Hivi TCRA, BRELA, Uhamiaji na NIDA wako nchi moja?

kandawe

JF-Expert Member
Jun 24, 2013
1,137
809
Kwa sasa nchini kwetu hupati huduma Hati ya kusafiria, kusajiri kampuni au kusajili laini ya simu bila kitambulisho cha uraia.

Binafsi leo ni karibia mwaka mzima toka niandikishwe kupata kitambulisho cha uraia lakini bado sijakipata pamoja na kupiga safari zaidi ya mara saba kwenye ofisi za NIDA na jibu nililolipata kwa siku zote hizo ni SUBIRIA HAKIJAWA TAYARI.

Ilitolewa code ya kuulizia namba ya hicho kitambulisho kwa simu *152*00# kwa maana ya kwamba ukiwa na namba tu inatosha kupata huduma. Hiyo nayo wameshakula shs 10 zangu mara zaidi hata ya ishirini hamna kitu.

Niko mjini Mwanza na ofisi za NIDA ziko Mkolani, ukienda ile ofisi hadi imekuwa kero, watu wamejaa toka asubuhi mpaka wanafunga.

Kuna wakati najiuliza,hivi hivi vitambulisho waliotakiwa kuvipata bila usumbufu ni wafanyakazi wa serikalini tu? Maana wao waliandikishwa maofisini kwao na wakapewa tu haraka.

Kuna ambao hawakujiandikisha na wamekuwa wakienda ofisini NIDA penyewe,wanavipata tu ndani ya wiki lakini ukiwauliza wanakuambia hii Tanzania ukifuata utaratibu utahangaika mno,inasemekana wanatoa shs 100,000 na wanapata faster! Sasa sie ambao hatuna hiyo 100,000 maana yake ni nini?

Laini zetu za simu wa watazifunga maana muda uliotolewa ni mwezi wa 12 na kwa dalili zinazoonekana NIDA hata hawana plan B ya kuharakisha hilo zoezi maana yaonekana nako ni kamradi watu wanajipigia hela na kuongeza kipato.
pia hatuwezi kufungua kampuni maana BRELA nao wanahitaji kitambulisho cha uraia. Na pia hatuwezi kupata hati ya kusafiria kwa sababu masharti ni kuwa na kitambulisho ya uraia.

Nafikiria sana na kuwaza, hivi hizi taasisis ziko chini ya serikali tofauti? Kulikuwa na uharaka gani wa kuweka hayo masharti wakati ukweli wanaujua kuwa watanzania asilimia kubwa hawajapata hivyo vitambulisho vya uraia?
Hivi, wakuu wa wilaya na mikoa hawaoni mlundikano wa watu kwenye ofisi za NIDA na kutoa ukweli wa hivyo vitambulisho?

Kwanini NIDA wasingeachwa wamalize zoezi japo kwa asilimia 80% ya watanzania wawe na vitambulisho ndiyo masharti yawekwe?
 
Wakati flani nenda Nida jiweke kwenye status, Nchi hii bila kiki haiendi. Mimi wakati nasajiri Brela niliteseka sana, kuna siku sitasahau nilienda Nida huku nimevaa tai yenye bendera ya taifa pamoja na ID ya kuzugia tu, jamaa walivyoniona kwanza wakasema karibu Mh. Ndani ya sekunde wakanitolea number. Ila ukweli huwa wana demand pesa
 
Ukosefu wa weledi kwa viongozi wetu ni tatizo kubwa sana.

Pia kuweka taratibu ngumu/usumbufu katika kupata kitambulisho cha uraia ni njia mojawapo inayotengeneza mazingira ya rushwa.

Hivyo basi, hizo ni mbinu za kutengeneza mazingira ya rushwa.
 
Wakati flani nenda Nida jiweke kwenye status, Nchi hii bila kiki haiendi. Mimi wakati nasajiri Brela niliteseka sana, kuna siku sitasahau nilienda Nida huku nimevaa tai yenye bendera ya taifa pamoja na ID ya kuzugia tu, jamaa walivyoniona kwanza wakasema karibu Mh. Ndani ya sekunde wakanitolea number. Ila ukweli huwa wana demand pesa

Dah, hapo lazima uwe komando.

