Hivi ndivyo wafugaji wengi wa kuku wanavyotapeliwa kwa kuuziwa vifaranga vya uzao wa pili au tatu

theriogenology

JF-Expert Member
Oct 7, 2016
8,750
15,632
Leo ningependa kuzungumzia hii biashara ya kuku inayofanywa na baadhi ya wafugaji ambao mwisho wa siku wanazalisha vifaranga na kuwauzia wajasiliamali wengine.

Somo hili ni mahususi kwa wale wajasiriamali ambao wanakimbilia kununua vifaranga kwa watu hapa na walenga wale wanaofuga Kuroiler ama Sasso.

Kwa ufupi ni kwamba mmachezewa mchezo mchafu na baadhi ya wafugaji kwa kuwauzia vifaranga ambao ni kizazi cha pili ama tatu ambapo kuku hao perforamance yao iko chini mno tofouti na mnavyoaminishwa na hao wafugaji. Mbaya zaidi, wameenda mbali sana kuwauzia kwa gharama ya juu zaidi ambapo kihalali inakuwa si sawa.

Labda nigusie kidogo hapa, hawa kuku wazazi wa either Layers, Broiler ama Kuroiler/Sasso ni gharama sana kuwaingiza hapa nchini na pia uleaji wake unahitaji umakini mkubwa sana tofouti na hawa kuku wetu wa kawaida. Kwa makadrio tu kifaranga kimoja cha parent stock mpaka kuingia nchini kitakugharimu kati ya USD 15~20 hivyo ni ngumu kwa mtu wa kawaida kumudu gharama yake, hivyo kupelekea makampuni makubwa kama Silverlands, Interchicks na Mkuza Chicks kuwa na kuku hao.

Baada ya kulelewa vyema kuku hao wazazi hutaga mayai na kupelekwa hatchery ambapo mayai ya broiler yatoa vifaranga vya kuku wa nyama ambavyo mtauziwa kwa lengo la kutoa nyama tu, mayai ya kuku wa mayai yatatoa kuku wa mayai kwa ajili ya mayai tu na mayai ya kuroiler/sasso vifaranga ambao watatumika kama kuku wa nyama au kwa ajili ya mayai pekee.

Sasa baadhi ya wafugaji hutumia mwanya huu kuwakuza hao kuku chotara na kupata mayai yao ambapo huyapeleka hatchery kutotoleshwa na kupata kizazi cha pili (2nd generation) na wao pia kuwauzia wafugaji wengine. Labda niwaambie tu hapa ndiyo huwa munaibiwa maana performance ya kuku hao itakuwa chini sana kwa maana kwamba kuanzia utagaji, ukuaji utakuwa chini na pia kuku hawa hawatokaukiwa na magonjwa maana kinga yao ya mwili iko chini mno.

Mwisho, kwa wafugaji ambao wangependa kuingia katika industry hii ningependa kuwataadharisha muache mara moja kununua vifaranga kwa wafugaji wa nyumbani maana mnatapeliwa mchana kweupe kwa kununua kuku ambao hawatokupa matokeo mazuri.

Kwa maana hiyo ningependa mnunue kuku hao katika makampuni makubwa ambayo yana kuku wazazi (parent stock) mtapata matokeo mazuri tofouti na hao wa mtaani.

Maelezo yote nimefupisha katika mchoro hapo chini.

Kama kuna sehemu hujaelewa na utahitaji maelezo zaidi weka swali lako hapo nami nitakujibu.

b9b6d0f75338469ab0a593aa7e10b621.jpg
 
Asante kwa somo, kwene hayo makampuni makubwa kuna uhakika gani kua watakuuzia hio parent stock, kwani Wenyewe Hawana hizi second generation? Na utawatambua vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Ahsante kwa swali zuri. Iko hivi hayo makumpuni makubwa wao huwa ndio wenye parent stock na hawawezi kukuuzia na ilitokea wanakuuzia basi huwa ni kwa kukuuzia kama nyama na si vinginevyo wanafanya hivyo kwa sababu ya kwamba ukipata huyo jogoo wa parent stock na ukienda kuwachanganya na kuku wako basi kuku wako watakuwa na uwezo mkubwa wa uzalishaji hivyo wanaliepuka hilo kwa sana maana wataua biashara yao.

Hivyo hao parent stock wakizeeka majogoo yote huchinjwa na hapo hufuatiwa na matetea ya parent stock baada ya siku 7~10 maana kwa siku hizo mayai yote ambayo ni fertilized yanakuwa hayapo tena.

Swali la pili, Makampuni tajwa hapo juu hayana second generarion bali wana 1st generation ambao ndio wanawauzia nyie ili nyie mkapate nyama au mayai pakee na sio kupata mayai na kuyapeleka hatchery kwa ajili ya utotoleshaji hivyo kuishia kupata second generation ambayo kwa performance inakuwa iko chini mno.

Kwa mfano. vifaranga wa 1st generation wa kuroiler na sasso wanaweza kukupa mayai 250 kwa mwaka lakni hao wa second generation wataishia kukupa mayai kati ya 80 mpaka 100 ambapo iko chini mno.

Na kwa upande wa nyama 1st generation anaweza kukupa kilo 1.8~ 2.2 za nyama kwa siku 56 tu wakati 2nd generation wanuwezo wa kukupa kilo 0.5~0.7 za nyama kwa siku tajwa hapo juu.

Siri kubwa ya kuku hawa ni kuwa kadli kizazi kinavyoshuka zaidi ndivyo performance iko chini mno.
 
Ahsante kwa swali zuri. Iko hivi hayo makumpuni makubwa wao huwa ndio wenye parent stock na hawawezi kukuuzia na ilitokea wanakuuzia basi huwa ni kwa kukuuzia kama nyama na si vinginevyo wanafanya hivyo kwa sababu ya kwamba ukipata huyo jogoo wa parent stock na ukienda kuwachanganya na kuku wako basi kuku wako watakuwa na uwezo mkubwa wa uzalishaji hivyo wanaliepuka hilo kwa sana maana wataua biashara yao.

Hivyo hao parent stock wakizeeka majogoo yote huchinjwa na hapo hufuatiwa na matetea ya parent stock baada ya siku 7~10 maana kwa siku hizo mayai yote ambayo ni fertilized yanakuwa hayapo tena.

Swali la pili, Makampuni tajwa hapo juu hayana second generarion bali wana 1st generation ambao ndio wanawauzia nyie ili nyie mkapate nyama au mayai pakee na sio kupata mayai na kuyapeleka hatchery kwa ajili ya utotoleshaji hivyo kuishia kupata second generation ambayo kwa performance inakuwa iko chini mno...

Kwa mfano. vifaranga wa 1st generation wa kuroiler na sasso wanaweza kukupa mayai 250 kwa mwaka lakni hao wa second generation wataishia kukupa mayai kati ya 80 mpaka 100 ambapo iko chini mno...

Na kwa upande wa nyama 1st generation anaweza kukupa kilo 1.8~ 2.2 za nyama kwa siku 56 tu wakati 2nd generation wanuwezo wa kukupa kilo 0.5~0.7 za nyama kwa siku tajwa hapo juu...

Siri kubwa ya kuku hawa ni kuwa kadli kizazi kinavyoshuka zaidi ndivyo performance iko chini mno...

Shukran mkuu
 
Kurudi nyuma kvp mkuu? Mimi nadhani ukifuga kuku wa kienyeji kwa mfumo wa kisasa unaweza kupata matokeo chanya zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani uko sahihi. Sema wengi wetu tumekariri. Kuku wa kienyeji pure anafaida sana ukimaanisha biashara kweli.
Pia kunanjia nyingi za kuminimise cost kwa kuku kienyeji kuliko hao kuroiler.

Zaidi ya hapo nyama kuroiler hata kwa dawa haiwez fikia kwa kuku toka musoma. Watu wanaangalia sana muda bila kujifunza ni kwa namna gani ya kuweza kuzalisha kwa wingi na kupunguza gharama ili upate faida zaidi.

Mfano mimi naweza nikanunua labda matetea 100 na majogoo 10. Nikitarget kwa muda miezi sita na kumaanisha biashara kweli na naweza jikuta nafikisha mtaji hata wa kuku 3000 wakafi wewe utakuwa baado unahangaika na chotara wako ila mim naweza kuwa nishauza vifaranga hata 2000kwa kuku hata1000 na nikaangiza milion mbili wakat weye umejibana ukanunua vifaranga 1000 kwa miezi yote pata faida ya kiwango changu.
 
Hili tatizo ni kubwa kuliko inavyodhaniwa kwa kawaida First Generation au F1 ya kuku kama Kuroiler kufikisha 5kg ni kitu cha kawaida lakini huwa nawakuta kuroiler wako tu kawaida kama hawa kuku wetu wa kienyeji. Nahisi taasisi kama jkt sua nk zingetoa mifano. Au quality control mechanism lazima zitafutwe.
 
Hili tatizo ni kubwa kuliko inavyodhaniwa kwa kawaida First Generation au F1 ya kuku kama Kuroiler kufikisha 5kg ni kitu cha kawaida lakini huwa nawakuta kuroiler wako tu kawaida kama hawa kuku wetu wa kienyeji. Nahisi taasisi kama jkt sua nk zingetoa mifano. Au quality control mechanism lazima zitafutwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wafugaji wengi wanaibiwa sana.
 
Hili tatizo ni kubwa kuliko inavyodhaniwa kwa kawaida First Generation au F1 ya kuku kama Kuroiler kufikisha 5kg ni kitu cha kawaida lakini huwa nawakuta kuroiler wako tu kawaida kama hawa kuku wetu wa kienyeji. Nahisi taasisi kama jkt sua nk zingetoa mifano. Au quality control mechanism lazima zitafutwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
WATU TUNAPENDA SHORT CUTS
 
33 Reactions
Reply
Back
Top Bottom