Kaduguda
JF-Expert Member
- Aug 1, 2008
- 724
- 641
Kampuni za mizigo bandarini Dar zalalamikia ushuru mpya
Na Leon Bahati
KAMPUNI zinazotoa huduma ya kupakua na kupakia mizigo (forwarding and Clearing) Bandari ya Dar es Salaam zimegoma na kusababisha hofu ya kuzuka kwa mkanganyiko wa uchumi nchini
Pamoja na kugoma, kampuni hizo zimedai zinafikiria kuitumia Bandari ya Mombasa nchini Kenya katika kupakua na kupakia mizigo ya kibiashara.
Habari zilizolifikia gazeti hili zilisema baadhi ya kampuni hizo zinatishia kuondoka Dar es Salaam baada ya Serikali kupandisha ushuru kwa karibu asilimia 50 tangu Jumatano iliyopita.
Baadhi ya wamiliki wa kampuni hizo , waliliambia Mwananchi Jumapili kuwa serikali imebadili mfumo wake wa kutoza ushuru wa forodha ambapo kila kontena linatozwa kati ya Sh20 milioni na 40 milioni, bila kujali aina ya mzigo uliopo ndani.
Lakini mchumi mmoja , alisema jana kwamba wakati wote mfanyabiashara akiongezewa gharama, basi atakayeumia ni mlaji (wananchi).
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Hamfrey Mushi alisema katika mazingira hayo, ni vigumu kupambana na mfumuko wa bei.
Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina gazetini, baadhi ya wenye kampuni walidai, awali walikuwa wanalipa ushuru kulingana na thamani ya bidhaa zilizopo ndani ya kontena.
Lakini mfumo mpya, uliobuniwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) unatoza Sh 20 milioni kwa kila kontena lenye urefu wa futi 20 na Sh.40 milioni kwa kila kontena lenye futi 40.
Bila kuangalia thamani.
Mwananchi Jumapili lilipowasiliana na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo alisema kuwa yupo safari ya kikazi, Kilosa Morogoro, na kushauri kuwasiliana na Katibu Mkuu wa Wizara, Ramadhan Kijja.
Hata hivyo, Kijja hakupatikana kupitia simu yake ya mkononi na hata ile ya ofisini kwake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa Kodi na Uhusiano wa TRA, Protas Mmanda naye hakupatikana ili kufafanua juu ya jambo hilo baada ya simu yake nayo kutopokelewa.
Pamoja na hali hiyo, habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa baadhi ya watendaji wakuu wa TRA walikuwa kwenye vikao mwishoni mwa wiki ili kujadili hatma ya mgogoro huo.
Bandari ya Dar es Salaam imekuwa ikishutumiwa kutokana na utendaji usioridhisha wa Ticts, ambao unasababisha foleni kubwa ya meli zinazosubiri kupakuliwa.
Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawamba alisema kuwa hali hiyo imekuwa ikisababishia serikali hasara ya Sh20, milioni kila siku kwa kila meli.
Wakizungumzia juu ya utendaji mbovu wa bandari hiyo pamoja na kuongezeka kwa gharama pamoja na ushuru wa forodha, wataalam kadhaa wa uchumi walisema athari zake ni kubwa kwa uchumi na kwamba zitaongeza ugumu wa maisha hasa kwa wananchi wa kipato cha chini.
Aliitaka serikali kuchukua hatua za haraka za kupambana na hali hiyo vingionevyo, hali ya uchumi wa nchi itaendele kudorora na hali ya maisha itazidi kuwaendea vibaya watu wa kipato cha chini.
SOURCE: MWANANCHI - 2/21/2009
My take: Naomba wadau mnieleweshe hivi inakuwaje container lilipiwe ushuru flat rate, maana hata maji ya DAWASCO siku hizi kuna meter unalipa kwa kadri unavyotumia. Sasa mtu kaleta container kisha unasema ni flat rate hii wadau imekaaje? JF kuna wadau wa aina zote hebu ,lio TRA mtuambie kulikoni hata mkafikia maamuzi hayo?
