Hivi Dodoma ndio hakuna maji namna hii?

Yesu Anakuja

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
9,446
19,227
Nimekaa hapa wiki moja nzima, mabomba hayatoi maji.

Nadhani serikali imeharakisha kuhamishia makao makuu hapa Dodoma kabla suala la maji halijatengemaa.

Awesu ndo yupo Italy anakula bata tu.

====

UFAFANUZI KUTOKA DUWASA

====

Mdau pole kwa changamoto hiyo

Mimi ni Mkurugenzi wa Usambazaji maji na Usafi wa Mazingira hapa DUWASA.
Kwanza ningependa kufahamu eneo uliloishi kwa muda huo wote ukakosa maji, pili nielewe kwa kifupi kuhusu hali ya maji jijini Dodoma.

Pamoja na kuhudumia Dodoma Mjini, DUWASA pia inahudumia miji ya Chamwino, Kongwa, Bahi na hivi karibuni tumeongezewa kibaigwa.

Ukiongelea Dodoma mjini, utakumbuka kuwa kati ya mwaka 2017/18 yalifanyika mabadiliko ya Serikali kuhamia Dodoma ambapo immediately kama taasisi tulitarajia ongezeko kubwa la mahitaji ya maji. Wakati huo tulikuwa tumekamilisha mradi wa maji hapa mjini ambao uliongeza uwezo wa uzalishaji na usambazaji maji kutoka lita 30 milioni hadi kufikia lita 61.5 milioni kwa siku. Mradi huu ulikamilika 2015, na miradi ya maji husanifiwa kwa kipindi cha kati ya miaka 20 mpaka 30.

Kutokana na hali hii ya ongezeko la mahitaji ukilinganisha na uwezo uliopo, hatua kadhaa zimechukuliwa na zinatekelezwa na DUWASA chini ya Wizara ya maji kutatua changamoto hii.

Mahitaji kwa sasa ni lita 133 milioni kwa siku wakati uwezo ni wastani wa lita 68 milioni kwa siku. Hii inatulazimu kutoa maji kwa mgao. Ndiyo maana nimeuliza eneo uliopo ili kujua nini kilitokea.

Tunaendelea na utatuzi wa changamoto hii katika hatua za Muda Mfupi (uchimbaji wa visima pembezoni Mfano Nzuguni), Muda wa kati (Ujenzi wa bwawa pa Farkwa), Muda Mrefu ( Kutoa maji ziwa Victoria)na Mpango wa Dharula (kutoa maji bwawa la mtera)

Yote hii ni kuhakikisha Dodoma inakuwa na huduma toshelevu ya majisafi.
 
Nimekaa hapa wiki moja nzima, mabomba hayatoi maji.

Nadhani serikali imeharakisha kuhamishia makao makuu hapa Dodoma kabla suala la maji halijatengemaa.

Awesu ndo yupo Italy anakula bata tu.
Hivi kule Dubai walitoa wapi maji, mbona palikuwa jangwa zaidi ya hata hapo Dodoma?

Anyway, labda fund capital ni tatizo kulingana na nchi zetu za dunia ya 3.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Hivi kule Dubai walitoa wapi maji, mbona palikuwa jangwa zaidi ya hata hapo Dodoma?

Anyway, labda fund capital ni tatizo kulingana na nchi zetu za dunia ya 3.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
There are two sources for water in the UAE: Ground water and desalinated sea water. The ground water levels are not enough and only serves a little more than 1% of its need. Close to 99% of potable drinking water in Dubai now comes from its desalination plants.
 
There are two sources for water in the UAE: Ground water and desalinated sea water. The ground water levels are not enough and only serves a little more than 1% of its need. Close to 99% of potable drinking water in Dubai now comes from its desalination plants.
Tatizo kubwa hasa nadhani ni financal capital.

2020 China ilijenga kiwanja cha ndege cha kimataifa kikubwa sana duniani juu ya bahari chenye square kilometers sawa na Jiji la Dar lote.

Huoni jinsi gani pesa imetumika hapo?

2018 Niliangalia chaneli ya Discovery Science Startimes, walikuwa wanadai China ilikuwa na project ya kujenga reli ya umeme chini kwa chini ardhini kwa miaka 20 ambapo ingerahisisha kusafiri kwa treni ya kisasa toka China hadi USA kwa masaa mawili tu.

Changamoto ni Earth's axis (muhimili wa dunia unapojizungushia) pana jotoridi kali sana hata waweke AC ya kiwango gani bado hakuna kiumbe kitachosalia ikiwa treni itakatiza kwenye huo muhimili wa dunia.

Pesa ina nafasi kubwa sana kujenga vitu ambapo hapana hata vigezo/sifa sahihi.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Nimekaa hapa wiki moja nzima, mabomba hayatoi maji.

Nadhani serikali imeharakisha kuhamishia makao makuu hapa Dodoma kabla suala la maji halijatengemaa.

Awesu ndo yupo Italy anakula bata tu.
Kichekesho hayo maji yenyewe yakitoka baada ya hiyo wiki moja, bado unakuta ni maji chumvi!!

Aisee huo mji unahitaji uwekezaji wa kutosha sana mpaka kuwa na hadhi ya kuitwa Jiji!
 
Afadhali maji yasitoke Dodoma ili mawaziri wadogo wasichukue wanafunzi Udom.
 
Ikulu yapo ya kutosha tu mpaka wameamua kufuga mabata na viboko viwe vinajivinjari humo majini
 
Back
Top Bottom