Hivi Bongo Muvi wana Shida gani hawa watu?

Hivi huyu marehemu anahitaji faraja kwa kipindi akiwa marehemu kuliko kipindi kile alipokuwa na kesi mahakamani!? Mbona mimi binafsi sikuwahi kuwaona hao vilaza wanaojiita bongo movies wakimfariji kipindi akiwa na kesi!?
mi nawaaangalia tuuu sipendagi unafki
 
Stiv Nyerere anavizia kula rambi rambi km alivyo fanya kwa Marehemu Kanumba
 
Eti kikao wanafanyia leaders club,,,labda wangesema tunakutana na familia yake tujue kinaendelea nini
 
Nimejiuliza sana,kuhusu Bongo muvi kuuvalia njuga msiba wa Agnes Nyie kama wakina nani? kwenye kesi yake mbona hamkuonekana hata? mnatoka na taarifa zinazotuchanganya mara mnasema kafa kwa homa ya matumbo na kupungukiwa damu leo mwingine anasema kafa kwa pumu...kila mtu anataka kuchukua ujiko kupitia kwa marehemu mara Irene Uwoya kasema hivi,mara Ka Steve Nyerere kanapanga ratiba ya msiba mara sijui Chopa anasema marehemu alimwambia maneno mawili kabla ya kukata roho WTF!! who are you people? Acheni mambo ya Kikanjunju....Familia ya Marehemu ipo waacheni wao ndio watoe na taarifa za msiba....Tangu lini Age alikuwa msanii wa filamu?
Leta Updates kinachojiri huko kwa kina Age
 
Binafsi Sioni tatizo wao kuubeba msiba,Aggy Kafariki akiwa na Chopa Huenda ijakawa alikuwa na urafiki na watu wa bongo movie japokuwa hajaigiza movie yoyote

Isitoshe ni rafiki wa Karibu wa irine uwoya na wasanii Wengine wa movie

Nilivyosikia ndugu zake wako mbeya ,wao kama wamejitolea kusimamia safari yake ya Mwisho msiwaseme vibaya kwasababu hao bongoflava hajajitokeza hata mmoja Japo nimemuona dogo janja ila alikuwa pale kwaajili ya mkewe
Nimekupenda bure
 
Mtazamo wangu
1. Sijaona ubaya bongo movie kuungana katika msiba wa marehemu Masogange hata kama hajaigiza movie yoyote,huko tunaita kujumuika kijamii(socialize) kama hujui maana uliza usaidiwe.Ndio maana hata katika misiba yetu sis tulioko kitaani ukifiwa majirani huja msibani je wale ni ndugu zako wa damu? je wanajipendekeza au wanakuja kukufariji?
2. Tuache kujidai wajuaji katika mambo ambayo yametuzidi kimo.Tuwe na akiba ya maneno,kuongea sana sio kuzuri.
3. Kwa desturi ya mwanadamu pindi binadamu mwenzetu anapofariki tulio hai tuna mafunzo ya kujifunza na kukumbuka kwamba duniani tupo kwa msimu tu kwa hiyo pumzi uliyonayo isikufanye ujifarague kwamba wewe ni bora kuliko aliyekufa wakati ni wewe ni marehemu mtarajiwa,isitoshe kati yetu hakuna ajuaye kifo chake kitakujaje.

Asante
 
Lakini mbona hawakujitokeza kipindi cha kesi yake,,,,,,, unamuonaga Dr cheni anavyohangaikaga kwenye kesi za lulu,anakua nae kwenye shida na raha,hata hawa bongo muvi ilibidi wawe wanaenda mahakaman kumsapoti,


Ataacha je kuhangaika na kesi ya mwanawe wa kufikiwa si nasikia huwa pale kwa mama Lulu Dr kaweka makoloni au?
 
Mungu anisamehe jamani ila haka kamtu nakaona kama kanafiki sana..na mwenzake McPilipili.


Huyo MC Pilipili na sauti yake ya kike kabisa sijawahi kujua anachekesha nini? Steve fupi nyundo sijui ni kundi la wazee au kijana mnisaidie hapo
 
Huwa simuelewi Steve anapenda sana nafasi ya kupokea rambirambi
Steve.jpg
 
Hivi bashite muda alioishi naye huyu alishindwa kutoa kopi hata moja ibaki kuwa kiburudisho kwa kizazi kijacho kaacha zigo lote limeenda bure duu! kweli hasara bashite katupa kushindwa kufyatua kopi ya dude hiloo baktelia wanafaidi huko jinga kabisa hili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom