Hivi 'chopa' ya CHADEMA inatumika Arusha na Moshi pekee?

Hivi 'chopa' ya CHADEMA inatumika Arusha na Moshi pekee?

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,146
Reaction score
3,830
WanaJF!

Ni imani yangu tuna tambua kuwa Tanzania yetu ni moja na watanzania wote ni wamoja katika mambo yote yanayohusu taifa letu, ikiwemo mambo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa, na wote kama watanzania tuna stahiki kupata mambo haya kwa usawa.

Katika hali kama hiyo ya kupata hayo mambo kwa usawa, nasikitika kusema kuna kundi fulani la watu aidha hawapo tayari kutoa usawa huo ama hawajui kuwa ndio tamaduni na desturi yetu watanzania kushiriki kwa usawa kwenye mambo tajwa hapo juu.

Katika kulisisitiza hili, ningependa tutizame siasa za CHADEMA, hivi karibuni umefanyika uchaguzi wa madiwani kwenye zile kata ambazo madiwani wake aidha walitimuliwa ama walifariki hivyo kata kubaki wazi, katika chaguzi zile CHADEMA walifanya ubaguzi mkubwa mno.

Kata zilizo kuwana uchaguzi zilikuwa maeneo mbalimbali ya nchi, ikiwemo Mbeya, Morogoro, Mara na Manyara, lakini 'CHOPA' ya CHADEMA ilipaa Arusha tu na wala haikuchungulia sehemu nyingine yoyote hapa nchini.

Aidha, huko Arusha 'CHOPA' ya CHADEMA ilikuwa busy kwenye kata zote, yani haikuwahi kutokea kampeni zifanywe bila matumizi ya 'CHOPA' hiyo kwa kipindi chote cha uchaguzi wa kata za pale Arusha.

Kama hiyo haitoshi, hivi sasa kamanda wa anga, bwana Mbowe, yupo Hai kama mbunge wa jimbo hilo, lakini kwa ubabe wake amehamua atumie 'CHOPA' hiyo kufanya shughuli zake zote, yani kama mbunge na pia mwenyekiti wa chama.

Kwa kufanywa hivyo inakuwa sio sawa, kama itakuwa hivyo basi na majimbo mengine nayo yapelekewa 'CHOPA' ya CHADEMA na isibaki Arusha na Moshi pekee, kwani ikiendelea hivyo itatafsiriwa kuwa CHADEMA ni chama cha ukanda.
 
Vita hupiganwa kwa hesabu, hata Mwanza chopa huja. Unataka wawashe chopa Zanzibar ambapo jimbo ni kijiji????
 
Hata CCM ni chama cha Ukanda, waulize Pemba kama unabisha; Unabwabwaja sana Mbowe ni Chair, Kambi rasmi na MP ana mambo mengi lazima atumike kwa faida kila dk inayopatikana, I hope umeelewa. Hujui ofisi za spika zilijengwa Urambo??? fikiria tena
 
Vita hupiganwa kwa hesabu, hata Mwanza chopa huja. Unataka wawashe chopa Zanzibar ambapo jimbo ni kijiji????

Usikimbie mada, mada haiongelei uchaguzi mkuu, kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2011 CHADEMA imekuwa ikifanya siasa na 'CHOPA' hapo Arusha tu, kama unabisha, ni kwanini kwenye uchaguzi wa madiwani chopa haikuvuka mipaka ya Arusha?
 
Tunafuga paka si kwasababu haibi chochote sometimes utakuta kala mboga, lakini vile ni mbaya zaidi kuishi na panya tena panya waharibifu wa kila sekta-utamaduni wameharibu, elimu wameharibu, madini wameharibu, uongozi wameharibu leo tunatukanwa kila kona na majirani, uchumi kutoka 4% hadi 19.2% mfumko wa bei huo, kodi zinapanda mshahara inakuwa duni, ubaguzi na udini, wizi na ufsadi yapo mengi tu, ndo maana tunamudu gharama za paka ili kuwaondosha panya na ukoo wake. Tutachangia helikopta kila siku ipasue anga.
 
"-------- ukimchukua ukimchanganya na ngano kwenye kinu atabaki na upumbavu wake." Mithali 27:22
 
Ile ni ya nyumbani kweni wengine inawahusu nini ile ya sisi kwa sisi tena mkome kuiulizia nyie wengine mnaoiulizia mnamchango gani kwa chadema.
 
Hata CCM ni chama cha Ukanda, waulize Pemba kama unabisha; Unabwabwaja sana Mbowe ni Chair, Kambi rasmi na MP ana mambo mengi lazima atumike kwa faida kila dk inayopatikana, I hope umeelewa. Hujui ofisi za spika zilijengwa Urambo??? fikiria tena

kwanini Kikwete ni nani?, mbona yeye uwa hana hizo anasa anazofanya Mbowe?, unasema Mbowe yuko bize kuliko JK hawapo nchini?
 
Usikimbie mada, mada haiongelei uchaguzi mkuu, kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2011 CHADEMA imekuwa ikifanya siasa na 'CHOPA' hapo Arusha tu, kama unabisha, ni kwanini kwenye uchaguzi wa madiwani chopa haikuvuka mipaka ya Arusha?

Nimekwambia vita ni hesabu unatakaje dogo?? ushamba wenu huo ndo maana tulianza mkiwa na majimbo yote sasa tumekula 50, subiri 2015 obvious times 3-4. hayo wa wachumba zenu hatuhesabu.
 
Nimekwambia vita ni hesabu unatakaje dogo?? ushamba wenu huo ndo maana tulianza mkiwa na majimbo yote sasa tumekula 50, subiri 2015 obvious times 3-4. hayo wa wachumba zenu hatuhesabu.

Hoja hapa ni kwanini 'CHOPA' ya CHADEMA itumike Arusha na Moshi?, kwani Mbeya CHADEMA haina wapenza na mashabiki?, mbona Chopa haikwenda huko katika chaguzi za kata na kuimarisha chama?
 
Usikimbie mada, mada haiongelei uchaguzi mkuu, kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2011 CHADEMA imekuwa ikifanya siasa na 'CHOPA' hapo Arusha tu, kama unabisha, ni kwanini kwenye uchaguzi wa madiwani chopa haikuvuka mipaka ya Arusha?

Uwe na kumbukumbu,chopa ilienda songea,mbeya,iringa,moro,mwanza,shinyanga na kumalizia manyara na arusha.Unachokizungumza ni ushabiki tuu.
 
Hivi hujui hata matumizi ya herufi kubwa!....hapa unaandika "watanzania" badala ya "Watanzania".....Embu jirekebishe....unatia aibu; alama kama mkato, nukta, zinakupiga chenga
 
kwanini Kikwete ni nani?, mbona yeye uwa hana hizo anasa anazofanya Mbowe?, unasema Mbowe yuko bize kuliko JK hawapo nchini?

kuwe busy mwehu yoyote anaweza kuwa hoja ni busy unafanya nini? hata vyangudoa wako busy sana
 
Hoja hapa ni kwanini 'CHOPA' ya CHADEMA itumike Arusha na Moshi?, kwani Mbeya CHADEMA haina wapenza na mashabiki?, mbona Chopa haikwenda huko katika chaguzi za kata na kuimarisha chama?


Ukishajua ni kwanini itakusaidia nini? Ungekuwa na mawazo hai ungemsaidia nape na hoja yake ya ajira kuliko kukimbilia hili ambalo halikisaidii chama chako cha magamba.
 
Hivi HAMY-D, Nani kakwambia kuwa chopa ilitumika kwenye kampeni zote za Arusha?

Kwa taarifa yako chopa ilitumika kwenye uzinduzi wa kampeni za Arusha tu na siku zilizobakia kamanda lema alikuwa anapiga kampeni kwa kutumia magari na bodaboda tu. Na siku ya kuitimisha kampeni kamanda Mboe alitumia chopa kuzunguka kata zote tz zilizokuwa na uchaguzi na Arusha alitua saa 4:20pm.

Hapo inaonyesha jinsi gani HAMY-D unaropoka na zaidi tunaona jinsi gani akili za mabosi wako Nape na Mwigulu zinavyofanya kazi kwa kurudi nyuma.
 
Last edited by a moderator:
Hivi hujui hata matumizi ya herufi kubwa!....hapa unaandika "watanzania" badala ya "Watanzania".....Embu jirekebishe....unatia aibu; alama kama mkato, nukta, zinakupiga chenga

Wewe baki na kiswahili choko sanifu mimi niache nilikomboe taifa.
 
Hoja hapa ni kwanini 'CHOPA' ya CHADEMA itumike Arusha na Moshi?, kwani Mbeya CHADEMA haina wapenza na mashabiki?, mbona Chopa haikwenda huko katika chaguzi za kata na kuimarisha chama?
Huko Mbeya CHADEMA wanaanza kushitukiwa, watu wa Mbeya wanaona wanavyotumika kubeba miizgo mizito ya bwana wao kama punda.
 
Back
Top Bottom