Pesa zipo tatizo watu wengi wavivu au wanaridhika mapema mno, mtu akipata kazi inamlipa kimilioni moja anaridhika kabisa anaendelea kukomaa nacho miaka inapita badala ya kufikiria atajiendeleza vipi akue zaidi ya hapo.
Ukitaka kuishi lifestyle kama hilo fungua biashara yako mwenyewe, si kitu rahisi ndiyo ila usitegemee kufanikiwa hata siku moja kwa kumfanyia kazi mtu mwingine, kua na biashara yako mwenyewe au share kwenye kampuni kubwa kitu ambacho ni kilekile meaning una ownership asilimia flani ya profit.
Nilirudi bongo juzijuzi nimekutana na watu kelele kibao nikawaambia kwa nini usinunue vitu huku cheap peleka kule uza three four times hela uliyonunulia, mtaji wa laki ukageuka 5mil ndani ya miezi miwili, leo hii mtu anaishi hana mawazo tena ya wapi pa kulala wala mawazo ya msosi anakula anachotaka.
Siri ni kuacha uvivu, kujituma kupiga kazi basi. Matajiri wote wamepitia hilo, ondoa wale waliorithi mali za wazazi.