Na Leon Bahati
KAMPUNI zinazotoa huduma ya kupakua na kupakia mizigo (forwarding and Clearing) Bandari ya Dar es Salaam zimegoma na kusababisha hofu ya kuzuka kwa mkanganyiko wa uchumi nchini
Pamoja na kugoma, kampuni hizo zimedai zinafikiria kuitumia Bandari ya Mombasa nchini Kenya katika kupakua na kupakia mizigo ya kibiashara.
Habari zilizolifikia gazeti hili zilisema baadhi ya kampuni hizo zinatishia kuondoka Dar es Salaam baada ya Serikali kupandisha ushuru kwa karibu asilimia 50 tangu Jumatano iliyopita.
Baadhi ya wamiliki wa kampuni hizo , waliliambia Mwananchi Jumapili kuwa serikali imebadili mfumo wake wa kutoza ushuru wa forodha ambapo kila kontena linatozwa kati ya Sh20 milioni na 40 milioni, bila kujali aina ya mzigo uliopo ndani.
Lakini mchumi mmoja , alisema jana kwamba wakati wote mfanyabiashara akiongezewa gharama, basi atakayeumia ni mlaji (wananchi).
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Hamfrey Mushi alisema katika mazingira hayo, ni vigumu kupambana na mfumuko wa bei.
Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina gazetini, baadhi ya wenye kampuni walidai, awali walikuwa wanalipa ushuru kulingana na thamani ya bidhaa zilizopo ndani ya kontena.
Lakini mfumo mpya, uliobuniwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) unatoza Sh 20 milioni kwa kila kontena lenye urefu wa futi 20 na Sh.40 milioni kwa kila kontena lenye futi 40.
Bila kuangalia thamani.
Mwananchi Jumapili lilipowasiliana na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo alisema kuwa yupo safari ya kikazi, Kilosa Morogoro, na kushauri kuwasiliana na Katibu Mkuu wa Wizara, Ramadhan Kijja.
Hata hivyo, Kijja hakupatikana kupitia simu yake ya mkononi na hata ile ya ofisini kwake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa Kodi na Uhusiano wa TRA, Protas Mmanda naye hakupatikana ili kufafanua juu ya jambo hilo baada ya simu yake nayo kutopokelewa.
Pamoja na hali hiyo, habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa baadhi ya watendaji wakuu wa TRA walikuwa kwenye vikao mwishoni mwa wiki ili kujadili hatma ya mgogoro huo.
Bandari ya Dar es Salaam imekuwa ikishutumiwa kutokana na utendaji usioridhisha wa Ticts, ambao unasababisha foleni kubwa ya meli zinazosubiri kupakuliwa.
Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawamba alisema kuwa hali hiyo imekuwa ikisababishia serikali hasara ya Sh20, milioni kila siku kwa kila meli.
Wakizungumzia juu ya utendaji mbovu wa bandari hiyo pamoja na kuongezeka kwa gharama pamoja na ushuru wa forodha, wataalam kadhaa wa uchumi walisema athari zake ni kubwa kwa uchumi na kwamba zitaongeza ugumu wa maisha hasa kwa wananchi wa kipato cha chini.
Aliitaka serikali kuchukua hatua za haraka za kupambana na hali hiyo vingionevyo, hali ya uchumi wa nchi itaendele kudorora na hali ya maisha itazidi kuwaendea vibaya watu wa kipato cha chini.
SOURCE: MWANANCHI - 2/21/2009
My take: Naomba wadau mnieleweshe hivi inakuwaje container lilipiwe ushuru flat rate, maana hata maji ya DAWASCO siku hizi kuna meter unalipa kwa kadri unavyotumia. Sasa mtu kaleta container kisha unasema ni flat rate hii wadau imekaaje? JF kuna wadau wa aina zote hebu ,lio TRA mtuambie kulikoni hata mkafikia maamuzi hayo?