Hivi 'mfumo dume' ndio nini?

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,349
6,476
Jana kwenye redio Ujerumani Bi. Sara Batilda Burian aliulizwa alivyomfahamu marehemu Wangari, akasema alikuwa jasiri na kuweza kupambana na "mfumo dume" uliopo duniani. Nikapata maswali mengi: hivi nje ya dunia kuna "mfumo jike"? Hivi nini maana ya dhana hii - mfumo dume? Hivi huku sio kusigina Bible? Je, ana-question kazi na maagizo ya kwenye Bible? Je, 'mfumo jike' ukoje? au mfumo 'mseto - jike+dume ukoje?
 
Mfumo dume umemfanya Halima Mdee aingie madarakani kupitia Mbowe.
 
Mfumo dume umemfanya Halima Mdee aingie madarakani kupitia Mbowe.

Mfumo dume umemfanya Mwita awe kibaraka wa Magamba, awatetee hata km wako wrong mradi anapewa mia mia za kuilea family yake!!
 

Nenda pale TGNP, TAMWA, WILAC au TAWLA watakupa semina ya kutosha...............na ninadhani wapo humu subiri watakuja kukuelimisha
 
kama siyo wanaume nyie hamuwezi kabisa, usikae kiti cha baba hicho, uchagani nyama inapikwa nzima nzima ni lazima baba akatekate vipande vipande awagawie nyie plus mama yenu, kahawa ni mali ya baba, etc.
 

Kitaalamu mfumo dume ni mfumo ambao wanaume wana sauti zaidi kama ambavyo kinadharia inawezekana kukaweko na mfumo jike yaani kwa maana kwamba, kama itatokea nchi fulani au muundo fulani wa utawala wanawake ndio wakawa wenye nafasi kubwa na sauti kubwa na ndio wanaotangulizwa mbele katika maamuzi tunaweza kuuita mfumo huo kuwa ni mfumo jike. Lakini mfumo dume ndio ambao umeondokea kuwa mashuhuri kutokana na harakati zilizojitokeza katika miaka ya hivi karibuni za Ufeministi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…