Hivi humu ni Home of great thinkers au...?

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
3,314
6,048
Tahadhar: Huu Uzi Una Sauti kubwa mno kama upo very sensitive pita Kulia!

Naona baadhi yetu huenda tumejikuta humu Kwa bahati mbaya Sana,hatuendani na hii platform ambayo imejipambanua kama sehemu yenye watu wenye akili kubwa au maono makubwa Kwa taafsiri isiyo rasmi.

Ukimuona mtu anachangia mada bila kusoma Uzi husika hivi huyu unamuweka kundi gani kama sio Darasa la Tatu B? Hawa ni wapuuzi wakubwa Sana,tena bila aibu anasema kabisa sijasoma huu Uzi au sijasoma wote,sasa kama hujasoma unapata wapi haki ya kuchangia kitu ambacho hukijui? Nyie ndio ambao huwa mnajibu mitihani bila kufuata instruction,Kwa maana nyingine hamjui mnacho fanya.

Yani unachangia mada kutokana na ufahamu wa mtu mwingine na sio wako wewe,je huyo ambaye umeona comment yake Una uwakika gani nae sio Darasa la Tatu B kama wewe? Je Una uwakika nae kaelewa mada au nae hajamaliza kusoma kama wewe? Kama sio upumbavu ni nini?

Humu ndani huwa hatujadili mtu na mara nyingi tunajikuta tunajadili udini,hii ni aibu Sana kwakweli,na hasa ikitokea ima Sheikh au Mchungaji/Padri kafanya makosa kama yeye na sio kama taasisi,lakini tulivyo wapumbavu kama ni Sheikh tutaanza kuutukana Uislamu mwanzo mwisho na kama ni Mchungaji/Padri tutaanza kuutukana Ukristo mwanzo mwisho, kama sio upumbavu ni nini? Kwanini asijadiliwe mtu husika na sio dini yake? Je Uislamu na Ukristo ndio umemtuma huyo mtu kufanya aliyoyafanya?

Kuna wapumbavu wengine ili mada zao zipate wasomaji wengi basi ni lazima Uislamu utukanwe,na kwakuwa watu wengi humu wamelishwa matango Pori kuhusu Uislamu wanajikuta katika upumbavu ule ule wa mtoa mada,ni aibu kwakweli tena Sana,wengine Kwa chuki ambayo imetokana na uelewa mbaya basi huleta hata Maandiko feki ilimradi Tu wazidishe uasi wao dhidi ya Dini ambayo hata haielewi mafundisho yake. Je nikiwaita nyie ni Wapumbavu wakubwa nitakosea?

Na waislamu vile vile tunaingia katika upuuzi huo huo,kwanini uendelee katika mjadala WA kipuuzi,unachoweza kufanya jibu hoja kama kuna ulazima WA kufanya hivyo, lakini ukiona unayejadiliana nae anaendekeza upuuzi cha Busara kwako piga kimya tu. Kuendelea kujadiliana na mtu kama huyo Kwanza ndo mnawafanya wazidi kuleta mada za kipumbavu na vile vile Kitabu chako kinakukataza kufanya mijadala ya kipuuzi.

Matusi yamekuwa sehemu ya jamii forums, kuwa na Utambulisho bandia hakukupi nafasi ya kutukana watu usio wajua,Sana Sana unatupa nafasi ya kujua tunajadiliana na mtu WA namna gani,kauli yako yatosha kujua Tabia zako na maono yako,wajanja watakupuuza mapema Sana, na ambao ni Wapumbavu kama wewe watakusapoti pia.

Unakuta mtu anamtukana mtu Kwa matusi makubwa kabisa akihusisha viungo vya uzazi vya mama yake, Yani hata kutaja hapa naogopa ndio maana nimetumia viungo vya uzazi vya mama yake. Unajiuliza hivi huyu ni mtu wa namna gani,mbona hana ustaarabu,mbona ni mpumbavu namna hii,mpo wengi tu humu. Unafaidika na nini ukitukana,je inakufanya ujisikie vizur? Nikiwaita nyie ni Wapumbavu nakosea?

