Hivi Wanawake wote mpo kama huyu?

prospa

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
554
156
Jamani wanajamvi msaada tutani , mke wangu ananishangaza sana.

Kabla sijamuoa nilimpa taarifa kuwa nina mtoto na akakubali kuwa atamlea kama mwanaye na akashauri nimchukue kutoka kwa mama yake ili tuishi naye sasa siku zikawa zinakatika mtoto umri umesogea na mda wa kwenda shule umefika ikabidi niende kumchukua.

Ila tukakubaliana kuwa nimwache kwa mama yangu kwanza , to cut story short nilikuta kwa mama mazingira si mazuri kwani mama ni mtu yupo bize sana na kazi zake ni mwajiriwa pia kilimo na mengineyo nikaona mda wa kumwangalia mtoto utakuwa mchache nikabadaili mawazo nikaja naye ninakoishi.

Nilipofika naye nikampa taarifa kwanini sikumwacha mtoto na kuamua kuja naye ikawa ni ugomvi kwenda mbele kila mtoto anachokifanya kwake ni kibaya.

Kila ntachomfanyia mtoto anasema namdekeza kwa kweli mimi kama baba naumia sana kwani sina hata nafasi ya kumsaidia mtoto wangu kumjenga kifikra na kimawazo.

Kwani nikitoka naye tu inakuwa nongwa nikaa naye kwenye kochi nongwa nikila naye nongwa , nina watoto wawili mmoja nimezaa naye na bado mdogo sana hajaanza kuongea na bahati nzuri wote wa kiume sasa nafikiria mambo mawili matatu ambayo ndiyo nahitaji ushauri kwenu.

1. Je nimpeleke mtoto boarding school mpaka mdogo wake akuwe ili niwe natoka / au nakaa nao pamoja kwan nataman kuwajenga wanangu kimaadili mapema?

2.Nimpeleke tu akaishi kwa bibi yake rejea hapo juu kuhusu mama yangu na ufinyu wa nafasi ya kulea mtoto mdogo kwan sisi wote watoto wake tushaanza kujitegemea?

3.Nivumilie tu labda ipo siku atajirudi kwan ashaniambia kuwa moyo wake umeshindwa kabisa kumkubali mtoto wangu huyu na anadai nimemsababishia shambulio la moyo kwa mawazo?

4. Naipenda familia yangu , nampenda mke na watoto wote sipendi kumpoteza hata mmoja, je nifanyeje wadau nipo njia panda?

Kwa hayo machache naitaji busara zenu zaid , hii sio hadith nio maisha halisi ya mtu hivyo utani tupa kule changia mawazo ya busara kama huna cha kuchangia naomba upite wima sio lazima kuandika.


ASANTEN KWA KUNISIKILIZA, NAWASILISHA.
 
Pole sana kwa matatizo yako......huyo mwanamke mwanzangu ni kigeu geu kabisa na trust me ukilazimisha mwanao akae hapo basi ujue atateseka sana. Maadam kashakwambia "moyo wake umekataa kumkubali mwanao" basi ni lazima ufanye maamuzi magumu kwa ustawi wa mtoto wako. Ungekua hujamwambia habari ya mtoto wako kabla hujamuoa labda ningeweza kuelewa kwa nini anafanya hivyo japo isingekua kigezo cha kumchukia mtoto asiye na hatia.

Na kinachonishangaza zaidi na yeye ni mwanamke na amezaa......hivi kesho au keshokutwa na yeye akiwa hayupo na akisikia mtoto wake anafanyiwa hivyo anavyomfanya yeye mtoto wa mwenzie atajisikiaje.

Mi ninachoweza kukushauri kwa sasa kaongee na mama yako maana mzazi ni mzazi ili mtoto wako akae kwa mama yako na pia kwa sababu shughuli za mama yako ni nyingi mtafutie msichana wa kazi hapo ili kumpunguzia mama yako mzigo na uwe na uhakika mwanao anamtu wa kumuangalia mama akiwa kwenye mishe zake. Pia uwe unamsaidia mama yako juu ya malezi kwa pesa na pia uwe unawatembelea mara kwa mara.

Kuna baadhi ya wanawake hata sijui wanaroho gani yarabi..........Mungu atusaidie sana.
 
Hapana sio wote kaka.... Kama vipi mpeleke boarding school,hatapata malezi yale uyatakayo but atakuwa katika maangaliz mazuri na atapata ku interruct na watoto wengine....#Mtazamo
 
1. je nimpeleke mtoto boarding school mpaka mdogo wake akuwe ili niwe natoka / au nakaa nao pamoja kwan nataman kuwajenga wanangu kimaadili mapema.

