Hivi inakuwaje mtu unashabikia CCM?

Hivi inakuwaje mtu unashabikia CCM?

Hivi inakuaje mtu unashabikia Chadema? Yaani ku act uhuni ndo manufaa??? Nishabikie kuchoma infrastructure ambazo kuna uwezekano wa kuja kutumiwa na kizazi changu chote ndo ujanja?

Hivi nyinyi nyumbu huwa mnajiona mna akili sanaaa????
WE CHAWA TUU..
 
Ni zaidi ya ajira mkuu, wengi wana ajira za serikali ila hawafurahishwi na namna nchi inaenda. Kuna kitu cha ziada wanapata zaidi ya hizi TGS scale !!
Wanasema TRUTH is stranger than fiction.

Me nakuambia hata huyo Lucy Mshambwa utakuta halipwi hata mia, hajulikani hata na mwenyekiti wa serikali za mitaa, basi tu mradi na yeye yuko kwenye harakati asikae bure hapa duniani. Yani Niamini.

Anaona tu raha kuanzisha controversies na kukoroga hisia za watu, kuwachezesha watu sebene na wao wanakubali kulicheza. Na Kujizoelea umaarufu uchwara basi.

Huku uraiani wengi wanachopata ni mishahara, per diems, kama wanahusika namna fulani na budget na manunuzi basi wanaongeza wanapiga vya juu basi. Nothing more at all.

Wakijilinganisha na wauza viatu huku ambao ndo wengi kuliko wao huko, wanajiona wamepatia maisha, wana akili sana. Wana bidii sana ya kazi watu wengine ni wavivu, ndo kuja kuwa motivational speaker huku.

Na ni spirit pia, mambo mengine tukikata kuyaelewa kutumia akili za kawaida hatutoelewa kamwe. They're just evil people.

"Mwenye haki huyaangalia madai ya maskini; Bali mtu mbaya hana ufahamu hata ayajue."
Methali.29.7.SUV
 
Idadi kubwa inayoshabikia CCM au serikali inatoka katika haya makundi.

1. Wafanyakazi wa serikali, walimu, madakatari, wanajeshi, polisi, wote waliochini ya payroll ya serikali.

2. Waisilamu wanaongozwa na BAKWATA

3. Vijana waliokimbia shule hasahasa mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Lindi, Pwani, Dodoma.

4. Wafanyabiasha wanaotegemea deal za rushwa serikalini.

5. Wasanii wa bongo fleva na midada ya mjini inayotegemea kudanga kupata chochote kitu.

6. Kundi kubwa la wazee, miaka kuanzia 55 kwenda mbele. Hawa wengi akili zao zilishavurugwa na propaganda za CCM kwa miaka na miaka.
 
Machawa mengi hasa haya mapimbi ya humu yanalipwa buku7 na free wi-fe tu

Piga hesabu kwa mwezi
7000×30=?!
 
Unajua huwa najiuliza na sipati jibu. Hivi inakuwaje mtu unashabikia ccm? Yaani pamoja na mateso yote haya yaliyosababishwa na yanayoendelea kusababishwa na hiki chama inakuwaje kabisa bado unashabikia CCM.

Kipindi cha mfumo wa chama kimoja unaweza kusema labda watanzania hawakuwa na uelewa ndio maana walikuwa wanashabikia ccm, lakini kwa karne hii, pamoja na utandawazi wote huu, information zote hizi bado tu kuna watu wanashabikia ccm. Hivi hawa watu wana shida gani kichwani? Ccm chama ambacho kimeshindwa kuwaletea unafuu wa maisha raia wake kwa kuweka sera nzuri za uchumi unakishabikia kwa lipi? Yaani Tanzania ili utoboe lazima ukwepe mishale mingi. Kufungua tu biashara rasmi unakutana na kodi na tozo lukuki, yaani serikali haipo kabisa kukuwekea sera rafiki za kutoboa. Vijana wengi wanakata mitaji yao simply because kuna vikwazo kibao kusimama kwenye biashara.

Nchi ina rasilimali za asili kibao lakini serikali haina uwezo wa kuzitumia kuwanufaisha wananchi wake. Viongozi wanashindana kuendesha magari ya gharama kubwa ilihali wananchi wanaowaongoza wanatopea kwenye umaskini. Rasilimali za nchi hazitumiki kuwanufaisha wananchi bali zinatumika kuwanufaisha viongozi, halafu bado kuna watu wanaishabikia ccm. Hivi hawa wana akili kweli au ni mazombie?

Barabara huko mawilayani na hata mijini pembeni pembeni hazipitiki kipindi cha mvua, ni mashimo na makorongo mtindo mmoja. Ukiwa na kigari chako huwezi kukiendesha kipindi cha mvua, au ukilazimisha kukiendesha basi gharama za matengenezo zitakuhusu maana si kwa ubovu huu wa barabara. Serikali ya ccm haijui kabisa somo la uchumi, yenyewe inachojua ni kuuza rasilimali za taifa na kununua magari ya kifahali ya viongozi wakati barabara ambazo ndio nyenzo muhimu ya kukuza uchumi wala haziwaumizi kichwa.

October 29, 2025 dunia imekuja kujua kumbe binadamu makatiri bado yapo duniani. Hivi kwa dunia ya leo kweli, yenye ustaarabu wa karne ya 21 ya sayansi na teknolojia unaweza kumuua binadamu kama unawinda wanyama porini. Hivi inawezekanaji dunia ya leo iliyostaarabika na iliyosoma unaua binadamu wenzako kama upo kwenye game reserve unawinda wanyama? Halafu kuproove kuwa hii mishetani kweli ni mishetani inahalalisha mauji kwa vitu vilivyoharibiwa. Hivi kweli kwa dunia ya sasa unaweza kumwambia mtu na akuelewa umeua binadamu mwenzako kwa sababu alikuwa anachoma miundo mbinu na kupora mali? Like seriously? Halafu bado kuna watu wanaishabikia ccm.

Mie nadhani wasomi wetu wa vyuo vikuu au kutoka mataifa mengine waje wafanye research watupe majibu kwa nini kuna watu bado wanaishabikia ccm. Huenda kuna very interesting findings wakaja nazo kuhusu hawa watu wanaoshabikia ccm. Maana hii sio hali ya kawaida, tunaomba utafiti ufanyike tupate majibu kwa nini kuna binadamu bado wanashabikia ccm.
Inakuwa hivyo kwa vile ni mashetani
 
CCM ni maisha yetu yakila siku, CCM ni chama cha kizalendo si chama cha mabeberu
 
Sawa Mkuu sisi wasomi tumekuelewa tutaufanyia kazi ushauri wako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom