Hivi kuna haja ya kuzaa?

Hivi kuna haja ya kuzaa?

Pole sana mdau. Jiulize swali moja tu! kama wazazi wako wangejiuliza kama unavyojiuliza wewe sasa, je wewe ungekuwepo??? Cha msingi ni kuendelea kujaribu na kumuomba muumba kwa imani yako, ipo siku mtpata mtoto.
 
I shake hand with tetere & SONGOKA na kwa kuongezea tu kama mliwai kushiriki kutoa mimba any of you lazima mwombe na kuvunja coz kuna damu inawalilia katika ardhi just in case

pacha nakubakiana na ww
lkn pia usisahau kuwa spiritual husband/wife huwa anasababisha sn hii mambo kutokea.
pia inaweza ikawa kuna vifungo vya asili za kuzaliwa au matamko yaliwekwa huko nyuma na either wazaz o babu na bibi zao then km unavyojua effect ndo hutokea kwa watt au wajukuu.

ol in ol kwa vyovyote vile they need deliverence
 
Last edited by a moderator:
Mimi ni kijana 33 yrs now..katika kuishi kwangu nilibahatika kuoa na sijawahi pata mtoto...miaka minne ya ndoa yetu kuna kipindi.wife alipata ujauzito na ilipofikia siku ya kujifungua mtoto akafariki akiwa tumboni..tukakaa kama miezi saba akapata ujauzito.mwingine ambao ulisumbua sana, miezi minne tu ya ile mimba akaambiwa alazwe bed rest hadi atakapojifungua...tukakubaliana na hali akalazwa hosp for 4 month na ilipofikia miezi nane siku moja ikaonekana mtoto kama anataka kutoka wakamwahisha thearter bahati mbaya ile anafika tu chumba hicho mtoto akafariki...nilipata na simanzi sana nikamshauri wife tukae mwaka na nusu bila kushika ujauzito na sasa tuna mwaka na miezi saba..sasa wife amepatwa na issue ingine tena ya kubleed mfululizo for three month now, tumejaribu kila aina za dawa za hosp, kanisani na mwishowe kuna bibi fulani alitipa dawa ikapungua na sasa namshukuru mungu imekata. Sasa nawaza hivi kuna haja ya kutafuta mtoto kweli ama nipotezee tu niandike walizo kufa wanatosha?

Yahaa, no comment from my side, nimesoma nikalia, i know what you are facing, nimenywea kikombe hiki. i have lost more than 3. KWELI INAUMA.
 
yanayokukuta ni mipango ya mungu. mshukuru kwa kila hali, umtegemee kwa muomba.... in shaa allah utapata!

Hapana huo sio mpango wa Mungu mkuu shetani tu huyo.
Mungu anatupenda.
hivi ushajiuliza mungu huyo huyo aruhusu mimba itungwe amwache mtt akue mpaka afike miezi kadhaa then aamuue? c angemuu b4 au asingeruhusu kabisa ht mimba itungwe?
 
Yahaa, no comment from my side, nimesoma nikalia, i know what you are facing, nimenywea kikombe hiki. i have lost more than 3. KWELI INAUMA.

Pole sana mkuu..hii kitu kama hujawahi pata utadhani ni tamthiria lakini kikombe kikikukuta ndio utajua nini maana ya uchungu..
 
Pole sana mdau. Jiulize swali moja tu! kama wazazi wako wangejiuliza kama unavyojiuliza wewe sasa, je wewe ungekuwepo??? Cha msingi ni kuendelea kujaribu na kumuomba muumba kwa imani yako, ipo siku mtpata mtoto.

Thank you mdau ila kiukweli inauma na inapoteza mood ya kuishi..
 
no brother fanyeni tu checkup vizuri ni tatizo la kiafya usikate tamaa mapema hvyo.
 
