Huo udwanzi wa cover watakuwa wameuleta wadwanzi tu.Naona vijana wanaibuka kwa kasi kutengeneza kava badala ya kuutumia mda huo kutengeneza hits zao, huu ni uduanzi, kama kweli nyie ni wasanii si mtengeneze hits zenu? Yaani unakaa unaskilizia staa fulani atoe wimbo ili 'usafirie nyota' yake upitie mgongo wake, dah vijana wa sikuhizi wanapenda dezodezo, hii spidi ya kava naiona kabisa itafikia wakati redioni kava zinakuwa nyingi kuliko nyimbo original. Mi nnavyoelewa kava zilikuwepo tangu enzi hizo, ila zilikuwa zina maana kubwa, hasa ilikuwa ni kwa ajili ya kuwaenzi ma'legend', mfano Brandy na Ray J walivyofanya another day in paradise ya Phil Collins, Jide alivyofanya Muhogo wa Jang'ombe ya Bi Kidude, Mr. Paul alivyofanya Zuwena ya Marijani, n.k, na nnavyoelewa hizi kava zilikuwa zinafanyika baada ya wimbo original kuwa umeshatoka miaka mingi, hiyo ina make sense, but hii ya kutoka baada ya mwezi mmoja hata hainiingii akilini. Halafu cha ajabu media zinasapoti huu ujinga, hapo ndo naamini kwamba media zinachangia kuua mziki. Nyie wasanii na Media acheni huu uduanzi aisee!
mkuu,iyo nyimbo si ishapigwa ban?Dah umenivunja moyo sana aisee kwani ndo nilikuwa namalizia kuandaa cover ya chura.
Unamsema SIWEMA SEPETUAYaani ndo tuseme huna talent kabisa hata ya kuandaa kava? Jaribu hata kava ya Man Fongo, hainanga ushemeji
Njopi hausike kwenye Africa kwenye hiyo kituMkuu pale kwenye IBAARIKIII usinikose aseee
Remix ya wimbo originalMkuu cover katika context ya muziki ndo nini? tusaidiane wengine hatuelewi