Hivi 'chopa' ya CHADEMA inatumika Arusha na Moshi pekee?

Hivi 'chopa' ya CHADEMA inatumika Arusha na Moshi pekee?

WanaJF!<br />
<br />
Ni imani yangu tuna tambua kuwa Tanzania yetu ni moja na watanzania wote ni wamoja katika mambo yote yanayohusu taifa letu, ikiwemo mambo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa, na wote kama watanzania tuna stahiki kupata mambo haya kwa usawa.<br />
<br />
Katika hali kama hiyo ya kupata hayo mambo kwa usawa, nasikitika kusema kuna kundi fulani la watu aidha hawapo tayari kutoa usawa huo ama hawajui kuwa ndio tamaduni na desturi yetu watanzania kushiriki kwa usawa kwenye mambo tajwa hapo juu.<br />
<br />
Katika kulisisitiza hili, ningependa tutizame siasa za CHADEMA, hivi karibuni umefanyika uchaguzi wa madiwani kwenye zile kata ambazo madiwani wake aidha walitimuliwa ama walifariki hivyo kata kubaki wazi, katika chaguzi zile CHADEMA walifanya ubaguzi mkubwa mno.<br />
<br />
Kata zilizo kuwana uchaguzi zilikuwa maeneo mbalimbali ya nchi, ikiwemo Mbeya, Morogoro, Mara na Manyara, lakini 'CHOPA' ya CHADEMA ilipaa Arusha tu na wala haikuchungulia sehemu nyingine yoyote hapa nchini.<br />
<br />
Aidha, huko Arusha 'CHOPA' ya CHADEMA ilikuwa busy kwenye kata zote, yani haikuwahi kutokea kampeni zifanywe bila matumizi ya 'CHOPA' hiyo kwa kipindi chote cha uchaguzi wa kata za pale Arusha.<br />
<br />
Kama hiyo haitoshi, hivi sasa kamanda wa anga, bwana Mbowe, yupo Hai kama mbunge wa jimbo hilo, lakini kwa ubabe wake amehamua atumie 'CHOPA' hiyo kufanya shughuli zake zote, yani kama mbunge na pia mwenyekiti wa chama.<br />
<br />
Kwa kufanywa hivyo inakuwa sio sawa, kama itakuwa hivyo basi na majimbo mengine nayo yapelekewa 'CHOPA' ya CHADEMA na isibaki Arusha na Moshi pekee, kwani ikiendelea hivyo itatafsiriwa kuwa CHADEMA ni chama cha ukanda.
Jamaa: Hello mrembo, samahani, una mpenzi?
Binti: Hapana. Sina mpenzi.
Jamaa: Kitabu cha Mwanzo 2: 18 "Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye."

Binti: Lakini mimi sikupendi jamani.
Jamaa: Waraka wa kwanza wa Yohana 4:8 "Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo."

Binti: Mh! Mi ntajuaje kwamba na wewe unamaanisha hayo maneno?
Jamaa: Injili ya Mathayo 12:34b "Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake."

Binti: Jamani leo kazi. Mi ntajuaje kwamba we ni mkweli na mwaminifu?
Jamaa: Injili ya Marko 13:31 "Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe."

Binti: Wewe! Na kwanini umekuja kwangu? Wasichana mbona wako wengi tu!
Jamaa: Mithali 31:29 "Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote."

Binti: We una mambo wewe! Sasa mimi kwangu umependa kitu gani?
Jamaa: Wimbo Ulio Bora 4:7 "Mpenzi wangu, u mzuri pia pia, Wala ndani yako hamna ila."

Binti: Mh! Huo uongo, mbona mimi hata sio mzuri kihivyo. Unaongeza chumvi tu!
Jamaa: Mithali 31:30 "Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa."

Binti: Nikisema nimekukubalia itakuaje?
Jamaa: Mwanzo 2:24 " Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja."

Binti: Jamani we mkaka. Inakuaje unajua maandiko kiasi hicho?
Jamaa: Yoshua 1:8 "Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana."

Binti: Wowwww! Naona unampenda sana Mungu.
Jamaa: Zaburi 34:8 "Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini."

Binti: Mh! Haya bwana. Basi nipe muda nifikirie ombi lako.
Jamaa: Wafilipi 4:8 "Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo."

Binti: Mh! Jamani wewe, haya, nimekubali. Mpaka hapo nakupenda tayari!!
Jamaa: Ufunuo wa Yohana 22:21b "Amina"
 
Kweli wewe BAVICHA, mada inajieleza kuwa ni jinsi gani CHADEMA inafanya siasa za ukanda, nimeweka CHOPA kama kithibitisho cha hoja yangu, ila wewe BAVICHA bado unauliza eti CHOPA ya CHADEMA inanihusu nini?