2.nimpeleke tu akaishi kwa bibi yake rejea hapo juu kuhusu mama yangu na ufinyu wa nafasi ya kulea mtoto mdogo kwan sisi wote watoto wake tushaanza kujitegemea.

Kuyafanya haya yote bado hayabadilishi uhalisia ya kwamba huyo ni mwanao...

Wewe ni mwanaume na ni kichwa cha familia, kaa chini umuonye huyo mkeo ya kwamba aamue moja;

Kuishi kwa amani na 'mtoto wenu' au yeye aondoke
 
Pole sana kwa matatizo yako......huyo mwanamke mwanzangu ni kigeu geu kabisa na trust me ukilazimisha mwanao akae hapo basi ujue atateseka sana. Maadam kashakwambia "moyo wake umekataa kumkubali mwanao" basi ni lazima ufanye maamuzi magumu kwa ustawi wa mtoto wako. Ungekua hujamwambia habari ya mtoto wako kabla hujamuoa labda ningeweza kuelewa kwa nini anafanya hivyo japo isingekua kigezo cha kumchukia mtoto asiye na hatia.

Na kinachonishangaza zaidi na yeye ni mwanamke na amezaa......hivi kesho au keshokutwa na yeye akiwa hayupo na akisikia mtoto wake anafanyiwa hivyo anavyomfanya yeye mtoto wa mwenzie atajisikiaje.

Mi ninachoweza kukushauri kwa sasa kaongee na mama yako maana mzazi ni mzazi ili mtoto wako akae kwa mama yako na pia kwa sababu shughuli za mama yako ni nyingi mtafutie msichana wa kazi hapo ili kumpunguzia mama yako mzigo na uwe na uhakika mwanao anamtu wa kumuangalia mama akiwa kwenye mishe zake. Pia uwe unamsaidia mama yako juu ya malezi kwa pesa na pia uwe unawatembelea mara kwa mara.

Kuna baadhi ya wanawake hata sijui wanaroho gani yarabi..........Mungu atusaidie sana.

Na ukishampeleka mtoto kwa bibi yake mwambie mkeo kuwa na mwanaye akikuwa ataenda kwa bibi yake ili mbaki peke yenu maana yeye hapendi watoto.
 
Makubwa!
Usilee ujinga mtoto wake na wako wote wana haki sawa kwako ni watoto wako iweje huyu akae huku yule kule. Kama ni bora basi wake apelekwe kwa bibi huyo abaki hapo.

Kama baba ni kichwa cha familia, usikubali kutenda uovu huo kwa mtoto mdogo asiye na hatia, mwambie achague moja kukaa ama kuondoka kama hataki kumkubali.
 
kuwa na msimamo mwanamke hatakuyumbisha na nyumba ya ghorofa haijengwi na msingi legelege what i mean anza kujenga msingi imara kwa ajiri ya mwanao aweze kuishi kwa amani hapo hapo nyumbani ukiyumba yumba hata wadogo zake watakuja kumbagua badae
 
Kama nimekuelewa vizuri umesema ulivyompeleka mtoto kwa mama ulikuta mazingira sio mazuri ukaamua umlete nyumbani ndio ukamweleza mkeo!
Ulivyokuta hali hiyo kwa mama je ulimpigia mkeo mdiscuss hiyo hali ili ajue mtoto anakuja? Au ulimstukiza na mtoto kashafika?
Kama ni hivi basi hapo ndio tatizo lilipoanzia. Je mkeo ana kazi? Kaa nae chini mzungumze kwa kirefu jaribu kuwa unawanunulia wote wa3 zawadi jaribu kumsaidia kazi zake. Kuwa karibu sana na mkeo na ajue unamjali then atapenda hata damu yako. Lakini aone unakaa kochi moja na mwanao wkt yeye hukai naye then hapo unaleta uhasama.

Ni ngumu sana kuwaelewa wanawake huyo wako hana roho mbaya ni umpende na umwonyeshe kwa vitendo ili asione huyo mtoto ni competitor!
 
Kaka angu si bora tu ungemuacha huyo mtoto kwa mama ake! Hata kama wangeishi kwa shida but upendo wa mama ake ungemsahaulisha hizo shida. Ukikubali matakwa ya huyo mkeo basi jua huko mbeleni ndo hutoamua chochote kuhusu mwanao. Mwambie mtoto wako hapo ndo kwao, kama hataki anaweza akaondoka tu. Kuwa na msimamo

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kuyafanya haya yote bado hayabadilishi uhalisia ya kwamba huyo ni mwanao...

