Historia ya Soko la Kariakoo na Mchora ramani Beda Amuli

IMG_7645.jpg

Historia ya jina la Kariakoo na soko la Kariakoo inaanzia tangu enzi za ukoloni wa Mjerumani wakati Tanzania Bara ikiitwa Tanganyika.

Mahala lilipo soko hilo palijengwa jengo la utawala wa Wajerumani ambalo lilikusudiwa litumike kama ukumbi wa kuadhimisha sherehe za kutawazwa kwa Mfalme Kaiser Wilheim wa Ujerumani kwa wakati huo.

Hata hivyo baada ya jengo kukamilika halikutumika kama ilivyokusudiwa kuwa na badala yake lilitumika kama kambi ya kikosi cha wapagazi waliobeba mizigo ya vita kuu ya kwanza ya dunia waliojulikana kama Carrier Corps.

Jina hilo la maaskari wabeba mizigo katika Kiswahili lilitamkwa karia- koo na liliendelea kutumika kama jina la eneo lote linalozunguka jengo hili la Soko la Kariakoo.

Baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia kuisha rasmi mwaka 1919 na nchi Tanganyika kuanza kutawaliwa na Uingereza, jengo hilo lilianza kutumika kama soko na kuhudumia wakazi wa Dar es Salaam. Wakati huo wafanyabiashara walikuwa wakiuza bidhaa zao sakafuni kwa sababu hapakuwa na meza. Wafanyabiashara hao waliendelea kufanya biashara zao sakafuni hadi miaka ya 1960, meza za saruji zilipojengwa. Kwa kadiri jiji la Dar es Salaam lilivyokua na wakazi wake kuongezeka, ndivyo soko hilo lilielemewa kuhudumia wananchi.

Hali hiyo iliwafanya viongozi wa halmashauri ya jiji kuona haja ya kuwa na soko kubwa na la kisasa kulingana na maendeleo ya jiji, na hivyo wakaanza kujadili uwezekano wa kujenga soko jipya kubwa na la kisasa.

Ujenzi wa soko

Uamuzi wa kujenga Soko Kuu la Kariakoo ulifanywa na serikali mwaka 1970 ambapo Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam iliagizwa kujenga soko jipya la kisasa ambalo lingechukua nafasi ya soko la zamani.

Matarajio ya serikali ya kujenga soko hilo yalikuwa ni kuwapatia wakazi wa jiji soko kubwa la chakula ambalo lingetosheleza mahitaji yao kwa muda wa miaka 50 hadi 70 Mipango ilikamilika na ujenzi ulianza rasmi Machi 1971.

Ramani ya jengo la soko ilitayarishwa na mchoraji wa ramani za majengo Mtanzania Beda Amuli. Kwa mujibu ya machapisho yanayoelezea historia ya soko hilo, mkandarasi huyo alitakiwa kwenda kujifunza katika nchi za Accra – Ghana na Lusaka-Zambia, kuangalia masoko yaliyojengwa katika miji hiyo miwili, ndipo atengeneze ramani yake, ambalo ndiyo soko linaloonekana hivi sasa. Mkandarasi aliyechora jengo hili ameweka baadhi ya maumbo yanayofanana na majengo hayo aliyokwenda kuyatazama. Hii ndiyo sifa pekee inalolifanya soko hili la Kariakoo kuwa la tofauti na masoko mengine katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati.

Ujenzi wa soko ulikamilika Novemba 1975 kwa gharama ya shilingi milioni 22 na kufunguliwa rasmi Desemba mwaka huo huo ambapo Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere alikuwa mgeni rasmi.

Zaidi:
1) Soko la Kariakoo lateketea kwa moto

2) TANZIA - Mzee Beda Amuli, mbunifu na mchoraji wa majengo, likiwemo Soko la Kariakoo afariki dunia

IMG_7644.jpg
 

Rugby Union

JF-Expert Member
Nov 21, 2012
402
249
Katika mwaka 1914, Serikali ya kikoloni ya Ujerumani ya Tanganyika iliamuru jengo la kwanza katika ardhi kwenye Soko la Kariakoo. Jengo lilijengwa kwa ajili ya kufanya sherehe ya maadhimisho ya kutawazwa kwa Mfalme Kaiser Wilheim, lakini Vita vya Kwanza vya Dunia vilianza kabla ya tukio kuweza kutokea.

