Hivi ni kwanini bando lina expire? Tungekuwa na wabunge kama huyu 100 nchi yetu ingeendelea kiuchumi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,141


"Hivi ni kwanini bando zina expire? Simu ni ya kwangu, nimenunua bando kwa fedha yangu halafu unanilazimisha nitumie kwa muda unaotaka wewe, hii ni kwanini Mh Spika? Kama ni sheria, basi iletwe sheria hapa ibadilishwe, kwasababu tunaibia wananchi.

"Anatafuta fedha kwa jasho, ananunua simu, anataka awasiliane, ananunua bando anataka limsaidie anaambiwa ndani ya siku 7 linatakiwa liwe limeisha! Hivi hii ni sheria ya nchi gani?

"Kama ni sheri basi tunaomba ije hapa, kwanini unipangie kutumia bando langu? Mimi si ndio najua umuhimu wa mawasiliano na ndio maana nikanunua bando la wiki moja? Kama nimeamua kulitumia taratibu wiki moja imeisha nimeweka akiba kwanini wewe ulikate?

"Mh. Spika nakuomba sana kwa hili uwe mkali utuongoze hili jambo la kuibia wananchi lifikie mwisho."
 
Kuna vitu kila mtu akipata access yake mapinduzi huweza kufanyika, nchi za dunia 3 huwa wananchi wake wananyimwa access ya info ili wasiweze kujua mambo yanaendaje.
 
Uelewa tu! Vifurushi ni kama offer tu! Kama unataka huduma ambayo hainakikomo tumia Salio lako la kawaida hakuna anaekupangia ni pesa yako tu!
 
Tanzania Wananchi wanapigwa kila mahali, Wizi kwenye kila sector.

BEI YA INTERNET IMEPANDISHWA ILI KUKUZA MAPATO, SERIKALI HAWAJALI WANANCHI KABISA.

Huduma ambayo wanachi wanatumia kwa kiasi kikubwa, serikali inatia mkono kuwanyonya wananchi pesa zao.

Serikali haiweki mazingira ya kuwapa ajira vijana ila inawanyonya Kwa kidogo walichonacho wananchi wao.

STUPID!
 
Tanzania Wananchi wanapigwa kila mahali, Wizi kwenye kila sector.

BEI YA INTERNET IMEPANDISHWA ILI KUKUZA MAPATO, SERIKALI HAWAJALI WANANCHI KABISA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
Umenena sahihi.

Serikali inaachia rasilimali almost bure kwa wageni, wanakuja kuwabana wananchi kama chanzo cha mapato kwny kila sekta kama ulivyonena
 
Kuna siku nilikua na watu wa research wa vodacom niliwapa hii kitu kuwa inaumiza ,jibu halikueleweka zaidi ya tutafikisha kwa wahusika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom