Hivi Hii Ya Marando Imekaaje?

Labda wanasheria waliobobea wanaweza kujitokeza kufafanua vizuri zaidi, Lakini kama mteja akikufuata ukataa kumsimamia kesi yake akikushtaki Mahakama kuu, unaweza kuvuliwa hata huo Uwakili, maana Sheria inasema Mtuhumuwa sio mtenda kosa hadi itakapo thibitishwa Mahakamani, na kiapo cha Uwakili ni kuwa utaheshimu hilo na kutunza siri za Wateja wako milele
 
huyo ndie aliyemmaliza mzee wa kiraracha kule tanga kwenye mkutano w NCCR MAGEUZI, usiulize we subiri atakapomaliza kazi CHADEMA, ndo utamjua yukoje.
 
Kwa Marando kumtetea FISADI huku akiwa CHADEMA ni kutaka tu kukiangamiza chama chake. Watu hawamuelewi na hivyo watashindwa kuielewa CHADEMA. CHADEMA wangeachana naye tu huyu mtu kwa usalama na ustawi wa chama.:msela:
 
Ebu naombeni mnieleze ufisadi wa Yusuph Manji kwa sisi tusiyemjua upande wake mwingine yukoje
je anauhusiano na RA + EL ? (Rada,Twin Tower,Richmond/Dowans,Meremeta na Kagoda)
 
Wandugu napenda kueleweshwa Mh. Mabere Marando ni mtu aliye mstari wa mbele katika kupiga vita ufisadi na mafisadi akiwa na joho la CDM. Lakini wakati huo huo anakuwa wakili wa Manji (mtuhumiwa wa ufisadi) ili kupinga kumuhusisha yeye Manji na ufisadi. Je hapa hamna conflict of interests? au sio unafiki kabisa?

ni halali sababu ofisi yake haiingiliani na ujinga wa siasa
 
huyo ndie aliyemmaliza mzee wa kiraracha kule tanga kwenye mkutano w NCCR MAGEUZI, usiulize we subiri atakapomaliza kazi CHADEMA, ndo utamjua yukoje.

Naona umechangia ilimradi hata bila kujua; Mrema alikuwa hovyo hasiye jua ata kusoma hasingewezana na watu wanaotumia akili, hii vita ya Siasa siyo vita mizinga na mabomu ni akili na mikakati ya chama, hili suala ni la kitaalam na lina mipaka yake siyo Siasa, Mahakamani hawafanyi siasa.
 
Kwa Marando kumtetea FISADI huku akiwa CHADEMA ni kutaka tu kukiangamiza chama chake. Watu hawamuelewi na hivyo watashindwa kuielewa CHADEMA. CHADEMA wangeachana naye tu huyu mtu kwa usalama na ustawi wa chama.:msela:

Hueleweki lengo lako nini? au umetumwa na CCM kujenga mgogoro husiokuwepo, Mbona husemi hakimu anayesikiliza ile kesi pia asikubali kusikiliza kesi ya Fisadi!!! Kama hujui jambo ni bora kuuliza badala ya kulalama kama pandikizi la CCM; katika kesi za mahakamani Hakimu, Karani, Muhendesha mashtaka na Wakili ni Sehemu ya Mahakama wote wanasaidiana katika kesi husika ili kumsaidia Hakimu atoe hukumu kwa mujibu wa Sheria.

PILI kesi yenye siyo ya Ufisadi.
 
Mnamuonea bure marando once u stop living in a dreamland u will look at this world a little more clearly..marando tafuta hela mazee achana na wauzastrungi,kisa cha kuua watoto kwa njaa?
 
hata kama daktari ni mwanasiasa ethics zinambana amuudumie mgonjwa ndo maana wanakula viapo! Marando anfanya kazi pale kwa misingi ya jinsi sheria inavyosema kama mwanasheria hata fisadi ana haki ya kutetewa!


Ngoja nikuulize swali dogo tu kaka,kwaiyo ina mmaana hata rostam akija kwa marando kumtaka awe wakili wake marando itabid akubali maana ethics inampasa amatee halaf akitoka hapo atapanda kwenye jukwaa la chadema na kusema rostam ni fisadi?get my point marando hafanyi kosa lolote professionally kumtetea manji ila morally ni kosa kusema unapigana against ufisadi halaf ukawa unamtetea mtu mwenye tuhuma za ufisadi mahakamani,
 
well said Magafu, I do enjoy ur post indeed coz they are always very constructive and meaningful
Baada ya Mungu kuumba mbingu na dunia ..... akamuumba mwanadamu na wote waliozaliwa na mwanadamu huyo wataishi kwa jasho lao. Mungu alitoa Kazi mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya watu. Wahandisi aliwaachia kuendeleza kazi ya uuambaji. Kwa kuumba Wahandisi watakula..... Madaktari wakaachiwa kazi ya kuhakikisha wanyama na wanadamu wanaendelea kuwa na afya njema. ......Kwa udhaifu wa miili yetu madaktari wanakula. ........orodha ni ndefu lakini cha msingi ni kuwa Kwa dhambi za watu Askofu Kakobe, Mzee wa Upako, Sheikh Simba na wengine wote walioitwa kwa jina la Mungu wao wanakula fedha za madhabahuni. Kwa ugomvi na faraka za watu Wanasheria kama Mabere Marando na wenzake wanakula fedha za watu kupitia mlango wa mahakamani. Je, kunatatizo gani? Manji na Mengi wasingefarakana Mabere Marando na wanasheria wenzake wote wasingekuwa na kazi......