Wewe ni mwanaume na ni kichwa cha familia, kaa chini umuonye huyo mkeo ya kwamba aamue moja;

Kuishi kwa amani na 'mtoto wenu' au yeye aondoke

Ndo jibu stahiki! Aidha akubali kukaa na kumlea vema, au aondoke! Unless otherwise mwanamke ndo kichwa cha familia!
 
Hapo ni kua mkalii kwa nini upelekeshwe na hiyo ni roho mbayaa tu ya huyo mkeo hataki aishi hapo,kua mkalii na umuonye pia mtoto mpeleke boarding utakuta hua anashinda njaa huyo mwanao, sasa hapo wivu wa ninii mtoto mkubwa,ningekua mimi ni mwanaume ningemtishaa kumuacha aone wanaume walivyo wachache tena we una mtoto mmoja wengine wana watoto wa 4 na wote uishi nao,
 
Kuyafanya haya yote bado hayabadilishi uhalisia ya kwamba huyo ni mwanao...

Wewe ni mwanaume na ni kichwa cha familia, kaa chini umuonye huyo mkeo ya kwamba aamue moja;

Kuishi kwa amani na 'mtoto wenu' au yeye aondoke

Yah na huo ndio uanaume....ingekuwa alimficha sawa sasa alimwambia na mwanamke akawa radhi.....sasa anataka mwenzie mtoto akamtupe?
 
Kuyafanya haya yote bado hayabadilishi uhalisia ya kwamba huyo ni mwanao...

Wewe ni mwanaume na ni kichwa cha familia, kaa chini umuonye huyo mkeo ya kwamba aamue moja;

Kuishi kwa amani na 'mtoto wenu' au yeye aondoke

Hata akimuonya haitasaidia wanawake wanakuwaga na roho mbaya ingawa wamezaa hata akimuonya atakuwa ana pretend tu ukiondoka mateso kama kawa huyo mtoto ampelekee kwa mamaake mzazi basi au boarding
 
ukipenda boga penda na UA lake. huyo so make kaka yangu. hata. mm nimeolewa na mwanamume mwenye mtoto na sasa nimezaa watoto wawili nae. hawa wstoto hawajui kama yule kaka yao c mwanangu wa kumzaa, kwa jinsi ninavyowalea . unavyomlea mmto kwa chuki ndinvyo unavyomuharibia maisha yake ya baadae. kwakua anaathirika kisakologia.
Huyo mkeo kama hawezi kukaa na mtoto wsko kama wake muache tena so mama mzuri hata kwa huyo mtoto ulie zaa nae.
 
Ni kweli wewe kama mwanaume ni kichwa cha nyumba na unauwezo wa kumuamrisha mkeo unavyotaka......lakini jamani tukumbuke kua huyo ni mtoto na maisha hayapaswi kua kwenye majaribio. Maamuzi yoyote atakayochukua baba yanamuathiri mtoto mojamoja iwe kwa ubaya au uzuri.......na kwa swala hili hupaswi kutumia nguvu nyingi kuliamua ni lazima busara za hali ya juu zitumikee kuamua mustakabali wa mtoto. Na mara zote wamama ndio wanakua na muda mwingi wa kua nyumbani kuliko wababa......so.....atakapo mlazimisha akubali kua huyo mtoto haondoki hapo.....unajuaje atakacho mtendea mtoto baba yake akiwa hayupo. Usije kumsababishia mtoto ulemavu wa maisha yake yote kutokana na maamuzi yako.

Kwa sasa mpeleke kwa bibi yake mpaka hali itakapokua shwari.........ogopa sana mwanamke mwenye wivu kijinga namna hiyo na maamuzi yake yakuwaga ya hivyo hivyo.
 
Hata akimuonya haitasaidia wanawake wanakuwaga na roho mbaya ingawa wamezaa hata akimuonya atakuwa ana pretend tu ukiondoka mateso kama kawa huyo mtoto ampelekee kwa mamaake mzazi basi au boarding


Mitazamo yetu inaendana my dia....ila mi naona kumpeleka mtoto boarding kama bado ni mdogo sana na hajajitambua. Akikua fine aende boarding. Mi wasiwasi wangu mtoto ataishi kwa mateso nyumbani baba yake akiwa hayupo na hiyo itamuharibia confidence kabisa maishani mwake. Wee mtu ata akikaa na mwanae kochi moja ni ishu leo eti umlazimshe, anaweza akakubali machoni na si moyoni na hiyo ni mbaya sana.

Nakuombea Mungu ufanye maamuzi sahihi kwa ustawi wa mtoto wako na wetu.
 
Back
Top Bottom