Hivi meno ya tembo ni malighafi ya nini?

nauza meno ya ngiri!!!! pia nanunua nguruwe hua nasafirisha kupereka nchi za arabuni na visiwa vya zbar!
 
Hello Mkuu, meno ya tembo huwa yanatumika kutengenezea mapambo kama vile vidani, pete, heleni na vitu vingine vya kuvaa kwenye miili ya binadamu. Vilevile, hutumika kutengenezea sanamu za viongozi au watu mashuhuri wenye michango mikubwa katika maendeleo ya nchi. Katika nchi za mashariki ya mbali, bidhaa hizo hununuliwa kwa bei kubwa na wanao nunua ni watu wenye ufahari kama vile wafalme, ma rais na watu wengine kama hao. Kumiliki bidhaa zilizotengenezwa kutokana na malighafi ya meno ya tembo ni jambo la ufahali kwa mataifa hayo na mtu anayemiliki malighafi hizo huthaminiwa katika jamii. Kwa hiyo ni utamaduni tu uliojengeka katika jamii hizo kumiliki bidhaa zilizotengenezwa na malighafi ya meno ya tembo kuwa ni wa kifahali.

Je huwezi kutengenezea sanamu za watu wasio mashuhuri na wasio na michango mikubwa katika Jamii?
Nauliza tu.
 
Meno ya Tembo hutumika sambamba na meno ya kiboko na seal (wanyama wa baharini waliochomoza meno kwa mbele, kama Ngiri) ila wahitaji huthamini zaidi meno ya Tembo kwani yana ukubwa unaozalisha bidhaa bora na nyingi zaidi kulinganisha na hayo meno mengine......

Zaidi ya kutengeneza urembo meno ya Ndovu pia hutengeneza keyboards za piano na baadhi ya bidhaa za asili za kiasia (haswa Japan) ambazo hutumiwa na familia za kifalme na hizo hazina malighafi mbadala za kutengenezea zaidi ya meno ya Tembo.

Bidhaa karibia zote zinaweza pia kutengenezwa kwa malighafi mbadala kama plastics...lakini kwa bidhaa hizo hizo zikitokana na meno ya Tembo huuzwa kwa watu maalum (matajiri au familia za kifalme) kwa bei ya juu sana kama dhahabu na ni fahari kwa mwenye uwezo kumiliki kifaa kilichotengenezwa na meno ya Tembo kwani bidhaa zinazofanania hizo zinamilikiwa pia na wengine lakini hazina thamani hiyo.

Hata kama zitatengenezea mipira ya pool table kama mchangiaji mmoja alivyoeleza hapo juu...lakini kamwe sio hii mipira tutakayoikuta dukani...mipira hii itakuwa ni kwa ajili ya watu maalum kama matajiri, watu maarufu n.k.

Sorry hapa nilitaka kumaanisha WALRUSES na sio SEALS,ingawa Walruses pia wanaishi baharini sehemu zenye baridi na barafu, wamechomoza meno kama Ngiri.........
 
Je huwezi kutengenezea sanamu za watu wasio mashuhuri na wasio na michango mikubwa katika Jamii?
Nauliza tu.

Hakuna sheria inayokataza watu wa kawaida kutengeneza sanamu zao. Isipokuwa watu mashuhuri sanamu zao hutumiwa kama vielelezo katika sehemu muhimu za kihistoria kama vile kwenye makumbusho (Museums), round about za barabara, au sehemu zinazokutanisha watu wa aina mbalimbali kitaifa na kimataifa. Mfano, sanamu ya Mwl. JK. Nyerere inafaa kuwepo katika makumbusho ya taifa, au uwanja wa ndege Dar sababu umetumia jina lake! Mtu wa kawaida itakuwa kama hasara, huwezi kutengeneza ukaiweka ndani tu kwani ni gharama kubwa mno!
 
Nasikia tu kuwa yanatumika kutengenezea madawa ya maradhi ya saratani ktk nchi za Asia japo haijathibitishwa kisayansi
 
Tembo hana Pembe!!

mkuu tembo au kwa jina jingine ndovu ana pembe mbili,izo pembe mbili ni meno chonge , ikumbukwe tembo ana meno 28 , yaani 26 ndani na mawili yanayochoma fizi na kutokea nje,ayo ndo yanaitwa pembe lakini pia ni meno...

Tenbo anazo pembe, wanyama wengi wenye pembe huw pembe zao zinaangalia juu lakini Tembo pembe zake zinaangalia chini.

jina pambe limetokana na pembeni yani kiungo cha mwili kinachoota pembezoni mwa uso au juu.

pia huwezi kusema yale ni meno kazi ya meno ni kulainisha chakula au kusaga sasa lini unaona Tembo anatafuna kwa kutumia pembe.
 
