Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,186
- 10,922
Israel imezidi kuonesha unyama wake na kibri kilichopitiliza ada kwa kukataa kufungua mpaka wa Rafah ili raia wa nchi rafiki zake waweze kuondoka Gaza.
Waziri wa mambo ya nje wa Misri amesema malori mengi ya misaada ya kibinadamu yapo mpakani tayari kuingia Gaza na upande wao uko wazi kwa misaada hiyo kuendelea na safari,tatizo upande wa pili ndani ya Gaza ambako Israel ndiyo yenye mamlaka wamekataa kufungua mpaka.
Sambamba na hilo raia waliokushanyika kwa msongamano mkubwa wa kibinadamu upande huo wa kusini ya Gaza wameendelea kupigwa kwa mabomu ya kutoka angani huku wakiwa hawana maji ya kutosha,chakula wala umeme.
Upande wa kaskazini ya Israel kwenye mpaka na Lebanon wanamgambo wa Hizbulah wameziharibu kamera kadhaa za vituo vya kijeshi vya Israel ambazo kazi zao ni kuangalia harakati zote za kuvuka mpaka kutoka kusini ya Lebanon kuingia nchini humo.
Inavyoonekana kwa sasa Marekani imetishika sana na kiburi cha Israel ikiona kama kwamba itawaharibia maslahi yao pia.Hilo linaonekana katika nenda rudi ya wanadiplomasia wa Marekani kuzungumza na Israel kuhusiana na kiburi chake cha kujifanya hataki kumsikiliza yeyote.
Mshirika mwengine muhimu wa Marekani ambayo ni mlinzi wa Israel ni Saudi Arabia. Kuonesha kukasirika kwa mwanamfalme Mohammed Suleiman, alimuacha Antony Blinken kwenye ukumbi kwa masaa akimsubiri bila kutokea mpaka pale Blinken alipochoka na wala hakujitokeza kuzungumza naye ikabidi aondoke tu.
Waziri wa mambo ya nje wa Misri amesema malori mengi ya misaada ya kibinadamu yapo mpakani tayari kuingia Gaza na upande wao uko wazi kwa misaada hiyo kuendelea na safari,tatizo upande wa pili ndani ya Gaza ambako Israel ndiyo yenye mamlaka wamekataa kufungua mpaka.
Sambamba na hilo raia waliokushanyika kwa msongamano mkubwa wa kibinadamu upande huo wa kusini ya Gaza wameendelea kupigwa kwa mabomu ya kutoka angani huku wakiwa hawana maji ya kutosha,chakula wala umeme.
Upande wa kaskazini ya Israel kwenye mpaka na Lebanon wanamgambo wa Hizbulah wameziharibu kamera kadhaa za vituo vya kijeshi vya Israel ambazo kazi zao ni kuangalia harakati zote za kuvuka mpaka kutoka kusini ya Lebanon kuingia nchini humo.
Inavyoonekana kwa sasa Marekani imetishika sana na kiburi cha Israel ikiona kama kwamba itawaharibia maslahi yao pia.Hilo linaonekana katika nenda rudi ya wanadiplomasia wa Marekani kuzungumza na Israel kuhusiana na kiburi chake cha kujifanya hataki kumsikiliza yeyote.
Mshirika mwengine muhimu wa Marekani ambayo ni mlinzi wa Israel ni Saudi Arabia. Kuonesha kukasirika kwa mwanamfalme Mohammed Suleiman, alimuacha Antony Blinken kwenye ukumbi kwa masaa akimsubiri bila kutokea mpaka pale Blinken alipochoka na wala hakujitokeza kuzungumza naye ikabidi aondoke tu.