Nikueleze mara ngapi kuwa haiwezekani kuprove negative?
Nimekupa mfano wa watu wawili kwenye chumba kisicho na kitu halafu kati ya hao watu wawili mmoja akadai ndani ya hicho chumba kuna kiti. Mwenzake akakanusha kwa kusema hakuna hicho kiti. Je hapa jukumu la kuthibitisha kuwa kiti kipo ndani ya hicho chumba ni nani?
Wewe inaonyesha huelewi logic ndiyo maana unarudia jambo nalokuambia.
Mimi nitaweza vipi kusema sababu za kutokuwepo uchawi angali nimeshasema haupo?
Hapo kinachotakiwa ni mwenye kudai uchawi upo atoe hoya mimi nikosoe kwa mapungufu nitakayo baini kwenye utetezi huo.
Ni sawa wewe unituhumu nimekuibia pesa yako halafu tena unaniambie niseme kipi kimenifanya nisidhani nimekuibia.
Hapo mantiki ipo wapi?
Ukishindwa kungamua haya nitajua wewe hujaiva kwenye kuchambua mambo critically.
Mkuu, embu nieleweshe,Tatizo mkuu hatuelewani kwa sababu unanipeleka ambapo mie sipo. Haya madai ya kuwepo uchawi tumezaliwa na kuyakuta,sasa wewe pia unadai kuwa hakuna huo uchawi ambao watu wanadai kuwa upo.
Kwahiyo mie nilichotaka kwako ni sababu zilizokufanya kuona hili jambo la kuwepo uchawi si la kweli na ndiyo maana ukasema hakuna uchawi,maana umepinga madai ya kuwepo uchawi hivyo lazima utakuwa na sababu zilizokufanya ukatae hayo madai ya kuwepo uchawi na ndiyo hicho nachotaka.
Hivyo sio kwamba mie nataka ueleze kwanini hakuna uchawi kama ulivyosema.
Kwani akili zipo? Mbona hatuzioni?Mbona hatuuoni
Unapaswa ufahamu kuwa anachokifanya yeye hapa ni kupinga madai ya kuwepo uchawi hivyo lazima atakuwa na sababu zilizofanya apinge kuwepo huo uchawi ambao watu wanadai kuwa upo, sasa mie nataka kuzijua hizo sababu zilizofanya apinge kuwepo huo uchawi ambao watu wanadai kuwa upo.Mkuu, embu nieleweshe,
Hivi? 'kuelezea sababu zinazofanya kwamba jambo la uchawi sio kweli' na 'kuelezea kwanini hakuna uchawi' ni mambo mawili tofauti?
"Kwanini" "kwasababu"
Kwani mungu unamuonaMbona hatuuoni
Nimeshafika, ni mtazamo wake na yuko sahihi kwa muktadha wake ILA kama ni mwamini wa dini fulani basi si msoma maandiko labda tu awe mpaganiNgoja my kaka Mshana aje.
Cc Mshana Jr
Namuomba akiweza Kesho aje Msata maana anasema ameishia kusimuliwa tu....mshana jr njoo uumpe facts huyu ana beep
Facts [emoji115] [emoji106] [emoji106]Inawezaka ni story kwako lkn kwa wengine is not a story.
Maswali.
1. Ww ni dini gani?
2. Unahudhuria kwenye nyumba za ibada
3. Una amini Mungu yupo?
4. Una amini shetani yupo?
5. Unaamini Majini yapo?
6. Una amini kuna nguvu za Mungu?
7. Una amini kuna nguvu za giza?
6. Una amini vitabu vya dini?
Tuanzie hapo kwanza. Nahitaji majibu. Ukishajibu nitakupa jibu kuhusu kile unachoamini