MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Dini zetu zinatufundisha tuamini kuwa ukitenda mema, ukawacha maovu na ukamwamini Mungu wako, utaingia Peponi. Mara nying kwenye nyumba za ibada na mihadhara tunaambiwa:
"Usishughulishwe na raha za Dunia, fikiria kesho siku ya Hukumu. Tenda wema, epuka maovu, saidia, swali, usiibe..." na mengine kibao tu ambayo ukiyatenda unaahidiwa kwenda Peponi.
Dini hizo hizo zinatufanya tuamini kuwa ni sisi tu wa dini yetu ndio tulio sahihi na wale wa dini nyengine wamepotea. Wataingia Motoni.
Mfano, ikiwa Myahudi anaamini yeye ni sahihi na Waislamu na Wakristo wamepotea; Muislamu anaamini hivyo hivyo dhidi ya Wakristo na Wayahudi; huku Wakristo wakiamini kuwa wao ndio wameokoka na Wakristo na Waislamu wote...Jahannam! hii ina maana kuwa hakuna PEPO. SOTE tutaingia MOTONI kwa sababu hatufuati dini ya wengine!
"Usishughulishwe na raha za Dunia, fikiria kesho siku ya Hukumu. Tenda wema, epuka maovu, saidia, swali, usiibe..." na mengine kibao tu ambayo ukiyatenda unaahidiwa kwenda Peponi.
Dini hizo hizo zinatufanya tuamini kuwa ni sisi tu wa dini yetu ndio tulio sahihi na wale wa dini nyengine wamepotea. Wataingia Motoni.
Mfano, ikiwa Myahudi anaamini yeye ni sahihi na Waislamu na Wakristo wamepotea; Muislamu anaamini hivyo hivyo dhidi ya Wakristo na Wayahudi; huku Wakristo wakiamini kuwa wao ndio wameokoka na Wakristo na Waislamu wote...Jahannam! hii ina maana kuwa hakuna PEPO. SOTE tutaingia MOTONI kwa sababu hatufuati dini ya wengine!