Mimi niko town toka utoto lakini hadi nimechoka, najaribu kuwafikiria walioko vijijini, hivi vitambulisho hata kuviona walishawahi kuviona kweli?

Halafu wanaambiwa simu zao desemba 31 mwaka huu zinazimwa.

Kweli tutafika tu na unyonge wetu. Ila kwa haya mazingira, wafanyakazi wanatengenezewa tu mianya ya rushwa.

Natamani, namba moja angefutilia mbali kwanza huu utaratibu mbovu,adeal na NIDa mpaka hapo watanzania watakapokuwa wamepata hivyo vitambulisho.

Na kinachoudhi,walioko serikalini kwa vile wao vitambulisho viliwafuata kwenye meza zao,wanatuona sisi tunaosota kuvitafuta kama wazembe tunaosubilia dakika za mwisho mwisho.
 
Nchi yetu ni ya kishamba sana, nimeshangaa anayetaka kupata kitambulisho cha NIDA eti aambatanishe kopi ya pass ya kusafiria ,wakati huo huo anayetaka pass ya kusafiria lazima awe na kitambulisho cha Taifa(NIDA)

Ukiangalia mfumo wa upatikanaji wa Passport tunascaniwa vidole, na mfumo wa kupata kitambulisho cha Taifa tunascaniwa tena, hata ukipata kutaka Leseni unascaniwa, najiuliza mlolongo wa nini huu?

Britanicca
 
Tatizo kubwa la viongozi wetu ni kupenda kiki za kisiasa! Viongozi wanafahamu fika kuwa uwezo wa kifedha wa serikali ni mdogo sana, lakini kila kukicha wanaanzisha miradi mikubwa ambayo inahitaji fedha nyingi. Matokeo yake utekelezaji unakuwa wa kusuasua!
Ukweli ni kuwa serikali haina fedha za kuwezesha NIDA wakamilishe zoezi la kutengeneza vitambulisho kwa wakati! Matokeo yake ni kukaribisha rushwa na usumbufu kwa wananchi!
 
Ukienda uhamiaji kwenda kuomba kupata Passport, masharti na maswali utakayokutana nayo huko unaweza ukaghairi kuomba hiyo passport.
 
Ndugu yangu yaani wewe tulia tu..
Nchi imekabidhiwa mikononi mwa washamba!
Yaani wao wanatamani walitakalo au walitamkalo litokee siku hiyo hiyo...
Hamnaga kabisa cross-sectoral or departmental coorperation/collaboration..
Nchi ni moja chini ya serikali ile ile; idara zile zile lakini kila idara iko busy kufanya mambo yake bila kushirikiana na nyingine ili kuokoa muda, kupunguza gharama na usumbufu kwa wananchi..
Alafu hapo utamsikia hawafu akikoroma na lisauti lake kama ngoma iliyolegea.. "Mimi ni mtetezi wa wanyonge" Hivi huyu hawafu anajua wanyonge wake hao wanapitia madhila gani toka siku inaaza hadi inaisha??
Nenda RITA - vizazi na vifo; mafoleni na ubabaishaji!
Nenda BRELA - ubabaishaji tu
Nenda TCRA - mizengwe
Nenda UHAMIAJI - usanii na urushaji
Nenda NIDA - unyanyasaji na urushaji (wanawaibia watu Tsh 100 kila meseji kwenda *152*00#)
Nenda TRA - uhuni uhuni na wizi
Nenda POLISI - rushwa

Hivi ni nani alitulazimisha kutumia mifumo ya Online au Biometric..?? Hii mifumo bado sana na inawapotezea watu wengi muda na gharama ambazo zinazorotesha uchumi wao na wa taifa kwa ujumla..
Unaenda NIDA au UHAMIAJI unaelekezwa kuwa tumehamia Online - Huko Online kila siku system iko down!
Ni kwa nini tusingefanya majaribio ya awali ili kujiridhisha kwanza kuwa hizi Online systems ndo tiba ya matatizo yetu ya analog au manual entries?
Why tusingejipa muda wa kutosha (why rush into something untested; very uncertain?).
Kulikuwa na ugumu gani kwa NIDA kupewa muda wa kutosha kuwahudumia watanzania kwa kiwango cha kila mtu kupata ID namba yake ndipo yatoke maelekezo ya kusajili laini za simu kwa mfumo wa Biometrics?

Nauliza! Kulikwa na ugumu gani kuwaruhusu uhamiaji kuwaelekeza wamiliki wa pasipoti za zamamni kuendelea kuzitumia hadi pale zitakapo expire ndo waki-renew wapewe hizo za electronics?

Alafu kuna tatizo gani kama TCRA, BRELA, TRA, UHAMIAJI na NIDA wakishirikiana ili kushare details ambazo tayari wanazo?

Enyi watoa matamko... Kumbukeni kuwa matamko yenu yasipopitia kwenye mfumo wa ubongo na yakachujwa na kuhaririwa vyema yanakuwa ni matatizo makubwa kwenye utekelezaji wake!!
 
Kwa sasa nchini kwetu hupati huduma Hati ya kusafiria, kusajiri kampuni au kusajiri laini ya simu bila kitambulisho cha uraia.
Binafsi leo ni karibia mwaka mzima toka niandikishwe kupata kitambulisho cha uraia lakini bado sijakipata pamoja na kupiga safari zaidi ya mara saba kwenye ofisi za NIDA na jibu nililolipata kwa siku zote hizo ni SUBIRIA HAKIJAWA TAYARI.
ilitolewa code ya kuulizia namba ya hicho kitambulisho kwa simu *152*00# kwa maana ya kwamba ukiwa na namba tu inatosha kupata huduma. Hiyo nayo wameshakula shs 10 zangu mara zaidi hata ya ishirini hamna kitu.
Niko mjini Mwanza na ofisi za NIDA ziko Mkolani, ukienda ile ofisi hadi imekuwa kero, watu wamejaa toka asubuhi mpaka wanafunga.
Kuna wakati najiuliza,hivi hivi vitambulisho waliotakiwa kuvipata bila usumbufu ni wafanyakazi wa serikalini tu? Maana wao waliandikishwa maofisini kwao na wakapewa tu haraka.
kuna ambao hawakujiandikisha na wamekuwa wakienda ofisini NIDA penyewe,wanavipata tu ndani ya wiki lakini ukiwauliza wanakuambia hii Tanzania ukifuata utaratibu utahangaika mno,inasemekana wanatoa shs 100,000 na wanapata faster! Sasa sie ambao hatuna hiyo 100,000 maana yake ni nini?
Laini zetu za simu wa watazifunga maana muda uliotolewa ni mwezi wa 12 na kwa dalili zinazoonekana NIDA hata hawana plan B ya kuharakisha hilo zoezi maana yaonekana nako ni kamradi watu wanajipigia hela na kuongeza kipato.
pia hatuwezi kufungua kampuni maana BRELA nao wanahitaji kitambulisho cha uraia. Na pia hatuwezi kupata hati ya kusafiria kwa sababu masharti ni kuwa na kitambulisho ya uraia.
nafikiria sana na kuwaza, hivi hizi taasisis ziko chini ya serikali tofauti? Kulikuwa na uharaka gani wa kuweka hayo masharti wakati ukweli wanaujua kuwa watanzania asilimia kubwa hawajapata hivyo vitambulisho vya uraia?
Hivi, wakuu wa wilaya na mikoa hawaoni mlundikano wa watu kwenye ofisi za NIDA na kutoa ukweli wa hivyo vitambulisho?
Kwa nini NIDA wasingeachwa wamalize zoezi japo kwa asilimia 80% ya watanzania wawe na vitambulisho ndiyo masharti yawekwe?
Huu mfumo wa Tsh 100 ndo umenivuruga kabisaaa
Yani ID nlikua nayo ikapotea leo hii naingiza particulars nilizosajilia ili nipate namba wananiambia hakuna taarifa zinazo exist, sasa cjui ile ID nilijipaga mwenyew

"Ukicheza na nguruwe kwenye matope mtachafuka wote alaf yy atafurahi" sasa tunasubir watufungie si ndo kuongeza uchumi kwenyew kwa awamu hii
 
Inaoneka kila office ina database yake ya fingerprints badala ya kuwa na database moja kwa nchi nzima.
 
Nchi yetu ni ya kishamba sana, nimeshangaa anayetaka kupata kitambulisho cha NIDA eti aambatanishe kopi ya pass ya kusafiria ,wakati huo huo anayetaka pass ya kusafiria lazima awe na kitambulisho cha Taifa(NIDA)

Ukiangalia mfumo wa upatikanaji wa Passport tunascaniwa vidole, na mfumo wa kupata kitambulisho cha Taifa tunascaniwa tena, hata ukipata kutaka Leseni unascaniwa, najiuliza mlolongo wa nini huu?

Britanicca
Nafikiri wanaoleta huo ufarm unawatambua

Ova
 
Wapo nchi moja ndiyo...

Ila kila idara wanajiona wao ndiyo Miungu watu, hawajali ule usumbufu unaoupitia...

Majibu yao ni marahisi sana... Bado rudi tarehe fulani...



Cc: mahondaw
 
Kwa sasa nchini kwetu hupati huduma Hati ya kusafiria, kusajiri kampuni au kusajiri laini ya simu bila kitambulisho cha uraia.
Binafsi leo ni karibia mwaka mzima toka niandikishwe kupata kitambulisho cha uraia lakini bado sijakipata pamoja na kupiga safari zaidi ya mara saba kwenye ofisi za NIDA na jibu nililolipata kwa siku zote hizo ni SUBIRIA HAKIJAWA TAYARI.
ilitolewa code ya kuulizia namba ya hicho kitambulisho kwa simu *152*00# kwa maana ya kwamba ukiwa na namba tu inatosha kupata huduma. Hiyo nayo wameshakula shs 10 zangu mara zaidi hata ya ishirini hamna kitu.
Niko mjini Mwanza na ofisi za NIDA ziko Mkolani, ukienda ile ofisi hadi imekuwa kero, watu wamejaa toka asubuhi mpaka wanafunga.
Kuna wakati najiuliza,hivi hivi vitambulisho waliotakiwa kuvipata bila usumbufu ni wafanyakazi wa serikalini tu? Maana wao waliandikishwa maofisini kwao na wakapewa tu haraka.
kuna ambao hawakujiandikisha na wamekuwa wakienda ofisini NIDA penyewe,wanavipata tu ndani ya wiki lakini ukiwauliza wanakuambia hii Tanzania ukifuata utaratibu utahangaika mno,inasemekana wanatoa shs 100,000 na wanapata faster! Sasa sie ambao hatuna hiyo 100,000 maana yake ni nini?
Laini zetu za simu wa watazifunga maana muda uliotolewa ni mwezi wa 12 na kwa dalili zinazoonekana NIDA hata hawana plan B ya kuharakisha hilo zoezi maana yaonekana nako ni kamradi watu wanajipigia hela na kuongeza kipato.
pia hatuwezi kufungua kampuni maana BRELA nao wanahitaji kitambulisho cha uraia. Na pia hatuwezi kupata hati ya kusafiria kwa sababu masharti ni kuwa na kitambulisho ya uraia.
nafikiria sana na kuwaza, hivi hizi taasisis ziko chini ya serikali tofauti? Kulikuwa na uharaka gani wa kuweka hayo masharti wakati ukweli wanaujua kuwa watanzania asilimia kubwa hawajapata hivyo vitambulisho vya uraia?
Hivi, wakuu wa wilaya na mikoa hawaoni mlundikano wa watu kwenye ofisi za NIDA na kutoa ukweli wa hivyo vitambulisho?
Kwa nini NIDA wasingeachwa wamalize zoezi japo kwa asilimia 80% ya watanzania wawe na vitambulisho ndiyo masharti yawekwe?
Hujasikia mbwembwe za Yona ,si amekwambia amerudisha nidhamu ya watumishi wa umma au Nida sio watumishi wa umma ?
 
b8b7d751-64a7-4f60-aba9-e26ef1a41fd4.jpg
 
Back
Top Bottom