witnessj
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 28,839
- 47,747
Mkuu nakushukuru sana yaani umenifungua nasoma sana agano la kale nakutana na hawa mafarisayo na masadukayo siwaelewi ni wakina nani!!Wasabato wanajumuishwa na hao wengine na wanatambuliwa kama mojawapo ya Christian cults zilizofanikiwa sana. Mojawapo ya mafundisho yao yanayopingana na Biblia ni hili: Wanaamini kuwa Yesu hakukamilisha kazi ya wokovu pale msalabani na kuanzia mwaka 1884 aliingia Patakatifu pa Patakatifu (Holly of Hollies) kuendelea kutuombea mbele ya Mungu Baba. Halafu wana kiherehere cha kutabiri kila jambo linalotokea duniani na kulihusisha na unabii. Yaani ukiwasikiliza aisee hutaweza kuishi. Ndiyo maana mwaka 1884 mwanzilishi wao aliwarubuni wafuasi wake kuwa mwaka huo Yesu anarudi wakauza kila kitu kumbe uwongo. Baadaye ndiyo ikasahihishwa kwamba mwaka 1884 haukuwa wa kurudi kwa Yesu bali ni Yesu alikuwa anahamia kwenye chumba cha Patakatifu pa Patakatifu huko mbinguni tayari kuanza kazi ya kutuombea mbele ya Mungu Baba.
Wanaweka msisitizo usio na sababu juu ya sheria za Musa hasa juu ya vyakula na ushikaji wa Sabato. Hakuna kula samaki wasio na magamba, wanyama wasio na kwato zilizogawanyika au wasiocheua na siku ya Sabato hairuhusiwi hata kupika. Msisitizo huu katika sheria za Musa hata Yesu aliukemea mara nyingi na alikuwa na ugomvi wa muda mrefu na Mafarisayo. Ndiyo maana aliwakemea walipomzonga baada ya kumponya mtu siku ya Sabato na kumwambia ajitwike godoro lake aende.
Wanadhani kuwa kushika sheria hizi ndiyo kutawaokoa na wanadhani kuwa kwa kushika misheria hii ya Musa basi wao ni watakatifu kuliko Wakristo wengine. Kumbe Biblia na Yesu mwenyewe walifundisha kinyume chake. Yaani ni mvurugano mtupu lakini wanaamini kuwa wao ndiyo watakatifu pekee watakaokwenda mbinguni.
Mara wakasirike pale wanafunzi wa Yesu wanakula bila kunawa yaani visheria vingi vigumu vugumu..
Kumbe ndo kama hawa Wasabato mkuu???