Kuna nyuzi nyingine sio lazima uchangie,kuna nyingine zipo nje ya uwezo wako na uelewa wako,cha kufanya na ambacho ni cha Busara pita kimya kimya na ujifunze Kwa wachangiaji wengine,nyuzi nyingine huenda haziendani na maadili yako sio vibaya ukapita Kulia utakuwa salama zaidi. Kuliko kutaka kuchangia kila kitu matokeo yake unatuonyesha ulimbukeni wako na upumbavu wako.

Always jitahidi Sana kuchota Busara kutoka Kwa wanajukwaa wengine,hii itakusaidia Sana katika Maisha yako ya kila siku,na Busara ni kuliweka kila Jambo Mahala pake.

Nawapenda Sana!

Ni hayo Tu!
 
Sawa kama wewe umeona hivyo
Ni kweli is the home of great thinker
lakini pia.
is where we dare to talk openly.
Uhuru WA kuongea Kwa mtazamo wangu haimaanishi basi tuongee mambo ambayo ni ya kuzusha na yenye mwelekeo wa kupotosha ukweli husika

Na kumbuka vile vile pia unapoishia Uhuru wako ndipo unapoanzia Uhuru wangu pia.

Tukifanya mambo Kati Kwa Kati naamini tutakuwa salama zaidi.
 
Najua wachangiaji ni wachache kutokana na tabia zilizojengeka kutokana na malezi na mfumo wa maisha lakini haionsoi ukweli kwamba mmomonyoko wa maadili uliokithiri unatokana na muundo wa nchi yetu kutoheshimu watu wengine.

Mfano nakumbuka Makonda alitaka kumpiga Jaji Warioba hakuchukuliwa hatua yoyoyote ya kinidhamu badala yake alitunukiwa cheo mpaka kuwa mkuu wa Mkoa Nape alimtukana matusi machafu Waziri mkuu mstaafu E.Lowassa hakuchukuliwa hatua zozote za kinidhamu badala yake alitunukiwa Uwaziri kama Taifa tunafundisha nini vijana?

Wamesikika kina Lusinde, Kibajaji, wakina mama ao usiseme wanatamka yasiyotamkika na watu wazima asa Bungeni lakini wanasindikizwa kwa makofi hizo tabia zinaonekana ni sawa kama Taifa zimebarikiwa matokeo yake watoto wanakuwa katika hali ya uharibifu nao wanazaa watoto mwaisho tumejikuta tuna kizazi cha ovyo kuliko.

Fuatilia mitandaoni uone vijana wanavyowatukana viongozi wa upinzani matusi mazito hakuna wa kukemea.

Ni mtu mmoja mmoja anatokea kuliona hili kama Taifa tumekwama kabisaaaa sijui tunafanyaje ili kujikwamua na kizazi hichi kibovu.
 
sio la tatu B ni makao makuu lumumba njia ya kwenda mnazi mmoja au makao makuu dodoma chama tawala kilipo
 
Najua wachangiaji ni wachache kutokana na tabia zilizojengeka kutokana na malezi na mfumo wa maisha lakini haionsoi ukweli kwamba mmomonyoko wa maadili uliokithiri unatokana na muundo wa nchi yetu kutoheshimu watu wengine
Mfano nakumbuka Makonda alitaka kumpiga Jaji Warioba hakuchukuliwa hatua yoyoyote ya kinidhamu badala yake alitunukiwa cheo mpaka kuwa mkuu wa Mkoa Nape alimtukana matusi machafu Waziri mkuu mstaafu E.Lowassa hakuchukuliwa hatua zozote za kinidhamu badala yake alitunukiwa Uwaziri kama Taifa tunafundisha nini vijana?
Wamesikika kina Lusinde, Kibajaji, wakina mama ao usiseme wanatamka yasiyotamkika na watu wazima asa Bungeni lakini wanasindikizwa kwa makofi hizo tabia zinaonekana ni sawa kama Taifa zimebarikiwa matokeo yake watoto wanakuwa katika hali ya uharibifu nao wanazaa watoto mwaisho tumejikuta tuna kizazi cha ovyo kuliko. Fuatilia mitandaoni uone vijana wanavyowatukana viongozi wa upinzani matusi mazito hakuna wa kukemea.

