Joe Biden kwenda Israel kesho

Mhaya

JF-Expert Member
Aug 20, 2023
1,658
4,866
Rais wa Marekani Joe Biden anatarajiwa kutembelea Israel kesho Jumatano katika kile kilichoripotiwa kuwa ni kuthibitisha kujitolea kwa Marekani kwa usalama wa Israel, hatua hiyo inakuja huku Israel ikipewa wito wa kufungua njia kuruhusu misaada kuingia Gaza.

Kwa mujibu wa majasusi nilionao White house wamenitaarifu kuwa ziara hiyo ya Rais Joe Biden wa Marekani nchini Israel kesho Jumatano imetangazwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken leo Jumanne.

Blinken amesema Rais Biden atathibitisha tena uungwaji mkono thabiti wa Marekani kwa Israel na kujitolea kwa Marekani kwa usalama wa Israel huku akisema Israel ina haki na wajibu wa kuwalinda Raia wake dhidi ya Hamas na makundi mengine ya kigaidi na kuzuia mashambulizi ya siku za usoni.

Blinken amesema, amekubaliana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuhusu mpango utakaowezesha misaada ya kibinadamu kuwafikia raia ndani ya Gaza, Blinken aliyerudi Israel baada ya ziara katika baadhi ya Mataifa ya Kiarabu kwenye Kanda hiyo, alifanya mazungumzo ya zaidi ya saa sita na Baraza la Mawaziri la Vita la Israel, hadi usiku wa manane.

Akiongea baada ya kukutana na Blinken, Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant alisema “Hivi vitakuwa vita vya muda mrefu, gharama itakuwa kubwa lakini tutashinda kwa ajili ya Israeli na Wayahudi na kwa maadili ambayo nchi zote mbili (Israel na Marekani) zinaamini.”
 
Yaani inawezekana hata hyo aliyefanya mashambulizi amepekekwa na mmarekani ili wapate sababu ya kumpiga mlengwa wao USA mjanja sana.
 
Yaani inawezekana hata hyo aliyefanya mashambulizi amepekekwa na mmarekani ili wapate sababu ya kumpiga mlengwa wao USA mjanja sana.
Yaani inawezekana hata hyo aliyefanya mashambulizi amepekekwa na mmarekani ili wapate sababu ya kumpiga mlengwa wao USA mjanja sana.
Ndo hivyo asee... Kesho Navy Force tutakuwepo pale Israel tunakinukisha
 
Rais wa Marekani Joe Biden anatarajiwa kutembelea Israel kesho Jumatano katika kile kilichoripotiwa kuwa ni kuthibitisha kujitolea kwa Marekani kwa usalama wa Israel, hatua hiyo inakuja huku Israel ikipewa wito wa kufungua njia kuruhusu misaada kuingia Gaza.

Kwa mujibu wa majasusi nilionao White house wamenitaarifu kuwa ziara hiyo ya Rais Joe Biden wa Marekani nchini Israel kesho Jumatano imetangazwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken leo Jumanne.

Blinken amesema Rais Biden atathibitisha tena uungwaji mkono thabiti wa Marekani kwa Israel na kujitolea kwa Marekani kwa usalama wa Israel huku akisema Israel ina haki na wajibu wa kuwalinda Raia wake dhidi ya Hamas na makundi mengine ya kigaidi na kuzuia mashambulizi ya siku za usoni.

Blinken amesema, amekubaliana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuhusu mpango utakaowezesha misaada ya kibinadamu kuwafikia raia ndani ya Gaza, Blinken aliyerudi Israel baada ya ziara katika baadhi ya Mataifa ya Kiarabu kwenye Kanda hiyo, alifanya mazungumzo ya zaidi ya saa sita na Baraza la Mawaziri la Vita la Israel, hadi usiku wa manane.

Akiongea baada ya kukutana na Blinken, Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant alisema “Hivi vitakuwa vita vya muda mrefu, gharama itakuwa kubwa lakini tutashinda kwa ajili ya Israeli na Wayahudi na kwa maadili ambayo nchi zote mbili (Israel na Marekani) zinaamini.”
wanapambana kutafuta namna ya kuachia mateka. wakifanikiwa lolote laweza kutokea. wakiwachinja, pale gaza patakuwa majivu kama ya sodoma.
 
Rais wa Marekani Joe Biden anatarajiwa kutembelea Israel kesho Jumatano katika kile kilichoripotiwa kuwa ni kuthibitisha kujitolea kwa Marekani kwa usalama wa Israel, hatua hiyo inakuja huku Israel ikipewa wito wa kufungua njia kuruhusu misaada kuingia Gaza.

Kwa mujibu wa majasusi nilionao White house wamenitaarifu kuwa ziara hiyo ya Rais Joe Biden wa Marekani nchini Israel kesho Jumatano imetangazwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken leo Jumanne.

Blinken amesema Rais Biden atathibitisha tena uungwaji mkono thabiti wa Marekani kwa Israel na kujitolea kwa Marekani kwa usalama wa Israel huku akisema Israel ina haki na wajibu wa kuwalinda Raia wake dhidi ya Hamas na makundi mengine ya kigaidi na kuzuia mashambulizi ya siku za usoni.

Blinken amesema, amekubaliana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuhusu mpango utakaowezesha misaada ya kibinadamu kuwafikia raia ndani ya Gaza, Blinken aliyerudi Israel baada ya ziara katika baadhi ya Mataifa ya Kiarabu kwenye Kanda hiyo, alifanya mazungumzo ya zaidi ya saa sita na Baraza la Mawaziri la Vita la Israel, hadi usiku wa manane.

Akiongea baada ya kukutana na Blinken, Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant alisema “Hivi vitakuwa vita vya muda mrefu, gharama itakuwa kubwa lakini tutashinda kwa ajili ya Israeli na Wayahudi na kwa maadili ambayo nchi zote mbili (Israel na Marekani) zinaamini.”
kati ya marais wasio na maana Marekani iliwahi kuwa nao, Biden ni mmoja wapo.
 
Back
Top Bottom