Siku hizi bwn watu watakutia moyo tu lakini hawakupi jibu

Yawezekana kwako ukaona kawaida sana na ni sawa tu kwa sababu ya mapenzi yako kwa mkeo,
hutaki apate mateso aliyoyapitia,but nina uhakika kwa mwanamke anaumia sana anapoona wenzie
wamebeba watoto yeye hana,itamgharimu sana mkeo. Ushauri wa muhimu ni kwamba mnapoomba
msimwendee Mungu kama mnavyoenda kwa madaktari na wagagnga,lazima mumwamini kuwa yeye
ni Mungu na Muumba. Na muende kwa madaktari bingwa wa wanawake.Namfahamu daktari mzuri sana
wa Muhimbili na mdada anaitw Dr.Ngalina alishanisaidia sana kwenye ndoa yangu.No.yake 0713406267
 
Duh.. Mkuu pole sana. Ni mojawapo ya challenge kubwa kwa wanandoa.
Kiukweli kuzaa / kutokuzaa sio ishu kubwa kiasi ambacho jamii yetu imekua ikiamini. Watu mnaweza kuishi maisha ya ndoa yenye amani na upendo bila kuwa na watoto especially inapotokea kutaka kuhatarisha maisha ya mmoja wenu.
Tatizo jamii zetu zimejijengea imani kuwa watoto ni kitu cha lazima na usipopata watoto unaonekana kama nini sijui..! Bado tuna yale mambo ya ooh.. ukizeeka nani atakutunza.. mara nani atarithi mali zako.. mara jina lako sijui litaisha.. n.k.. Na hawakawii kuanza kukushauri utafute mke mwingine! Mi nawafahamu watu wengi tu wako kwenye ndoa zaidi ya miaka 15 hawana mtoto wala nini lakini maisha yanaenda. Wengine wana watoto lukuki lakini hawawasaidii chochote zaidi ya kuwatia presha tuu.. Kwa wenzetu nchi zilizoendelea watu huwa wanaoana na wanakubaliana kabisa kuwa hawatazaa na wanaishi hivyo. Kwahiyo mkuu we usiumize kichwa sana. Pia unaweza ku adapt kama utaona unahitaji mtoto wa kuchangamsha nyumba. Pole sana.

mkuu wewe una mtoto? maana hayo mambo unayoongea yalipitwa na wakati kitambo mno, tena ni ya watu wa mashambani!!! Kuna umri mtu unakuwa naham ya MTOTO tu, ndani ya nyumba yenu mnahitaji kampani ya mtoto, mtoto ana raha ndugu yake, ndiyo maana watu wengine wanafikia hatua ya kuasili! BTW, pole sana mkuu Kifulambute , kabla hamjaamua kujaribu bahati yenu jaribu kuonana na madaktari bingwa ili wawape ushauri, kama ni risky basi acheni tu, mnaweza kuchukua hata mtoto wa ndugu yenu atawafariji sana hapo nyumbani, POLENI SANA!
 
Last edited by a moderator:
Hapana huo sio mpango wa Mungu mkuu shetani tu huyo.
Mungu anatupenda.
hivi ushajiuliza mungu huyo huyo aruhusu mimba itungwe amwache mtt akue mpaka afike miezi kadhaa then aamuue? c angemuu b4 au asingeruhusu kabisa ht mimba itungwe?

Kwa hiyo anayeuwa watoto wadogo ni shetani? I thought watoto wadogo wako innocent na hivyo mungu anawalinda, na ni yeye tu mwenye mamlaka ya kuwachukua kwa sababu zake! Haya masuala ya imani ni magumu sana, na mkianza kujadili imani kwa sasa mtamchanganya tu huyu mkuu mwenye shda.
 
huyo mke wako alishatoa mimba waqt wa ujana wake. tafuta nyumba ndogo zaa achana na hilo kopo

Dah aisee punguza strange WORDS!!hata kama alitoa mimba ngapii haihusu,mshauri mwenzio vzur so unamtia tena machungu!unaweza ukawa una point lakin hayo maneno yako unayotumia ni ya shombo!grown up aisee!
 