Ni mtu mmoja mmoja anatokea kuliona hili kama Taifa tumekwama kabisaaaa sijui tunafanyaje ili kujikwamua na kizazi hichi kibovu.
Asante Sana mkuu Kwa uchambuzi wako mzuri Sana ukihusisha na mifano kadhaa ambayo imeonyeshwa na watu maarufu ambao tunawaona kama kioo cha jamii lakini bahati mbaya kabisa ndio wachafuzi wakubwa.

Ni kweli kabisa Uongozi WA inchi umetuonyesha mfano mbaya Sana WA kuyakaalia kimya mambo kama haya,je wanategemea Sisi kama wananchi tunajifunza nini.

Unajua nakumbuka zamani viongozi wa Ccm walikuwa lazima wapitie katika vyuo vya Uongozi kama Chuo cha Ccm Kivukoni na Lushoto kama sikosei,nayafahamu hayo kwakuwa Baba yangu alikuwa mmoja wapo WA wahadhiri.

Lakini siku hizi wanachaguana Tu matokeo yake ndio hayo
 
Mimi hilo la dini sitaingilia maana ninyi nyote wenye dini huwa mnafanana akili ila nitakuunga mkono hapo kwenye watu kusoma mada either heading tu au kusoma nusu kisha kukimbilia kujibu.

Utakuta mada imekuja,ame-reply ila wewe unamsoma unaona katoka nje ya mstari unajaribu kumsahihisha kwa kumwambia arudi main post asome vizuri ila anaendelea kujibu anachotaka yeye mwisho unakuta post 18 za mwanzo ni za watu walikuwa wanamsahihisha mtu mwishowe thread inakosa ladha.

Inakera sana na wapo wale hawasomi kuelewa ulichoandika wanasoma ili kukujibu hawa ni kama mbuzi hawaelewi jambo nje ya angle wanayoielewa wao ukikutana nao JF utaiona haina maana.
 
Mimi hilo la dini sitaingilia maana ninyi nyote wenye dini huwa mnafanana akili ila nitakuunga mkono hapo kwenye watu kusoma mada either heading tu au kusoma nusu kisha kukimbilia kujibu.

Utakuta mada imekuja,ame-reply ila wewe unamsoma unaona katoka nje ya mstari unajaribu kumsahihisha kwa kumwambia arudi main post asome vizuri ila anaendelea kujibu anachotaka yeye mwisho unakuta post 18 za mwanzo ni za watu walikuwa wanamsahihisha mtu mwishowe thread inakosa ladha.
Asante Sana mkuu Kwa mchango mzuri juu ya wandugu zetu ambao naweza sema huwa wanapenda kukurupuka

Shukrani sana
 
Umekula lakini?halafu tabia ya kuanza kupangia watu ambao huwanunulii hata bando..namna ya kucomment umeianza lini..hivi wavaakobazi mna kili za kushikiwa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Umekula lakini?halafu tabia ya kuanza kupangia watu ambao huwanunulii hata bando..namna ya kucomment umeianza lini..hivi wavaakobazi mna kili za kushikiwa.

#MaendeleoHayanaChama
Sishangai Kwa mtu kama wewe kusema hayo unayosema maana ndio nilio wazungumzia hapa.

Inabidi tuishi nanyi hivyo hivyo Tu!
 
Umeona sasa umewakilisha kundi kubwa la watu kwenye dini yenu.

Wewe mwenyewe kwenye mada yako umekiri kuna mambo watu hatuyaelewi halafu kufafanua hapo umeshindwa.
Mkuu kuna Jambo mtu anakuuliza unajua kabisa huyu anataka ufafanuzi au kujua ukweli hapa.

Mimi sio mgeni na maswali yenu,najua unachotaka hapa ndio maana sitakujibu
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom