Chatumkali
JF-Expert Member
- Sep 9, 2011
- 2,037
- 458
Kituo cha TV cha TBC1 kimeonyesha shule ya msingi ya ajabu katika taarifa ya habari ya saa mbil usiku.Shule hiyo iliyopo mkoani Rukwa ina hali mbaya sana.
Watoto wamekaa kwenye mawe na magogo ya miti!Wlimu wanafundisha kwenye kipande cha bati kama ndio ubao!Madarasa yamejengwa kwa kuta za nyasi.
Cha kusikitisha mbunge wa eneo husika (jina sikulidaka vizuri) anamlaumu diwani wa eneo husika kwamba eti anafanya kazi gani! Halafu anasisitiza kwamba yeye binafsi hajawahi kuona shule kama hiyo katika maisha yake! Sasa yeye kama mbunge anafanya kazi gani?
Bungeni anamuwakilisha nani kama shule iliyopo ndani ya jimbo lake haijui? Ina maana wakati anapita huko kuomba kura hakuiona hiyo shule kituko? Hivi mbunge kama huyu anafaa kuwa mwakilishi wa watu kweli?
INASIKITISHA SANA!
Watoto wamekaa kwenye mawe na magogo ya miti!Wlimu wanafundisha kwenye kipande cha bati kama ndio ubao!Madarasa yamejengwa kwa kuta za nyasi.
Cha kusikitisha mbunge wa eneo husika (jina sikulidaka vizuri) anamlaumu diwani wa eneo husika kwamba eti anafanya kazi gani! Halafu anasisitiza kwamba yeye binafsi hajawahi kuona shule kama hiyo katika maisha yake! Sasa yeye kama mbunge anafanya kazi gani?
Bungeni anamuwakilisha nani kama shule iliyopo ndani ya jimbo lake haijui? Ina maana wakati anapita huko kuomba kura hakuiona hiyo shule kituko? Hivi mbunge kama huyu anafaa kuwa mwakilishi wa watu kweli?
INASIKITISHA SANA!