Hivi kuna mwanamke yeyote anaekubali hili?

Eiyer

JF-Expert Member
Apr 17, 2011
28,258
20,708
Sikumbuki kama jambo hili lilishajadilia,lakini hata kama tayari lilishajadiliwa nilitaka kujua na nina sababu.Ni kwamba tangu nizaliwe sijawahi kuona ndoa ya uke wenza ina amani baina ya hao wake wawili au wa idadi yoyote.Miezi miwili iliyopita kuna binti aliolewa na mume mwenye mke tayari,lakini leo binti ameachika na amerudi kwao kwa sababu,tangu ameolewa vurugu na mke mkubwa haziishi,bi mdogo kuumwa kila leo,akipelekwa hospital ugonjwa hauonekani,lakini watu wazima wamemwambia kuwa ake mwenzie ndie anamroga!Nae binti kusikia hivyo amefungasha na kuondoka kwa mumewe na anadai talaka.Huo ni mfano mmoja,najua iko mingi,nimekua nikijiuliza sana;hivi kuna mwanamke anakubali kushea mume na mwanamke mwenzie bila kulazimishwa na dini,umaskini,wazazi au mila?Kama hakuna kwanini wanawake waendelee kujitesa na ndoa hizi?Au wapo wanakubali ndoa hizi?Kama wapo ningependa kusikia kutoka kwao . . . . . . !!!!
 
wapo wanaopatana, haswa kama wana kazi za nje, muhimu kuungana ili ratiba ikivurugika kidogo washtuane
 
Ni ngumu sana hii
Huu ni ubinafsi tu wwanaume na tamaa zao
Cjui kama wanawake wangeamua kuwa na waume wawili kama pangekalika maana huu mkuki umeelekezwa upande mmoja tu.!
 
Ni kweli inawezekana ila kwa nadra sana na pia sio kwa kizazi hiki! Nina mfano pia, wakati naanza kazi maeneo ya kigoma kwenye ofisi yetu boss wangu alikua kamuoa sekretari wetu ndoa ya kikristo kabisa ila ikatoe anataka kuongeza mke basi walibadili dini wote na huyo bosi akaongeza wife kwa ndoa ya kiislam na walikua wananapendana hao watatu usipime! Hiyo ilikua 80s, wamezaa wamekuza watoto wanne jumla, wawili bi mkubwa na wawili bi mdogo, mwaka 2010 nilienda Bongo kwenye ndoa ya binti yao mkubwa bado wako vile vile na "threesome" lao wanapendana ajabu
 
Inawezekana ,niliwahi kumsikia mwanamke mmoja anamwambia mtu mwingine kuwa ndoa ya mwanamke mmoja ni pasua kichwa akatolea mifano na ndoa za mwanamke mmoja na za mitaala zinavyoendeshwa.
Note;yeye yupo kwenye ndoa ya wake wawili
 
kuna dini zinachochea ndoa kama hizo halafu tunasema wanamwabudu Mungu

Hivi mfalme Daudi alikuwa dini gani vile? sijui lakini alikuwa na wake zaidi ya mmoja...tena aliwahi kuua ili arithi mke wa tatu, na akiwa mzee alioa tena binti kijana aliyesababisha nusura amuue mwanae wa kumzaa kwa kuwa na affair naye! Huyu ni nabii anayeheshimika na dini zote mbili!

Na mfalme Suleiman alikuwa dini gani sijui? lakini najua alikuwa mmoja kati wa watu waliopendwa na mungu, na nabii anayeheshimika na dini zote mbili...huyu alikuwa na wake kwa maelfu!

Na Yakobo sijui dini gani? Huyu baada ya kusota kwa miaka 7 akichunga mifugo mjombaye Labani aliozeshwa Leah badala ya kuozeshwa Raheli aliyempenda..akasota mingine 7 akawa na wake wawili. Mpaka sasa biblia ina vifungu visemavyo 'mimi ndiye mungu wako, mungu wa Isaka na Yakobo.....' ikionyesha jinsi livyokuwa mcha mungu na wakeze wawili..

Need me say more?
 
wapo wanaokubali kuwa nyumba ndogo
kila mtu na kipaji chake
 
Ni ngumu sana hii
Huu ni ubinafsi tu wwanaume na tamaa zao
Cjui kama wanawake wangeamua kuwa na waume wawili kama pangekalika maana huu mkuki umeelekezwa upande mmoja tu.!

Talking as if ni kosa la mwanaume peke yake.

Kwani wewe unayeolewa mke wa pili si una akili pia? Mimi naamini inahitaji akili za kitumwa na udumafu wa mawazo kwenda kushea kiungo cha mwanaume as if wanaume wameisha.

Naonaga kama mchezo wa kuigiza na huu ndio ugumu wa kuwa mwanamke. Hivi kweli umelala unauwaza huku mwenzio anautumia saa hiyo, loh!

Labda niwaulize swali; Unaweza kuukula na mdomo ilhali unajua jana yake ulichomekwa sehemu?
 
Hivi mfalme Daudi alikuwa dini gani vile? sijui lakini alikuwa na wake zaidi ya mmoja...tena aliwahi kuua ili arithi mke wa tatu, na akiwa mzee alioa tena binti kijana aliyesababisha nusura amuue mwanae wa kumzaa kwa kuwa na affair naye! Huyu ni nabii anayeheshimika na dini zote mbili!

