Scolari Ndenga
JF-Expert Member
- Aug 4, 2008
- 271
- 43
WanaJF,
Ukiangalia post lukuki zinasanifu hali halisi ya ukosefu wa ajira inayozidi kumea Tanzania. Ni kweli hata nchi nyingine zinakumbwa na tatizo hili, lakini je hapa kwetu nini haswa tufanye kuwa mwarobaini?
Mchango kwa mapana na wahusika wote; yaani kama serikali, je kijana mwenyewe naye afanyaje?
Ukiangalia post lukuki zinasanifu hali halisi ya ukosefu wa ajira inayozidi kumea Tanzania. Ni kweli hata nchi nyingine zinakumbwa na tatizo hili, lakini je hapa kwetu nini haswa tufanye kuwa mwarobaini?
Mchango kwa mapana na wahusika wote; yaani kama serikali, je kijana mwenyewe naye afanyaje?
Hili ni suala sugu ulimwenguni kote, lakini kwa TZ ni kubwa zaidi kutokana na mfumo wetuwa elimu. Elimu inayotolewa, mfumo wa kusoma-kufundisha unalenga zaidi katika kupasi mitihani kuliko kuwa wabunifu. Pia tunatoka katika mfumo wa kutegemea zaidi ajira za sekta ya umma kuliko sekta binafsi.
Suluhisho ni kujiajiri, lakini hili nalo lina ugumu wake, kukosa mtaji na ujuzi. La kufanya ni kwa vijana wenye ujuzi mbali mbali kujikusanya na kubuni miradi. Umoja ni nguvu.