Hivi walimu tumemkosea nini Mungu?

Hivi walimu tumemkosea nini Mungu?

Mungu angewezesha kufikia kofia na rungu la Nyumba nyeupe kuna watumishi wanahitaji empowerment ya hali ya juu .
Mwalimu ni kiongozi wa kwanza popote pale lakini Tz mwalimu ni sawa nothing effect kwenye jamii naumia sana kwa kazi wazofanya Walimu wetu.
 
Siwezi kumshauri au kukubali ndungu yangu awe Mwalimu. Walimu wanapitia wakati mgumu kuliko watumishi wote serikalini ,kuanzia muda wao, mazingira yao ya kufundishia hadi kuishi asilimia kubwa ni duni, Msongo wa mawazo kuanzia kwa wanafunzi wazazi na hadi hao waajiri wake na bado maslahi hakuna, Ndo maana Jinsia ya kike wanajiingiza kwenye mambo ya ajabu ajabu nje na kazi yao(mikopo yenye riba kubwa sana na mahusiano yanayo wapelekea kuwa single mothers wengi wao). Jinsia ya kiume ( Mikopo, ngono na ulevi hapo ndo wanaenda kupunguzia stress zao.
 
Unasema kazi uliyonayo ya ualimu ni mbaya? Je nzuri unayo?Ipoteze hiyo uliyonayo ndipo utaona cha mtema kuni.tafuta muda wa ziada ufanye ujasiriamali.
 
sawa mkuu mi nimeishia darasa la 3 usinihukum .
Sijakuhukumu mkuu na kamwe siwezi kufanya hivo ila aina ya ushauri mnaoutoa ndo una ukakasi kumwambia mtu ashasema hali duni ndo imemfanya aingie huko na unamwambia awe mjasiriamali....ujasiriamali in zaid ya kutamka tu hilo neno kuna mengi sana
 
Mpaka siku mtakapoacha kuipigia CCM kura ndipo akili zitakapo warudi
 
Sijakuhukumu mkuu na kamwe siwezi kufanya hivo ila aina ya ushauri mnaoutoa ndo una ukakasi kumwambia mtu ashasema hali duni ndo imemfanya aingie huko na unamwambia awe mjasiriamali....ujasiriamali in zaid ya kutamka tu hilo neno kuna mengi sana
kweli mkuu
 
usipojiheshimu katika kada hiyo na ukiwa muoga, kila siku utakuwa unawalamba miguu hao wanaitwa mabosi....

Uzuri mimi huwa sipendi kupelekeshwa, yaani hii mikwara yao kuna siku nitatafuna kor'dani za mtu.
 
Mamy K,ukitaka kuifurahia kazi hii jiamini,tekeleza majukumu yako kwa wakati pia
Ukija huku kanda ya ziwa kuna sehemu panaitwa Bulima,huwezi fanya kazi kama ukiwa na roho nyepesi,majungu kutoka kwenye kamati ya shule,staff,mwenyekiti wa kijiji,vitongoji,Veo,Diwani na mwenyekiti wa chama cha...!

Kila sehemu hali ni hiyo hiyo, halafu huko kanda ya ziwa kila mtu anajikuta rais kisa ndugu yao rais
 
Fanya yako wenzio sasa hivi wala hatuna muda tunafanya yetu tuu!

Ualimu ukiufikiria utapata stress Fanya yako

Wee Gen huku kijijini najiongezaje, labda nijiuze kwa wakulima. Halafu uhamisho analeta Zengwe.
Kwanza njoo pm unipe mikakati uliondokaje Mtwara.
 
Watumishi wa umma wa Tanzania ni kikundi cha watu wasiojua thamani wala umuhimu wao. mtu akilipwa kamshahara kake ka laki 2 akanunua ka tv flat na kasimu ka techno huhisi kamaliza.
wamejawa na majungu, uongo, uzandiki, kujipendekeza kwa wakubwa zao hata kwa gharama za wenzao, chuki na fitna
Sad truth!
 
UKIAMUA KUACHA NA KUSOMEA FANI NYINGINE KITAHARIBIKA KITU KWANI

Not that easy as you think Josee...napenda nifanye biashra, ila umeiona hii vita ya TRA na wafanyabiashara? Halafu hakuna anayenisupport, ndugu nikiwaambia naacha wananambia nisiache. Yani ni stress.
 
Andika barua yako ya malalamiko uipeleke kwa mwalimu wa kemia pale getini magogoni.

Nasikia na mkewe pia alikuwa mwalimu kabla ya kuingia jumba jeupe.

Huenda wakakusikia, maama wanajua machungu ya waalimu.
Huyo Mkemia yeye tu hamtaki Mkewe, unategemea ataeapenda Walimu wengine?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom