Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,362
- 11,249
Jimmy Carter ni rais wa Marekani wa 39 ambaye mnamo oktoba 1 mwaka 2023 alikuwa akisherehekea miaka yake 99 tangu kuzaliwa kwake mwaka 1924.
Rais huyo mstaafu alitwala Marekani kuanzia mwka 1977 mpaka 1981.
Miongoni mwa mafanikio ya utawala wake ilikuwa ni kufanikisha kutiiana saini ya kurejesha uhusiano kati ya Israe na Misri mnamo mwaka 1979.
Kwa sasa Raisi huyo amepelekwa kwenye nyumba zenye huduma za afya za kuhudumia wazee baada ya kupata maradhi ya saratani isiyotibika tena.
Katika umri huo Jimmy Carter ndiye raisi aliyewahi kuishi miaka mingi zaidi na aliyebaki hai muda mrefu zaidi baada ya kuondoka madarakani.
Muhimu kwa binadamu wengine ni kujifunza kwamba katika maisha inafika muda heshima zote zinaondoka na hata marafiki binafsi, urasimu wa kimadaraka vinaisha na kuonekana mzigo na familia na kutokuwa na umuhimu wowote wa kutafutwa ushauri kutoka ofisi uliyoihudumia.
Inafika wakati vyakula vyote vizuri unavimiliki lakini hata ukivitumia havibadilishi afya ya mwili.
Dawa zozote za kutibu za hali ya juu haziwezi tena kutibu maradhi yanayokupata.
Rais huyo mstaafu alitwala Marekani kuanzia mwka 1977 mpaka 1981.
Miongoni mwa mafanikio ya utawala wake ilikuwa ni kufanikisha kutiiana saini ya kurejesha uhusiano kati ya Israe na Misri mnamo mwaka 1979.
Kwa sasa Raisi huyo amepelekwa kwenye nyumba zenye huduma za afya za kuhudumia wazee baada ya kupata maradhi ya saratani isiyotibika tena.
Katika umri huo Jimmy Carter ndiye raisi aliyewahi kuishi miaka mingi zaidi na aliyebaki hai muda mrefu zaidi baada ya kuondoka madarakani.
Muhimu kwa binadamu wengine ni kujifunza kwamba katika maisha inafika muda heshima zote zinaondoka na hata marafiki binafsi, urasimu wa kimadaraka vinaisha na kuonekana mzigo na familia na kutokuwa na umuhimu wowote wa kutafutwa ushauri kutoka ofisi uliyoihudumia.
Inafika wakati vyakula vyote vizuri unavimiliki lakini hata ukivitumia havibadilishi afya ya mwili.
Dawa zozote za kutibu za hali ya juu haziwezi tena kutibu maradhi yanayokupata.