Mimi ni kijana 33 yrs now..katika kuishi kwangu nilibahatika kuoa na sijawahi pata mtoto...miaka minne ya ndoa yetu kuna kipindi.wife alipata ujauzito na ilipofikia siku ya kujifungua mtoto akafariki akiwa tumboni..tukakaa kama miezi saba akapata ujauzito.mwingine ambao ulisumbua sana, miezi minne tu ya ile mimba akaambiwa alazwe bed rest hadi atakapojifungua...tukakubaliana na hali akalazwa hosp for 4 month na ilipofikia miezi nane siku moja ikaonekana mtoto kama anataka kutoka wakamwahisha thearter bahati mbaya ile anafika tu chumba hicho mtoto akafariki...nilipata na simanzi sana nikamshauri wife tukae mwaka na nusu bila kushika ujauzito na sasa tuna mwaka na miezi saba..sasa wife amepatwa na issue ingine tena ya kubleed mfululizo for three month now, tumejaribu kila aina za dawa za hosp, kanisani na mwishowe kuna bibi fulani alitipa dawa ikapungua na sasa namshukuru mungu imekata. Sasa nawaza hivi kuna haja ya kutafuta mtoto kweli ama nipotezee tu niandike walizo kufa wanatosha?


Pole sana mkuu, pia mtafute Dr. Kapona 065 528 6125, huyu ni dokta mzuri sana wa magonjwa ya kina mama, zamani alikuwa Tumaini Hospitali ila kwa sasa ana hospitali yake kule Buyuni Chanika. Changamoto ni kwamba hospitali yake haijajiunga na hizi Bima za afya hivyo lazima uwe na Cash mkononi.
 
Pole sana mkuu, pia mtafute Dr. Kapona 065 528 6125, huyu ni dokta mzuri sana wa magonjwa ya kina mama, zamani alikuwa Tumaini Hospitali ila kwa sasa ana hospitali yake kule Buyuni Chanika. Changamoto ni kwamba hospitali yake haijajiunga na hizi Bima za afya hivyo lazima uwe na Cash mkononi.

Ahsante mkuu nitamtafuta maana na tena huko ni karibu na ofisi pia.. Cash katika matatizo ndipo inatumika ndugu
 
Kuna prof mmoja wa muhimbili anafanyia kazi maeneo ya upanga ni mzuri kwa tatizo hilo shuka Palm beach kisha uliza kwa prof Kiasi utaelekezwa. Pole sana na usikate tamaa kwani ni wengi wapo kama wewe
 
hayo ndio madhara ya kutumia vidonge na njia zingine za uzazi wa mpango, pole sana, yapo mengi yaliyofichika katika matumiz ya dawa na njia hiz ambayo mawakala wa kifo hutumia lugha lain na nyepesi kuhalalisha uharibifu wa matamizi ya vidonge na njia hizo za uzazi wa mpango, kama mkeo alikua mtumiaji wa visonge hivyo uombe Mungu, mana malengo ya hawa watu ni kuhakikisha wanazuia kazi ya uumba kwa kuua vizazi na utoaji mimba.
 
hayo ndio madhara ya kutumia vidonge na njia zingine za uzazi wa mpango, pole sana, yapo mengi yaliyofichika katika matumiz ya dawa na njia hiz ambayo mawakala wa kifo hutumia lugha lain na nyepesi kuhalalisha uharibifu wa matamizi ya vidonge na njia hizo za uzazi wa mpango, kama mkeo alikua mtumiaji wa visonge hivyo uombe Mungu, mana malengo ya hawa watu ni kuhakikisha wanazuia kazi ya uumba kwa kuua vizazi na utoaji mimba.

Sio wote watumiaji wa hizo dawa
 
Issue Hapa ni Majanga yanayofanywa na akina dada kwenye early years Zao za Ujana!! Sasa ukipata daktari mwelewa anaweza kukupa black and White!! Hayo ni matatizo ya wanawake wengi hasa wasomi (Sorry for this explanation)
 
Back
Top Bottom