Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Kwenye Biblia,Mw 2:18 imeandikwa;"BWANA Mungu akasema,Si vema huyo mtu awe peke yake,nitamfanyia msaidizi wa kufanana nae".Ndipo akamletea wanyama kibao lakini hakuonekana wa kufanana nae,Mw 2:19-20,ndipo Mungu alipomuumba mwanamke kutoka ubavuni mwa Adam. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Hapa nimegundua kuwa,Mwanaume alianza kuhitaji msaidizi wa kawaida lakini ngono sio sababu ya kuumbwa mwanamke.Pili,mwanaume alihitaji kusaidiwa,hii maana yake ni kwamba,Mwanaume kamwe hawezi kutimiza majukumu yake bila mwanamke.Tatu,mwamke aliumbwa kwaajili ya mwanaume,lakini mwanaume hakuumbwa kwaajili ya mwanamke.Nne,kazi iliyomleta au kusababisha mwanamke kuumbwa ni kumsaidia mwanaume tu.Tano,malengo ya uumbaji wa Mungu hayakumhusisha mwanamke,yaani mwanamke yupo duniani si kwaajili ya kutimiza malengo ya uumbaji wa Mungu bali kumsaidia mwanaume kuyatimiza malengo ya Mungu. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Jamani msinirushie mawe,kama Mungu hakumaanisha hivyo leta tafsiri yako,unless uwe huiamini Biblia.Hebu tujadiliane inawezekana nimepotoka!