The Future.
Member
- Jan 7, 2011
- 71
- 0
Kwa heshima taadhima natumia nafasi kujitambulisha hapa na kuomba kuwa mmoja wenu katika kuchangia mada mbalimbali, nimekua nikipitia mtandao huu mara kwa mara na nimekua nikijifunza mengi kutoka humu. Hongera sana kwa uongozi mzuri wa mtandao huu ambao umekua na hadhi ya kukubalika na kuheshimika sana. Naomba kujiunga ili niweze endelea kujifunza mengi kutoka kwa wataalam mbalimbali waliopo hapa. Mwisho kabisa natoa pole zangu za dhati kwa uongozi wa chadema, wanachama na watanganyika wote kwa ujumla hasa wafiwa na wahanga wa udhalimu wa serikali na jeshi la polisi kwa yaliyotokea arusha. Mungu awatie moyo na ujasiri hasa katika kipindi hiki kigum. Asanteni sana.