Hivi vyakula vya asili vimepotelea wapi?

mambo_safi

Senior Member
Jul 22, 2019
147
391
Nimezaliwa na kulelewa Bukoba mpaka nilipoanza kidato cha kwanza ndo kama nilihama mkoa wangu mpaka sasa umri unasoma kula chumvi nyingi.
Tangu miaka hiyo sijawahi kukutana na vyakula hivi vya asili kwa majina ya kihaya vinaitwa:
"Amakongo"
"Ebira"
"Ebira ebilikweera"
"Amasoma"
"Enumbu"

AMAKONGO ni jamii kama mihogo vile lakini yenyewe ni mviringo na mmea wake unatambaa chini au juu kama utapata mahali pa kujishikiza. Ukiyapika yanakuwa magumu kiasi kwamba ukiwa unayatafuna yanalia kama muhogo mbichi.

EBIRA: vyenyewe ni vikubwa kama papai jamii ya mihogo na mmea wake unatambaa chini au juu kama utapata mahali pa kujishikiza. Ukiyapika yanakuwa malaini na yanakuwa na rangi rangi fulani hivi.

EBIRA Ebilikwela ni jamii moja ya Ebira isipokuwa hivi ni vyeupee na vinanukia nukia vizuri saana ukivipika mtaa wa pili lazima wanuse

AMASOMA tofauti na jamii hizo tatu juu ambazo ukulia ardhini jamii hii utokeza kwenye mmea juu ya ardhi na mmea huu utambaa ardhini au juu ya ardhi ukipata pa kujishikiza

ENUMBU ni jamii kama tangawizi mwonekano na kuzaliana kwake lakini zenyewe nyeupe na zikipikwa msosi mmoja matata.

Ebu wajuzi na wenyeji wa Bukoba tuelimishe tafadhari!
 
Mbona vipo kibao tu Bukoba hadi Dar unavipata Sinza Mori kwa Kazaura. Sema siku hizi vimekuwa si vingi km kipindi cha nyuma.

Mimi leo nimetoa e'bitakuri anga e'mfuma.
IMG_20200215_151117_526.jpg
 
Mbona vipo kibao tu Bukoba hadi Dar unavipata Sinza Mori kwa Kazaura. Sema siku hizi vimekuwa si vingi km kipindi cha nyuma.

Mimi leo nimetoa e'bitakuri anga e'mfuma.
Hivi si ni viazi vitamu kila mahali vipo na tunavijua! Tunataka hiyo chakula mdau kaongelea anayejua utunagabalishe!
 
Kuna mkoa nilienda mwaka jana,ni Tabutupu !!!kila siku asubuhi wanaenda shamba wanaleta vitu fulani vigumuuuuu vinachemshwa na magimbi....japo sikukaa hata wiki lakini nililose some weight ndani ya huo muda mchache tu

Tatizo vyakula vingi vya asili sio vitamu,viendelee kupotea hivyo hivyo asee
 
Kuna mkoa nilienda mwaka jana,ni Tabutupu !!!kila siku asubuhi wanaenda shamba wanaleta vitu fulani vigumuuuuu vinachemshwa na magimbi....japo sikukaa hata wiki lakini nililose some weight ndani ya huo muda mchache tu

Tatizo vyakula vingi vya asili sio vitamu,viendelee kupotea hivyo hivyo asee
Mkoa gani huo? Ni kawaida wengi tukienda nyumbani asili tulikotokea lazima to loose weight (tukonde) kutokana na kukosa dishes za kitown town hivi! Hahahah! Pole sana!
 
Umenikumbusha mbali. Ebira ebikweela kwetu tunaviita "kashuli", kashuli na mchuzi wa samaki akiyekaushwa kwa moshi wa kuni na nyasi ni mlo niliupenda sana.

Niliwahi kupata kula kashuli hoteli ya kanisa KKKT pale Bukoba mjini. Vyakula ulivyotaja bado vipo ukiondoa enumbu . Enumbu zililimwa kwenye maeneo yaliyokuwa wazi. Sasa ardhi wazi imepungua sana hivyo kilimo hivyo kupunguza sana.
Nimezaliwa na kulelewa Bukoba mpaka nilipoanza kidato cha kwanza ndo kama nilihama mkoa wangu mpaka sasa umri unasoma kula chumvi nyingi.
Tangu miaka hiyo sijawahi kukutana na vyakula hivi vya asili kwa majina ya kihaya vinaitwa:
"Amakongo"
"Ebira"
"Ebira ebilikweera"
"Amasoma"
"Enumbu"

AMAKONGO ni jamii kama mihogo vile lakini yenyewe ni mviringo na mmea wake unatambaa chini au juu kama utapata mahali pa kujishikiza. Ukiyapika yanakuwa magumu kiasi kwamba ukiwa unayatafuna yanalia kama muhogo mbichi.

EBIRA: vyenyewe ni vikubwa kama papai jamii ya mihogo na mmea wake unatambaa chini au juu kama utapata mahali pa kujishikiza. Ukiyapika yanakuwa malaini na yanakuwa na rangi rangi fulani hivi.

EBIRA Ebilikwela ni jamii moja ya Ebira isipokuwa hivi ni vyeupee na vinanukia nukia vizuri saana ukivipika mtaa wa pili lazima wanuse

AMASOMA tofauti na jamii hizo tatu juu ambazo ukulia ardhini jamii hii utokeza kwenye mmea juu ya ardhi na mmea huu utambaa ardhini au juu ya ardhi ukipata pa kujishikiza

ENUMBU ni jamii kama tangawizi mwonekano na kuzaliana kwake lakini zenyewe nyeupe na zikipikwa msosi mmoja matata.

Ebu wajuzi na wenyeji wa Bukoba tuelimishe tafadhari!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mkoa nilienda mwaka jana,ni Tabutupu !!!kila siku asubuhi wanaenda shamba wanaleta vitu fulani vigumuuuuu vinachemshwa na magimbi....japo sikukaa hata wiki lakini nililose some weight ndani ya huo muda mchache tu

Tatizo vyakula vingi vya asili sio vitamu,viendelee kupotea hivyo hivyo asee
Shida siku hizi tunapenda vyakula vitamu vyenye sukari nyingi ndio maana magonjwa ya sukari na figo yameshamili. Mungu alikua na maana kuumba vyakula visivyo na sukari nyingi. Na mara nyingi vyakula visivyo na sukari ni dawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida siku hizi tunapenda vyakula vitamu vyenye sukari nyingi ndio maana magonjwa ya sukari na figo yameshamili. Mungu alikua na maana kuumba vyakula visivyo na sukari nyingi. Na mara nyingi vyakula visivyo na sukari ni dawa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu,vyakula vitamu sikumaanisha utamu wa sukari...mimi sio mtumiaji wa sukari na hata kwenye chai sometimes naweza kunywa bila kuweka sukari kabisa

Hivyo vyakula nilivyomaanisha hapo ni the way walivyokuwa wanaviandaa ni kwa namna ambayo sikuwa nimeizoea,ni chumvi na maji tu basi
 
Back
Top Bottom