Fohadi
JF-Expert Member
- Jul 24, 2020
- 770
- 2,408
Binafsi sio mpenzi wa chama chochote cha siasa japo nafuatilia siasa kwa sababu siasa ina affect sekta zingine zote za kimaisha hivyo upatikanaji au uwepo wa viongozi bora ni kitu muhimu sana kwa maendeleo. Na ili tupate maendeleo, tunahitaji mawazo mbadala kila kukicha.
Inasikitisha kuona kuna watu wamekuwa 'Monopoly' wa majimbo yao miaka nenda rudi. Na kibaya zaidi kwa miaka yote waliyosimamia majimbo bado matatizo ni yaleyale. Kuna muda unashangaa kuona mbunge amekaaa kwenye hilo jimbo kwa zaidi ya miaka 20 lakini bado kila mwaka wa uchaguzi vipaumbele vyake ni vilevile. Hii ni kwa wabunge wote wa chama tawala na upinzani.
Unakuta mtu toka uchaguzi wa 2005 kwenye jimbo lake hoja zake kuu zilikuwa MAJI, AFYA NA ELIMU. Mtu huyo huyo ndani ya jimbo hilohilo mwaka 2020 anakuja na hoja zilezile na mbaya zaidi anakuwa na nguvu ya kushinda kwa sababu amesha monopolize ile nafasi. Na usishangae 2025 panapo uhai akaja kugombea na hoja zilezile.
Ni vema ukomo kwenye hizi nafasi ukaangaliwa ili kuleta mawazo mapya. Itapendeza kama mtu atakaa jimboni kwa mihula 2 tu kama ilivyo nafasi ya urais. Iwekwe sheria kuwa hairuhusiwi mtu ambae tayari ni mbunge kugombea ubunge zaidi ya mara 2. Hii itasaidia hata watu wengine wawe na access ya kula keki ya taifa na kuwatumikia wananchi. Hii itasaidia kuondoa ile dhana iliyojengeka kuwa jimbo fulani ni la fulani.
Nawasilisha.
Unakuta mtu toka uchaguzi wa 2005 kwenye jimbo lake hoja zake kuu zilikuwa MAJI, AFYA NA ELIMU. Mtu huyo huyo ndani ya jimbo hilohilo mwaka 2020 anakuja na hoja zilezile na mbaya zaidi anakuwa na nguvu ya kushinda kwa sababu amesha monopolize ile nafasi. Na usishangae 2025 panapo uhai akaja kugombea na hoja zilezile.
Ni vema ukomo kwenye hizi nafasi ukaangaliwa ili kuleta mawazo mapya. Itapendeza kama mtu atakaa jimboni kwa mihula 2 tu kama ilivyo nafasi ya urais. Iwekwe sheria kuwa hairuhusiwi mtu ambae tayari ni mbunge kugombea ubunge zaidi ya mara 2. Hii itasaidia hata watu wengine wawe na access ya kula keki ya taifa na kuwatumikia wananchi. Hii itasaidia kuondoa ile dhana iliyojengeka kuwa jimbo fulani ni la fulani.
Nawasilisha.