Tenbo anazo pembe, wanyama wengi wenye pembe huw pembe zao zinaangalia juu lakini Tembo pembe zake zinaangalia chini.

jina pambe limetokana na pembeni yani kiungo cha mwili kinachoota pembezoni mwa uso au juu.

pia huwezi kusema yale ni meno kazi ya meno ni kulainisha chakula au kusaga sasa lini unaona Tembo anatafuna kwa kutumia pembe.

I'm sorry to say this, ila brother HUJUI UNACHOKIONGEA!!! Hivyo naomba nikueleweshe kidogo, kwanza kabisa kama hukujua Tembo ana Meno 26, 12 kati ya hayo ni premolars( au magego ya kati), 12 mengine ni molars (au magego ya nyuma) na mawili ni Incisors. Kwa tembo na baadhi ya wanyama meno haya hukua na kuchomoza nje ya kinywa!! Composition(au mchanganyiko wa kemikali) wa meno hayo ni sawa kabisa na meno mengine hivyo huwezi kusema ni pembe huku pembe na meno vina composition tofauti!! Pia ukisema faida pekee ya meno ni kulainisha chakula basi hata hawa wanyama pia hizo ni pembe na sio meno!
wildboarpics%203.jpg

800px-Noaa-walrus22.jpg

common_hippo_mouth.jpg
 
kushinda hii vita ni kupiga marufuku vinavyotengenezwa na meno ya tembo kuuzwa madukani na kokote kule,
 
Tembo hana Pembe!!

mkuu tembo au kwa jina jingine ndovu ana pembe mbili,izo pembe mbili ni meno chonge , ikumbukwe tembo ana meno 28 , yaani 26 ndani na mawili yanayochoma fizi na kutokea nje,ayo ndo yanaitwa pembe lakini pia ni meno...

I'm sorry to say this, ila brother HUJUI UNACHOKIONGEA!!! Hivyo naomba nikueleweshe kidogo, kwanza kabisa kama hukujua Tembo ana Meno 26, 12 kati ya hayo ni premolars( au magego ya kati), 12 mengine ni molars (au magego ya nyuma) na mawili ni Incisors. Kwa tembo na baadhi ya wanyama meno haya hukua na kuchomoza nje ya kinywa!! Composition(au mchanganyiko wa kemikali) wa meno hayo ni sawa kabisa na meno mengine hivyo huwezi kusema ni pembe huku pembe na meno vina composition tofauti!! Pia ukisema faida pekee ya meno ni kulainisha chakula basi hata hawa wanyama pia hizo ni pembe na sio meno!
wildboarpics%203.jpg

800px-Noaa-walrus22.jpg

common_hippo_mouth.jpg
Hivi kumbe mifupa ya Mammals huwa kuna mingine inaundwa na composition tofauti na calcium carbonate dah! sikujua aisee!!

Okay unajua kiswahili kigumu hizo pembe kwa jina la kitaalamu zinaitwa Tusks quite differ from teeth.

any way asante kwa somo naona leo nimepata kitu kipya.
 
Hivi kumbe mifupa ya Mammals huwa kuna mingine inaundwa na composition tofauti na calcium carbonate dah! sikujua aisee!!

Okay unajua kiswahili kigumu hizo pembe kwa jina la kitaalamu zinaitwa Tusks quite differ from teeth.

any way asante kwa somo naona leo nimepata kitu kipya.

Yes jino lina composition tofauti. Like, pembe hua ni hard extension toka kwene fuvu (mostly made of skin/hair kama kwa case ya rhino) ila teeth ni very different, one difference i can think of ni ENAMEL, teeth has enamel huku horns don't. I saw a documentary once on the subject so you can verify everything on Google, its all legit. Yeah TUSK ni sahihi, tena si kwa tembo 2 bali kwa meno ya wanyama wote hao yaliyotoka nje,ka niliowaweka juu hapo. You're welcome
 
Yes jino lina composition tofauti. Like, pembe hua ni hard extension toka kwene fuvu (mostly made of skin/hair kama kwa case ya rhino) ila teeth ni very different, one difference i can think of ni ENAMEL, teeth has enamel huku horns don't. I saw a documentary once on the subject so you can verify everything on Google, its all legit. Yeah TUSK ni sahihi, tena si kwa tembo 2 bali kwa meno ya wanyama wote hao yaliyotoka nje,ka niliowaweka juu hapo. You're welcome

Can skin and hair made a Tusk?
 
Can skin and hair made a Tusk?
Duh , feel like we're going off topic here ila just to ans you! NO, Tusks as i said ni Meno na meno Main composition ni 'Ca' and Enamel on top of it! Ila Pembe/HORNS can and are usually made of tough skin and hair!!
 
Duh , feel like we're going off topic here ila just to ans you! NO, Tusks as i said ni Meno na meno Main composition ni 'Ca' and Enamel on top of it! Ila Pembe/HORNS can and are usually made of tough skin and hair!!
Where did you find this imposture?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom