wiseboy.
JF-Expert Member
- Aug 11, 2014
- 2,932
- 4,534
Wahanga wa misukosuko wa serikali za CCM zilizopita na iliyopo ni wengi,hakuna jipya kwa serikali ya rais Magufuli,anachofanya ni kupita njia hiyo hiyo waliopitia watangulizi wake japokuwa kila mmoja kwa staili yake.
Jenerali Ulimwengu alijikuta akiishi ndani ya taifa alilozaliwa na kukulia kwa kulipia kibali kila mwaka,si hivyo tu,Ulimwengu aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Ngara,lakini aliponzwa na kalamu yake baada ya kuanza kuikosoa serikali,papo hapo ikabainika kuwa huyo hakuwa raia halali wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Kama mtu aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya,yaani msaidizi mkuu wa rais wilayani alikiona cha moto ije kuwa Abdul Nondo tu?
Hakuna anayeweza kukutamkia hadharani kuwa ni lazima uwe CCM,na usijaribu kwa namna yoyote ile kuikosoa CCM na serikali yake.
Mambo yanayoendelea tu yanatosha kukupatia jibu tosha kabisa kuwa,kuikosoa CCM na serikali yake ni kwamba hujipendi.
Kwa hiyo ni lazima uipende CCM tu.
Kakobe amehubiri neno la Mungu miaka nenda rudi akiwa hapa hapa Tanzania,Kakobe ni maarufu sana na alikuwa akihubiri kwenye TV na kuonekana nchi nzima.
Baada ya kumtaka rais Magufuli atubu dhambi zake,tayari uraia wa Kakobe unatia mashaka ,halafu kuna watu wanashangilia mambo ya ajabu na huzuni yanayoendelea nchini.
Kila anayeikosoa serikali ni lazima limkute la kumkuta,jamani endeleeni kushangilia na kufurahia tu,ila mkumbuke kuwa hii meli tumepanda sote,inatobolewa mnacheka kwa kejeli,na wakati ikizama tunazama wote.
Jenerali Ulimwengu alijikuta akiishi ndani ya taifa alilozaliwa na kukulia kwa kulipia kibali kila mwaka,si hivyo tu,Ulimwengu aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Ngara,lakini aliponzwa na kalamu yake baada ya kuanza kuikosoa serikali,papo hapo ikabainika kuwa huyo hakuwa raia halali wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Kama mtu aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya,yaani msaidizi mkuu wa rais wilayani alikiona cha moto ije kuwa Abdul Nondo tu?
Hakuna anayeweza kukutamkia hadharani kuwa ni lazima uwe CCM,na usijaribu kwa namna yoyote ile kuikosoa CCM na serikali yake.
Mambo yanayoendelea tu yanatosha kukupatia jibu tosha kabisa kuwa,kuikosoa CCM na serikali yake ni kwamba hujipendi.
Kwa hiyo ni lazima uipende CCM tu.
Kakobe amehubiri neno la Mungu miaka nenda rudi akiwa hapa hapa Tanzania,Kakobe ni maarufu sana na alikuwa akihubiri kwenye TV na kuonekana nchi nzima.
Baada ya kumtaka rais Magufuli atubu dhambi zake,tayari uraia wa Kakobe unatia mashaka ,halafu kuna watu wanashangilia mambo ya ajabu na huzuni yanayoendelea nchini.
Kila anayeikosoa serikali ni lazima limkute la kumkuta,jamani endeleeni kushangilia na kufurahia tu,ila mkumbuke kuwa hii meli tumepanda sote,inatobolewa mnacheka kwa kejeli,na wakati ikizama tunazama wote.