Hivi umeshawahi kujipa likizo na kwenda vacation? Ukirudi productivity inaongezeka au iko vilevile?

Hivi umeshawahi kujipa likizo na kwenda vacation? Ukirudi productivity inaongezeka au iko vilevile?

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
31,139
Reaction score
88,800
Wakuu, poleni na mapambano. Leo nina swali au mjadala general.

Mara nyingi tunakimbizana na mishe za kila siku bila hata kuupa mwili na akili nafasi ya kupumzika, ukiachilia mbali vacation.
IMG_1807.jpeg

Vacation inaweza kuwa fupi tu, hata wikiendi moja nje ya mji, lakini matokeo yake yakawa makubwa sana.

Kuna tafiti nyingi zinaonyesha mapumziko husaidia kupunguza msongo wa mawazo na kurejesha nguvu mpya ukirudi mzigoni. Swali langu, je, wewe ukirudi kazini au kwenye shughuli zako baada ya vacation unahisi tofauti?
IMG_1806.jpeg

Kuna watu wanasema productivity huongezeka mara mbili kwa sababu akili inakuwa fresh, mwili umepumzika, na ubunifu unarudi kwa nguvu.

Wengine wanahisi ni kama hakuna mabadiliko makubwa, wanaendelea tu kama kawaida.
IMG_1805.jpeg

Huenda hii inategemea mtu, nature ya kazi yake na aina ya likizo aliyojipa (labda ni ya kupumzika kabisa au ni safari lakini yenye shughuli nyingine tena)!

Lakini pia kuna changamoto; mara nyingine ukirudi kutoka likizo, kazi ulizokimbia unazikuta so unaweza uone kama mapumziko hayakusaidii sana.

Ila kwa upande wangu na nature ya ajira yangu, nikitoka likizo mwili na akili vinakuaga vimepumzika sana. Especially nikitoka vacation ata ya week moja tu aisee uwa nakua fresh sana.

Je, kwa uzoefu wako binafsi, vacation imekuwa na faida gani kwako kwenye kuongeza au kubadilisha kiwango cha uzalishaji? Na mara ya mwisho lini ulienda vacation?
 
Je, kwa uzoefu wako binafsi, vacation imekuwa na faida gani kwako kwenye kuongeza au kubadilisha kiwango cha uzalishaji?
Binafsi ina faida kwa sababu napumzika na nakua reenergized again nikirudi kazini productivity inakua juu!

Atleast safari 3 kwa mwaka na once lazima nisafiri alone bila familia.
Na mara ya mwisho lini ulienda vacation?
3 months ago

Na next week naenda tena na KERATO MOMBAA
 
Nimenza ka utaratibu kila mwaka,nimeenda Ngorongoro,udzungwa water fall,Magoroto forest.mwaka huu najipanga niende sijui wapi.

** Udzungwa water fall pazuri sana,lakini usiwe mvivu kutembea maana unatembea kama KM 3 hivi halafu ni milima na miteremko.
 
My annual baecation timetable
1. February-Kilimanjaro marathon naitumia kama weekend break
2.March/April-Easter weekend hii Lushoto au Moro
3.Dodoma marathon-another weekend break
4 Selous marathon hii naenda weekend hii.
5.Xmas,New year break...hii ni must

Nikirudi kichwa kinakuwa chepesi sana na ari ya kuwajibika inaongezeka.
 
Uzuri hata ukikimbia kwenda mbali kuupumzisha ubongo na kujipa Comfort, ukirudi moto ni ule ule uliouacha utaukuta unakusubiri, hapa kila kitu ni saikolojia kujua inafanyaje kazi.
 
Back
Top Bottom