Hivi Mgao umeanza tena kimyakimya?

Hivi Mgao umeanza tena kimyakimya?

Baada tu ya kushika wadhifa wa uwaziri wa Nishati na madini, Prof Sospeter Muhongo alitamka kwa Watanzania, tena kwa mbwembwe na kujiamini kabisa kwamba mgawo wa umeme sasa utakuwa historia, kwani ulikuwa unapikwa tu kutokana na ufisadi nk nk.

Leo hii asubuhi ktk kipindi cha Nipashe cha Radio One Stereo, akielezea kukatika katika kwa umeme mara kwa mara hivi sasa amenukuliwa kwamba hali hiyo ni kutokana na miundombinu ya Tanesco ya usamazaji umeme iliyochoka kabisa na Tanesco inalishughulikia suala hilo.

Nauliza: Hivi wakati ule alipowaahidi Watz kuwa mgao wa umeme utakuwa historia, hakuwa na habari kwamba miundo mbinu ya Tanesco imechakaa?

Mimi naona mambo yanarudi kuwa ni yale yale tu -- hawa mawaziri wanatoka katika mfumo ule ule wa chama kilichochoka na cha kifisadi.

hapo kwa blue si kila umeme ukikatika ni mgao! na miundombinu kuchakaa si kitu cha ajabu! na ili kurekebisha inabidi kuzima, acha watu wafanye kazi mwaka 2015 sii mbali utaweka hao unaowataka umeme uszimike milele! na nchi itakuwa kama ahera!

 
Wana jf mnisaidie huu ni mgao wa umeme au matengenezo?maeneo mengi ya dar hayana umeme kuanzia saa tisa hadi sasa.
 
Tabia ya kukatika katika kwa UMEME hapa moshi bila taarifa inatia shaka,hivyo tunaomba wanachi wa moshi tupewe maelezo ni kwa nini umeme unakatika ovyo?Je, yule Profesa wa nishati,yupo hapa nchini?Si aliahidi hakutokuwa na mgao?Je ameshindwa au?Kwa mfano kuanzia saa tatu asubuhi hadi sasa bado umeme haujarudisha sehemu kubwa ya mji wa moshi.Hali hii imekuwepo kwa muda mrefu sasa hapa moshi mjini. halio hii inakera sana...
 
Bado nakumbuka kauli ya waziri wa nishati na madini kwamba kusingekuwa na mgawo wa umeme mwaka huu.Ni zaidi ya wiki sasa mgao wa umeme umeanza kimya kimya sijamsikia waziri wa nishati na madini akitoa kauli yoyote,sijamsikia kaimu mkurugenzi mtendaji wa TANESCO akitujuza kulikoni mgao umeanza kwa makali na ghafla kiasi hiki au kuna hujuma au utabiri wake ulikosa mashiko ya kisayansi ?.

 
Alitoa kauli kabla hajaijua serikali hii...amekuja kungundua kinachoongelewa na wanasiasa na kinachotekelezwa tofauti.!
 
Bado nakumbuka kauli ya waziri wa nishati na madini kwamba kusingekuwa na mgawo wa umeme mwaka huu.Ni zaidi ya wiki sasa mgao wa umeme umeanza kimya kimya sijamsikia waziri wa nishati na madini akitoa kauli yoyote,sijamsikia kaimu mkurugenzi mtendaji wa TANESCO akitujuza kulikoni mgao umeanza kwa makali na ghafla kiasi hiki au kuna hujuma au utabiri wake ulikosa mashiko ya kisayansi ?.


Na wewe hatujakuskia ukikanusha ule umbea wako wa Lema kupigwa jukwaani Arusha.
 
Facilitator bahati mbaya wewe Lema kwako ni nabii hakosei,hana dhambi,hahojiwi na hilo litakuja wacosts mbele ya safari.Nilichosema juu ya Lema kinasimama mpaka leo ukijiondoa katika box la ushabiki utabaini ukweli mweupe.Sasa kama unataka nibadili nilichokiandika ili nikufurahishe utasubiri sana.

