Hivi faida ya "show off" ni nini?

No Escape2

JF-Expert Member
Jul 4, 2020
228
322
Kujionesha kwamba una nyumba kubwa!

Kujionesha kwamba una ujauzito (Tumbo kubwa!)

Kujionesha kwamba na wewe unaitwa baba mtandaoni.

Kujionesha kwamba una gari kali.

Kujionesha kwamba wewe una Shamba kubwa! Tupia picha za mahindi yako, matikikiti yamejaa shambani huku umenyoosha mikono na mengineyo yanayofanywa huko mitandaoni.

Cha ajabu kuna watu wanafanya makubwa zaidi ya hayo lakini wapo kimya.

Timiza malengo yako kimyakimya utatoboa. Achana na kiki!
 
Mbona swali na jibu tofauti? Kama kuna faida na sisi tuanze. Namaanisha labda faida ya kimaendeleo yaani kiuchumi hivi au vyovyote au mnataka mtajirike peke yenu!
 
Hayo ndiyo mambo ya Vijana wa Miaka ya 82' wanakera sana kwa Show off za kike haswaaa. Na ilishajadiliwa humu ndani kuwa Mwanaume mzima na akili zako kupigapiga picha unaonyesha sura yako mwishowe utaishia kuombwa marinda ebboo.
 
Hivi kabla ya social medias hizi show offs zilikua zinafanyikaje? Tusiopost chochote huko watsapp status tunaonekana kama wanama/washamba flani.
 
Back
Top Bottom