Halafu, hivi hujui mafuta na matengenezo ya CHOPA hiyo yanatokana na pesa ya ruzuku ambayo ni karibu 90% ya matumizi yote yanayo fanywa na CHADEMA?

ruzuku siyo fadhila bali ni haki ya kila chama kikatiba hau wewe unataka kutuaminisha sisi wenye akili zetu timamu kama ninyi mnavyo waaminisha watanzania ccm imejenga mabarabara na kuwaaminisha kama mmewasaidia,bila wao kujua ni haki ya serikali yoyote kikatiba,kujenga mabarabara afya elimu, na ni haki yao kwa sababu wao wanalipa kodi,
 
Na pia Mbowe anazidi kuwa tajiri kila kukicha. Sijui anafanya biashara gani zaidi ya zile alizokuwa anafanya kabla ya kuwa mwenyekiti wa Chadema. Isije ikawa michango inayopitishwa kwenye mikutano ya Chadema kwa lugha ya changia Chadema ndiyo inampa huo utajiri.
 
ruzuku siyo fadhila bali ni haki ya kila chama kikatiba hau wewe unataka kutuaminisha sisi wenye akili zetu timamu kama ninyi mnavyo waaminisha watanzania ccm imejenga mabarabara na kuwaaminisha kama mmewasaidia,bila wao kujua ni haki ya serikali yoyote kikatiba,kujenga mabarabara afya elimu, na ni haki yao kwa sababu wao wanalipa kodi,

Kama wewe unaweza kupandisha sauti na kuhoji serikali kuwa kwanini inafanya hivi?, kwanini inafanya vile? n.k kwa kuwa tu unalipa kodi, basi kodi hiyo hiyo ambayo mimi, wewe na yule tunailipa ndio hiyo hiyo inafanya CHADEMA waweze kurusha CHOPA yao angani, sasa kwanini unizuie mimi kuhoji juu ya matumizi ya CHOPA ya CHADEMA?

Angalizo: hakuna asiyejua kuwa ni haki ya CHADEMA kupewa ruzuku, hoja ni je, ruzuku inatumika kwa usawa?
 
Na pia Mbowe anazidi kuwa tajiri kila kukicha. Sijui anafanya biashara gani zaidi ya zile alizokuwa anafanya kabla ya kuwa mwenyekiti wa Chadema. Isije ikawa michango inayopitishwa kwenye mikutano ya Chadema kwa lugha ya changia Chadema ndiyo inampa huo utajiri.

nafikiri hui fahamu vizuri familia ya mzee freeman,uliza kwa walio kua wanamjua mzee freeman hata nyerere alimjua vizuri na uwezo alio kuwa nao,,ni hivi kwa kina mbowe hamna njaaa,,fahamu hilo tena hela halali sio za unga wala za rada na za kusafirisha twiga,
 
ha ha ha ha ha! nildhani chopa ni maj ya bomba ndio maana akalalamika hivo.... ha ha ha ha ha !
 
Usikimbie mada, mada haiongelei uchaguzi mkuu, kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2011 CHADEMA imekuwa ikifanya siasa na 'CHOPA' hapo Arusha tu, kama unabisha, ni kwanini kwenye uchaguzi wa madiwani chopa haikuvuka mipaka ya Arusha?

Dada yangu Hamida najua wewe sio mjinga, najua kwamba una akili sana ila tatizo ulilonalo ni lile lile walilonalo vijana wengi kama sio wote wa green guards la kujitoa ufahamu. Ile kata iliyopo mheza ni arusha? Kule mbeya ni arusha? Mbulu? Hanang? Kilosa? Kote huko chopa ilitua wakati wa kampeni za chaguzi ndogo za udiwani, lakini dada yangu Hamida umeona ile ya arusha pekee, Kweli nimeamini ukiwa kwenye hicho chama cha Mateja (ccm) hata kama ni prof. uwezo wako wa kupambanua mambo unazidiwa na mtoto wa darasa la nne la mkoloni.
 
ha ha ha ha ha! nildhani chopa ni maj ya bomba au umeme ndio maana akalalamika hivo.... ha ha ha ha ha !
 
Kama wewe unaweza kupandisha sauti na kuhoji serikali kuwa kwanini inafanya hivi?, kwanini inafanya vile? n.k kwa kuwa tu unalipa kodi, basi kodi hiyo hiyo ambayo mimi, wewe na yule tunailipa ndio hiyo hiyo inafanya CHADEMA waweze kurusha CHOPA yao angani, sasa kwanini unizuie mimi kuhoji juu ya matumizi ya CHOPA ya CHADEMA?

Angalizo: hakuna asiyejua kuwa ni haki ya CHADEMA kupewa ruzuku, hoja ni je, ruzuku inatumika kwa usawa?

ruzuku; yenu inatumikaje?
 
nafikiri hui fahamu vizuri familia ya mzee freeman,uliza kwa walio kua wanamjua mzee freeman hata nyerere alimjua vizuri na uwezo alio kuwa nao,,ni hivi kwa kina mbowe hamna njaaa,,fahamu hilo tena hela halali sio za unga wala za rada na za kusafirisha twiga,

Kwanza, hakuna mtu anayeitwa mzee Freeman kwa upande wa Mbowe.

