Hivi nini kimeikumba biashara ya mayai ya kware !?

Hivi nini kimeikumba biashara ya mayai ya kware !?

Fiziolojia

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2019
Posts
815
Reaction score
1,085
Hii biashara nakumbuka ilivuma sana miaka ya 2012-2014. Tuliambiwa mayai haya yanafaida lukuki za kiafya lakini Sijui ni nini kimetokea maana yamekuwa adimu kweli kweli.

Mfano, leo nimezunguka kila kona kuyafuta mayai ya kware lakini sikufanikiwa hata kupata connection. Wafanyabiashara wengine ukiwauliza sokoni ndio hata hawayajui.

Nachojiuliza ni kwamba serikali kupitia wizara ya afya/ mamlaka ya chakula au waliyapiga ban ila mimi ndio sina habari, au zile zilikuwa ni promo za mitandaoni tu kipindi kile!?

Kama kuna mtu anayefahamu sababu za kuadimika/ kutoweka kwa biashara hii naomba anijuze tafadhali, na ikiwezekana kuniuzia kabisa kwani nimezunguka sana mjini mpaka nahisi kukata tamaa.

Asanteni.
Screenshot_2019-10-21-22-31-24-301_org.mozilla.firefox.jpeg
 
Watu walishapiga hela na hiyo wave ikapita. Saa hizi kware wanaishi kwa amani.
 
Hata wewe ukitaka kupiga ela
Tafuta idea tu, tangaza wazo mbuni anaponya kansa na ni kinga kwa walio wazima idea ikibamba hakikisha una mayai na vifaranga wa kutosha kuanza kusambaza. Mpk ije isitukiwe ushakuwa bakhresa
 
Hata wewe ukitaka kupiga ela
Tafuta idea tu, tangaza wazo mbuni anaponya kansa na ni kinga kwa walio wazima idea ikibamba hakikisha una mayai na vifaranga wa kutosha kuanza kusambaza. Mpk ije isitukiwe ushakuwa bakhresa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]ila mkuu kumbuka hata kwenye biblia ndege hawa wana wa izraeli walishushiwa kware kutoka mbinguni wakiwa jangwani. Hapo achilia mbali utafiti wa kisayansi kuthibitisha faida lukuki za ndege huyu.
 
Biashara nyingi za Tanzania zinakufa sababu ya fursa na kudanganyana.
Wafugaji wengi wanaingia sababu ya story wakishaingia wanakutana na mambo tofauti
 
Nawe unayasaka kwa lengo la ‘faida za kiafya’ au biashara..?

Biashara ni promo na timing, kwa sasa tunauza sana CHIA SEEDS kwamba zina faida lukuki kiafya.... jifunze kwenda na mdundo.
 
Nawe unayasaka kwa lengo la ‘faida za kiafya’ au biashara..?

Biashara ni promo na timing, kwa sasa tunauza sana CHIA SEEDS kwamba zina faida lukuki kiafya.... jifunze kwenda na mdundo.
Nayatafuta ili niyatumie mimi na nyumba yangu kwa sababu nimezijua faida za kware.
 
Back
Top Bottom