Wandugu napenda kueleweshwa Mh. Mabere Marando ni mtu aliye mstari wa mbele katika kupiga vita ufisadi na mafisadi akiwa na joho la CDM. Lakini wakati huo huo anakuwa wakili wa Manji (mtuhumiwa wa ufisadi) ili kupinga kumuhusisha yeye Manji na ufisadi. Je hapa hamna conflict of interests? au sio unafiki kabisa?
huyo ndie aliyemmaliza mzee wa kiraracha kule tanga kwenye mkutano w NCCR MAGEUZI, usiulize we subiri atakapomaliza kazi CHADEMA, ndo utamjua yukoje.
Kwa Marando kumtetea FISADI huku akiwa CHADEMA ni kutaka tu kukiangamiza chama chake. Watu hawamuelewi na hivyo watashindwa kuielewa CHADEMA. CHADEMA wangeachana naye tu huyu mtu kwa usalama na ustawi wa chama.:msela:
hata kama daktari ni mwanasiasa ethics zinambana amuudumie mgonjwa ndo maana wanakula viapo! Marando anfanya kazi pale kwa misingi ya jinsi sheria inavyosema kama mwanasheria hata fisadi ana haki ya kutetewa!
Baada ya Mungu kuumba mbingu na dunia ..... akamuumba mwanadamu na wote waliozaliwa na mwanadamu huyo wataishi kwa jasho lao. Mungu alitoa Kazi mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya watu. Wahandisi aliwaachia kuendeleza kazi ya uuambaji. Kwa kuumba Wahandisi watakula..... Madaktari wakaachiwa kazi ya kuhakikisha wanyama na wanadamu wanaendelea kuwa na afya njema. ......Kwa udhaifu wa miili yetu madaktari wanakula. ........orodha ni ndefu lakini cha msingi ni kuwa Kwa dhambi za watu Askofu Kakobe, Mzee wa Upako, Sheikh Simba na wengine wote walioitwa kwa jina la Mungu wao wanakula fedha za madhabahuni. Kwa ugomvi na faraka za watu Wanasheria kama Mabere Marando na wenzake wanakula fedha za watu kupitia mlango wa mahakamani. Je, kunatatizo gani? Manji na Mengi wasingefarakana Mabere Marando na wanasheria wenzake wote wasingekuwa na kazi......
Jamani acheni ale kwa kadri Mungu alivyomwamuru na kwa kadri aonavyo tatizo ni pale kweli Manji akiwa ni fisadi na yeye kumtetea kwenye majukwaa ya siasa.
Wanasheria wana haki ya kudecline client au kuaccept, ukitaka kujua nenda kwa mkono ambaye hachukui croiminal cases only with exceptions kama za ditopile....swali langu kama jamaa akiona profession ni muhimu kuliko wananchi then inabidi Aache siasa kwani leo manji kesho rostam atabisha hodi kumwambia nyaucho marando amsimamie kesi sijui hapo wadau watasemaje au bado itakuwa professionLabda wanasheria waliobobea wanaweza kujitokeza kufafanua vizuri zaidi, Lakini kama mteja akikufuata ukataa kumsimamia kesi yake akikushtaki Mahakama kuu, unaweza kuvuliwa hata huo Uwakili, maana Sheria inasema Mtuhumuwa sio mtenda kosa hadi itakapo thibitishwa Mahakamani, na kiapo cha Uwakili ni kuwa utaheshimu hilo na kutunza siri za Wateja wako milele
Wanasheria wana haki ya kudecline client au kuaccept, ukitaka kujua nenda kwa mkono ambaye hachukui croiminal cases only with exceptions kama za ditopile....swali langu kama jamaa akiona profession ni muhimu kuliko wananchi then inabidi Aache siasa kwani leo manji kesho rostam atabisha hodi kumwambia nyaucho marando amsimamie kesi sijui hapo wadau watasemaje au bado itakuwa profession
</p>Wandugu napenda kueleweshwa Mh. Mabere Marando ni mtu aliye mstari wa mbele katika kupiga vita ufisadi na mafisadi akiwa na joho la CDM. Lakini wakati huo huo anakuwa wakili wa Manji (mtuhumiwa wa ufisadi) ili kupinga kumuhusisha yeye Manji na ufisadi. Je hapa hamna conflict of interests? au sio unafiki kabisa?
kwani mengi sio fisadi??mengi ana personal vendetta na wafanyabiashara wenzake lakini na yeye ni fisadi tu...after all a person is innocent until proven guilty,.that is a general rule,..exception ni RA
]Mabere Nyaucho Marando ni wakili wa Mengi[/SIZE].Huyo Marando ambaye ni wakili wa Manji ni yupi?Au kesi hii ina mawakili waliofanana majina pande zote mbili?
unakazania wakili, wakili! lakini unafumbia macho uwanasiasa wake na jukumu lake la kutetea wanyonge, hebu fikiria nje ya box, RA amekuwa akitajwa sana kwenye issue ya DOWANS akijitokeza kufungua kesi dhidi ya wanaomtajataja ( wengi wao CDM ) harafu Tundu Lisu aende kumtetea kama mwanasheria kwako wewe iko sawa?Marando ni wakili.
Nini kazi ya wakili?
Wakili kazi yake ni kuhakikisha kuwa mteja wake anatendewa haki mahakamani (sio tu kumtetea).
Kama Mteja wa wakili amefanya kosa na ana hatia basi apewe adhabu kulingana na kosa alilofanya na adhabu iliyowekwa kwa mujibu wa sheria, asionewe.
Marando anaposimamia Manji ali ahukumiwe(kama ana hatia) kwa mujibu wa sheria bila kuonewa, kwa upande wangu mimi sioni kosa lake.