Pili, kaka yake Freeman Mbowe unamfahamu?, unajua ana uwezo gani kipesa?, kwa ufupi ni kwamba ana uwezo wa middle income na sio kama Freeman Mbowe ambae ni tajiri.

Tatu, kama wewe unajua zaidi kuhusu vyanzo vya mapato vya bwana Mbowe, kwanini usiviorodheshe badala tu ya kutetea kwa maneno mepesi bila ya uthibitisho?

Tueleze mzee Aikael Mbowe alipata wapi pepa ya kumiliki kiwanja katika ya jiji (Posta) na kujenga kumbi ya starehe ilikuwa ikijulikana kama Mbowe na sasa (bilicanas), amepata wapi pesa ya kumiliki ardhi kubwa Arusha na Moshi na kuweza kujenga mahoteli kule?
 
Dada yangu Hamida najua wewe sio mjinga, najua kwamba una akili sana ila tatizo ulilonalo ni lile lile walilonalo vijana wengi kama sio wote wa green guards la kujitoa ufahamu. Ile kata iliyopo mheza ni arusha? Kule mbeya ni arusha? Mbulu? Hanang? Kilosa? Kote huko chopa ilitua wakati wa kampeni za chaguzi ndogo za udiwani, lakini dada yangu Hamida umeona ile ya arusha pekee, Kweli nimeamini ukiwa kwenye hicho chama cha Mateja (ccm) hata kama ni prof. uwezo wako wa kupambanua mambo unazidiwa na mtoto wa darasa la nne la mkoloni.

haaaaaaa [saronga] umenichekesha sana, pale ccm kuna kaugonjwa cha ,:mimba:,kuvimbiwa madaraka siunamkumbuka pro tibaijuka alivyokua jembe kabla hajaja ccm? vp bwana omari nundu? wote kwishi nhehi, kwenye chama cha kufungwa,,:tape:,,nakumalizwa,:A S-confused1:,,naku,,:behindsofa:,,,,kitaaluma, hupo hapo bwana [saronga]?
 
Ile ni ya nyumbani kweni wengine inawahusu nini ile ya sisi kwa sisi tena mkome kuiulizia nyie wengine mnaoiulizia mnamchango gani kwa chadema.

mwenyu wewe...chadema hatupo hivyo.
 
Kwanza, hakuna mtu anayeitwa mzee Freeman kwa upande wa Mbowe.

Pili, kaka yake Freeman Mbowe unamfahamu?, unajua ana uwezo gani kipesa?, kwa ufupi ni kwamba ana uwezo wa middle income na sio kama Freeman Mbowe ambae ni tajiri.

Tatu, kama wewe unajua zaidi kuhusu vyanzo vya mapato vya bwana Mbowe, kwanini usiviorodheshe badala tu ya kutetea kwa maneno mepesi bila ya uthibitisho?

Tueleze mzee Aikael Mbowe alipata wapi pepa ya kumiliki kiwanja katika ya jiji (Posta) na kujenga kumbi ya starehe ilikuwa ikijulikana kama Mbowe na sasa (bilicanas), amepata wapi pesa ya kumiliki ardhi kubwa Arusha na Moshi na kuweza kujenga mahoteli kule?

hivi,kagoda,meremeta,richimondi na dowansi,orodhesha hapa mrejesho wake,na mimi nitakuorodheshea,
 
dada HAMIDA hivi huna jambo jingine la maana la kitaifa zaidi ambalo unaweza kuliweka hapa na watu tukalichangia kwa umakini zaidi?au ndio masharti ya buku saba za lumumba kwamba lazima kila siku uandike habari za kijinga kuhusu chadema?Kweli hakuna umaskini mbaya fikra kama wako!yaan upo radhi kutumika kama ile mipira ya c......m ukimalizwa unatupiwa kule.
 
FaizaFoxy
Acha kuwa na akili za kuku,ukikuta watu wanatolewa huduma kinyume na maumbile utaenda na wewe ufanyiwe kwa sababu wao wanafanyiwa? Kwa kuwa Vatikan crime wanafanya nawe ufanye? Una akili kweli
JITAMBUE

Wewe ndio mwenye akili finyu, kwanini uhusishe mambo ya Zanzibar na Uislaam na ushindwe kuhusisha dhambi za vatikano na ukristo?
 
kwanini Kikwete ni nani?, mbona yeye uwa hana hizo anasa anazofanya Mbowe?, unasema Mbowe yuko bize kuliko JK hawapo nchini?

U-busy wake uko kwenye kutetea na kuwalinda wauza unga. Kwahiyo u-busy unatofautiana.
 
Back
Top Bottom