengi ya kueleza hapa lakini nitawachosha wasomaji. yangu machache ni hayo tu.
Kigezo gani umetumia kusema dar ina wajinga wengi hapa Tanzania wakati tuna wabunge wawili na mmoja alichakachuliwa....tatizo la watu wengi dar misheshe mingi hata kufatilia vyombo vya habari wengine inakuwa shida maana mida hiyo huwwa kwenye vyombo vya usafiri ama wakilejea makwao au wakienda kibaruani....
 
Hapo kwenye RED hiyo ndio sifa ya CCM mwenyekiti JK MZARAMO ( MAANA MODS WAMESHALIHUJUMU HILI JUKWAA UKIANDIKA ****** WAO WANAWEKA NYOTA NA SIO ULICHOANDIKA ) ni mwislamu na anatoka ukanda wa pwani, katibu mkuu ni Yusuf Makamba, ni Mwislamu na anatoka ukanda wa pwani, kwahiyo CCM ndio chama cha kikanda na kidini na sasa hivi mmempata na yule Mufti Simba aliyeishia darasa la saba.

Kubali au kataa lakini ukweli upo pale pale.

Chadema kimejikita zaidi na kina sura dhahiri kabisa ya Ukanda na Udini.

Changamoto kwa hawa vijana hususan katika uchaguzi na mwelekeo wao waliangalie hilo
 
Kubali au kataa lakini ukweli upo pale pale.

Chadema kimejikita zaidi na kina sura dhahiri kabisa ya Ukanda na Udini.

Changamoto kwa hawa vijana hususan katika uchaguzi na mwelekeo wao waliangalie hilo
CCM ni chama cha KIISLAMU sasa hivi, katibu mwenezi ni mufti Shaaban bin Simba yule ambaye ameishia darasa la saba.
 
Back
Top Bottom