Na mfalme Suleiman alikuwa dini gani sijui? lakini najua alikuwa mmoja kati wa watu waliopendwa na mungu, na nabii anayeheshimika na dini zote mbili...huyu alikuwa na wake kwa maelfu!

Na Yakobo sijui dini gani? Huyu baada ya kusota kwa miaka 7 akichunga mifugo mjombaye Labani aliozeshwa Leah badala ya kuozeshwa Raheli aliyempenda..akasota mingine 7 akawa na wake wawili. Mpaka sasa biblia ina vifungu visemavyo 'mimi ndiye mungu wako, mungu wa Isaka na Yakobo.....' ikionyesha jinsi livyokuwa mcha mungu na wakeze wawili..

Need me say more?

Justification ya kuoa wanawake wengi?

Sasa we oa, vijana mtaani watakusaidia kuwaridhisha.

Kwa akili za kuambiwa, ukiulizwa mko wangapi unasema wa5 (yaani wewe na wake zako wa4) unasahau kuwauliza wakati round ipo mashariki, wa kaskazini anakuwa anafarijiwa na nani?
 
hivi mfalme daudi alikuwa dini gani vile? Sijui lakini alikuwa na wake zaidi ya mmoja...tena aliwahi kuua ili arithi mke wa tatu, na akiwa mzee alioa tena binti kijana aliyesababisha nusura amuue mwanae wa kumzaa kwa kuwa na affair naye! Huyu ni nabii anayeheshimika na dini zote mbili!

Na mfalme suleiman alikuwa dini gani sijui? Lakini najua alikuwa mmoja kati wa watu waliopendwa na mungu, na nabii anayeheshimika na dini zote mbili...huyu alikuwa na wake kwa maelfu!

Na yakobo sijui dini gani? Huyu baada ya kusota kwa miaka 7 akichunga mifugo mjombaye labani aliozeshwa leah badala ya kuozeshwa raheli aliyempenda..akasota mingine 7 akawa na wake wawili. Mpaka sasa biblia ina vifungu visemavyo 'mimi ndiye mungu wako, mungu wa isaka na yakobo.....' ikionyesha jinsi livyokuwa mcha mungu na wakeze wawili..

Need me say more?


stooooop. Dont say more
 
Ndoa bwana ni ya mke mmoja na mumu mmoja asikudanganye mtu huyo binti ameyataka mwenyewe maana kaenda kuingilia mapenzi ya wawili ndo akome sikunyingine asikubali matara yanaua
Sikumbuki kama jambo hili lilishajadilia,lakini hata kama tayari lilishajadiliwa nilitaka kujua na nina sababu.Ni kwamba tangu nizaliwe sijawahi kuona ndoa ya uke wenza ina amani baina ya hao wake wawili au wa idadi yoyote.Miezi miwili iliyopita kuna binti aliolewa na mume mwenye mke tayari,lakini leo binti ameachika na amerudi kwao kwa sababu,tangu ameolewa vurugu na mke mkubwa haziishi,bi mdogo kuumwa kila leo,akipelekwa hospital ugonjwa hauonekani,lakini watu wazima wamemwambia kuwa ake mwenzie ndie anamroga!Nae binti kusikia hivyo amefungasha na kuondoka kwa mumewe na anadai talaka.Huo ni mfano mmoja,najua iko mingi,nimekua nikijiuliza sana;hivi kuna mwanamke anakubali kushea mume na mwanamke mwenzie bila kulazimishwa na dini,umaskini,wazazi au mila?Kama hakuna kwanini wanawake waendelee kujitesa na ndoa hizi?Au wapo wanakubali ndoa hizi?Kama wapo ningependa kusikia kutoka kwao . . . . . . !!!!
 
Eee ndugu, hakuna mke anataka ku-share muhogo - that's the fact.
Hata hivyo wapo wanishi pamoja bila ya ugomvi miaka nenda miaka rudi.
 
Sikumbuki kama jambo hili lilishajadilia,lakini hata kama tayari lilishajadiliwa nilitaka kujua na nina sababu.Ni kwamba tangu nizaliwe sijawahi kuona ndoa ya uke wenza ina amani baina ya hao wake wawili au wa idadi yoyote.Miezi miwili iliyopita kuna binti aliolewa na mume mwenye mke tayari,lakini leo binti ameachika na amerudi kwao kwa sababu,tangu ameolewa vurugu na mke mkubwa haziishi,bi mdogo kuumwa kila leo,akipelekwa hospital ugonjwa hauonekani,lakini watu wazima wamemwambia kuwa ake mwenzie ndie anamroga!Nae binti kusikia hivyo amefungasha na kuondoka kwa mumewe na anadai talaka.Huo ni mfano mmoja,najua iko mingi,nimekua nikijiuliza sana;hivi kuna mwanamke anakubali kushea mume na mwanamke mwenzie bila kulazimishwa na dini,umaskini,wazazi au mila?Kama hakuna kwanini wanawake waendelee kujitesa na ndoa hizi?Au wapo wanakubali ndoa hizi?Kama wapo ningependa kusikia kutoka kwao . . . . . . !!!!

Kwa nijuavyo mimi huyo mke mdogo huwa anaambiwa kitu ni uamzi wake kukubali au kukataa, kama yeye ameshindwa akaombe talaka siyo kama wakristo kama mie
 
Back
Top Bottom