Bahati mbaya mada si Lema ukitaka nikumwagie habari zaidi anzisha uzi mwingine hapa tunajadili kauli ya waziri wa nishati na madini.


Na wewe hatujakuskia ukikanusha ule umbea wako wa Lema kupigwa jukwaani Arusha.
 
Last edited by a moderator:
Facilitator bahati mbaya wewe Lema kwako ni nabii hakosei,hana dhambi,hahojiwi na hilo litakuja wacosts mbele ya safari.Nilichosema juu ya Lema kinasimama mpaka leo ukijiondoa katika box la ushabiki utabaini ukweli mweupe.Sasa kama unataka nibadili nilichokiandika ili nikufurahishe utasubiri sana.

Bahati mbaya mada si Lema ukitaka nikumwagie habari zaidi anzisha uzi mwingine hapa tunajadili kauli ya waziri wa nishati na madini.

Ni kweli, hapa si topic ya Lema, na nataka pia ujue (in principle) kuwa ulidanganya watu hapa. Na vilevile, kwangu mimi Lema si nabii kama unavyotaka kulazimisha hapa. Mimi nilikuwepo mkutanoni na nilishuhudia mwanzo mpaka mwisho wa tukio lenyewe. Kanusha kwanza ulichosema wewe ndo upate legitimacy ya kudai Prof. Muhongo akanushe kauli yake. PERIOD.
 
Siasa za bongo kweli ajabu sana kinadharia wanadai hamna mgawo lakini kivitendo upo,hamna cku inapita bila hawa jamaa wa hilo shirika kukata umeme tena bila taarifa,wenye kujua tatizo watujuze ili tupangilie namna ya kuishi kwa umeme wa mgao
 
yule bint msemaji wa hilo shirika ndo anaongoza kwa propaganda ambazo hazitusaidii sisi,this frequent power woes is just killing us
 
kaka we acha, tu nadhani kunamgao hapa moshi, niko mitaa ya soweto hata sasa hakuna umeme, kila siku ikifika sa moja jioni tu kosa, halafu waweza kukatika nakurudi zaidi ya mara kumi ndani ya masaa 6. kwa kweli hawa jamaa siowaungwana kabisa wanatuharibia ratiba zetu na malizetu bila utaratibu, haieleweki kama ni matengenezo au ni ni hujuma .... wanakera sio siri
 
Hapa tuko gizani unaambiwa hakunaga wala hautotokea mgao bongo. Mhh kweli hui ndio bongo
 
si moshi mjini tu, ni maeneo mengi ktk mkoa wa k'njaro. umeme unakatwa kwa masaa 24 unarudi kwa sekunde 3 unakatwa tena masaa 20, tena bila taarifa, hii ni kero kwa wateja
 
si moshi mjini tu, ni maeneo mengi ktk mkoa wa k'njaro. umeme unakatwa kwa masaa 24 unarudi kwa sekunde 3 unakatwa tena masaa 20, tena bila taarifa, hii ni kero kwa wateja

Mkuu kweli maana hadi Rombo huku unakatika more than 24 hrs, sijui tatizo nini duuu!
 
Niko mkoani morogoro kwa sasa kwa issue ya kikazi nashangaa hapa umeme umekatika ghafla ndo nauliza wadau ambao either ni wafanyakazi wa Tanesco au mna undugu na Tanesco kuna mgao au ni tatizo la mtandao?
 
Huku sinza dar unakatika kila baada ya dk 2 hatujui nini shida.
 
Nimeshangaa,leo huku home kwetu wamekata umeme si chini ya mara kumi kutwa mzima,chakushangaza zaidi ni withini 5 minutes wanarudisha
 
Siku hizi hawaruhusiwi kutumia neno MGAO WA UMEME, wanatumia maneno kama kukata miti inayohatarisha njia za umeme, kurekebisha hitilafu n.k......(Mawazo yangu)
 
Back
Top Bottom