Jamani acheni ale kwa kadri Mungu alivyomwamuru na kwa kadri aonavyo tatizo ni pale kweli Manji akiwa ni fisadi na yeye kumtetea kwenye majukwaa ya siasa.
 
Labda wanasheria waliobobea wanaweza kujitokeza kufafanua vizuri zaidi, Lakini kama mteja akikufuata ukataa kumsimamia kesi yake akikushtaki Mahakama kuu, unaweza kuvuliwa hata huo Uwakili, maana Sheria inasema Mtuhumuwa sio mtenda kosa hadi itakapo thibitishwa Mahakamani, na kiapo cha Uwakili ni kuwa utaheshimu hilo na kutunza siri za Wateja wako milele
Wanasheria wana haki ya kudecline client au kuaccept, ukitaka kujua nenda kwa mkono ambaye hachukui croiminal cases only with exceptions kama za ditopile....swali langu kama jamaa akiona profession ni muhimu kuliko wananchi then inabidi Aache siasa kwani leo manji kesho rostam atabisha hodi kumwambia nyaucho marando amsimamie kesi sijui hapo wadau watasemaje au bado itakuwa profession
 
Wanasheria wana haki ya kudecline client au kuaccept, ukitaka kujua nenda kwa mkono ambaye hachukui croiminal cases only with exceptions kama za ditopile....swali langu kama jamaa akiona profession ni muhimu kuliko wananchi then inabidi Aache siasa kwani leo manji kesho rostam atabisha hodi kumwambia nyaucho marando amsimamie kesi sijui hapo wadau watasemaje au bado itakuwa profession

Una hasira tu! jaribu kutuliza hasira zisizidi uwezo wa akili;hivyo vitu havina uhusiano hata kidogo, labda kama tupo vitani sawa lakini siasa la hasha!!! unataka kusema ukiingia Billizs randomly hutapata mwanachama wa CCM??? au una maana gani?? au una maanisha Mpira ukichezwa CCM Kirumba kama wewe CDM huingii??!! ebu fafanua manaa nyie CCM upeo wenu sufuri sana; sijakuelewa? yaani ukiwa Dom huingii Clab 84!!! mhmm kama ni hivyo mabasi yote ya mikoani hupandi.
 
<p>
Wandugu napenda kueleweshwa Mh. Mabere Marando ni mtu aliye mstari wa mbele katika kupiga vita ufisadi na mafisadi akiwa na joho la CDM. Lakini wakati huo huo anakuwa wakili wa Manji (mtuhumiwa wa ufisadi) ili kupinga kumuhusisha yeye Manji na ufisadi. Je hapa hamna conflict of interests? au sio unafiki kabisa?
</p>
<p>&nbsp;</p>Kwa nini hukuwahi hoji utetezi wa Bob Makani(m'kiti mstaafu wa CDM) kwa balozi Prof Mahalu ktk kesi ya ufisadi kule Italy?mnajifanya kuhoji leo hii baada ya upepo wa siasa kuwakalia vubaya. ccm na cuf acheni kuhoji vitu ambavyo mnavifahamu...siasa itenganishwe na profesheni. Ni sawa na kusema kuwa mwanafunzi anayefanya degree ya animal science & production pale SUA basi asihudhulie lectures concerning 'PIGS' kwasababu ni muislam?
 
kwani mengi sio fisadi??mengi ana personal vendetta na wafanyabiashara wenzake lakini na yeye ni fisadi tu...after all a person is innocent until proven guilty,.that is a general rule,..exception ni RA

Hiyo vendetta si tungeambiwa basi badala ya kuificha? Mimi nafikiri mengi ni wa kupongezwa kwa kupaza sauti yake na kutamka yale ambayo wengi wetu tunaishia kunung'unikia kwenye mito ya vitanda. Hili la Marando, pamoja na kwamba yuko kazini lakini kuna suala la utashi binafsi na hasa unapokuwa ni mwanasiasa wa majukwaani na huku ukihubiri maovu ya ufisadi!
 
That is serious business man nothing personal there. Yuko kikazi zaidi mkuu
 
]Mabere Nyaucho Marando ni wakili wa Mengi[/SIZE].Huyo Marando ambaye ni wakili wa Manji ni yupi?Au kesi hii ina mawakili waliofanana majina pande zote mbili?

Ilikuwa nichangie thread hii, lakini baada ya kukumbana na watu waliokurupuka usingizini kama huyu,naona ngoja nitafute thread nyingine hapa napoteza muda wangu tu. sasa mtu hata hajui kama Marando ni wakili wa Manji hapa tutajadiliana nini? napita wakuu tukutane kwenye thread nyingine.
 
Marando ni wakili.
Nini kazi ya wakili?
Wakili kazi yake ni kuhakikisha kuwa mteja wake anatendewa haki mahakamani (sio tu kumtetea).
Kama Mteja wa wakili amefanya kosa na ana hatia basi apewe adhabu kulingana na kosa alilofanya na adhabu iliyowekwa kwa mujibu wa sheria, asionewe.
Marando anaposimamia Manji ali ahukumiwe(kama ana hatia) kwa mujibu wa sheria bila kuonewa, kwa upande wangu mimi sioni kosa lake.
unakazania wakili, wakili! lakini unafumbia macho uwanasiasa wake na jukumu lake la kutetea wanyonge, hebu fikiria nje ya box, RA amekuwa akitajwa sana kwenye issue ya DOWANS akijitokeza kufungua kesi dhidi ya wanaomtajataja ( wengi wao CDM ) harafu Tundu Lisu aende kumtetea kama mwanasheria kwako wewe iko sawa?
 
Back
Top Bottom