Hivi TBC mnakwama wapi?

komanyahenry

JF-Expert Member
Sep 15, 2017
903
1,352
Naangalia Dr Shein akifunga maonesho ya viwanda ya SADC ikiwa ni mubashara, nikajaribu kufuatilia television zinazorusha mubashara tukio ili muhimu ni ITV, EATV, Channel Ten na TBC, kufika hiyo television ya taifa nimekutana na kitu cha ajabu sana, nashindwa kuelewa kama hakuna wataalamu wanaoweza kuleta mageuzi kwenye hiyo television. Kwanza rangi ni mbovu kushinda hata Dira TV. Pili, licha ya kuwa mlengwa ni Dr Shein lakini sidhani kama ilikuwa ni sahihi kuwakata/ kuoneshwa nusu sura kwa walinzi wa Rais wetu wazanzibar
 
Tuliambiwa watakuja marais wengi na watu wengi kama elfu mbili na kumi na nne kwa ajili ya mkutano wa SADC na tukaambiwa tusiende bila kuoga mjini, vipi mkutano unaendeleaje huko?
 
Huwezi kuona ratiba za vipindi vyao kwenye info kwenye ving'amuzi halafu hawajui hata matumizi ya PG. niliona wanaonyesha katuni halagu wameweka PG 13. Maaba yake ni kuwa wasiangalie watu chini ya miaka 13
 
Huwezi kuona ratiba za vipindi vyao kwenye info kwenye ving'amuzi halafu hawajui hata matumizi ya PG. niliona wanaonyesha katuni halagu wameweka PG 13. Maaba yake ni kuwa wasiangalie watu chini ya miaka 13

kuna cartoon za adults only mkuu..., mfano southpark, na familyguy zile language kwa vijana wadogo hazifai (weka mbali na watoto even PG13)

 
Hayo ndo mambo ya kina Anganile wa TBC, wanajiona wajaaaanja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…