Wakati wa vita, Dar es Salaam na Tanganyika zilianguka chini ya utawala wa Uingereza. Jeshi la Uingereza lilitumia jengo kama kambi la kitengo cha jeshi la askari, timu ya mabawabu wa kiafrika ambao waliunga mkono jeshi la Uingereza kwenye vita. Timu ya wachukuzi Watanzania waliotegemezwa kwa askari wa Uingereza katika mapigano.

Baada ya vita mwaka 1919, serikali ya kikoloni ya Uingereza ilibadilisha sehemu hiyo na kuwa soko. Soko likaitwa "Kariakoo", ambayo ni tafsiri ya Kiswahili ya neno "Jeshi la askari", kwa heshima ya watu waliopigana katika vita. Kadri Dar es Salaam ilivyozidi kukua kama jiji, mazao kadhaa wa kadha yalipitia soko hilo kwa wingi, mnamo miaka ya 1960, baada ya uhuru wa Tanzania, serikali ndogo ya Nyerere iliamuru simenti na magenge imara yajengwe kwa ajili ya wauzaji.

Mwaka 1970, serikali ya taifa iliagiza Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam wafanye mipango ya ujenzi wa soko la kisasa litakalodumu kwa miaka hamsini mpaka sabini. Uongozi wa kitaifa uliiagiza Halmashauri ya Jiji kushirikisha sehemu muhimu ya soko la mazao lililopo katika Jiji Accra nchini Ghana na Lusaka nchini Zambia.

Msanifu majengo Mtanzania Beda J. Amuli alichora ramani ya jengo jipya na ujenzi ulianza Machi 1971, iliyoongozwa na kampuni ya Kitanzania Mwananchi Engineering and Contracting Co. Soko lilikamilika Novemba mwaka 1975 kwa gharama ya shilingi milioni 22 pesa ya Kitanzania.

Sehemu ya soko ina majengo mawili, jengo kuu lenye ghorofa tatu yenye magenge na maofisi, na jengo dogo la pili. Vyote kwa pamoja vikijumuisha eneo la mita za mraba zaidi ya 17,000. Desemba 8, 1975 Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere alifungua soko jipya la kihistoria kwa hafla.

Kabla ya ujenzi kuisha, Oktoba 1974 Bunge ilianzisha Shirika la Soko la Kariakoo (SMK) na kuihusisha na kazi za uendeshaji wa soko. SMK ilipaswa kujilipia uendeshaji wake kwa kupangisha magenge kwa wauzaji na kuwatoza asilimia ya faida ya mauzo. Shirika lilipewa fedha na fungu la jumla la shilling za kitanzania milioni 25, ambayo ilimilikiwa na serikali kwa asilimia mia.

Mkataba wa soko ulithibitisha kua SMK itaongozwa na Meneja Mkuu na bodi ya wakurugenzi ambao wote watateuliwa na rais mwenyewe. Meneja mkuu na bodi nzima walipaswa kuchagua maafisa watakaoongoza soko pamoja nao.

Kabla ya ujenzi kumalizika, katika mwezi kumi mwaka 1974, Bunge lilithibitisha Shirika la Soko la Kariakoo (SMK), shirika la serikali litakaloendesha soko. SMK liliombwa kujilipia shughuli zake kwa kupangisha maduka kwa wachuuzi na kuchukua asilimia ya faida ya mauzo.

Kwa kuanza, Shirika liligharamiwa na Hisa zilizofikia milion 25 za Kitanzania kwa jumla, zilizomilikiwa na serikali kwa 100%.

Toka mwaka 1975, Shirika la Soko la Kariakoo linaendelea kuendesha soko chini ya uongozi wa Serikali ya Tanzania. Soko linaendelea kuwa mahali pakuu pa kuuza mazao Tanzania.

Chanzo: Soko la Kariakoo
 
SMK baada ya kupatikana soko hilo shirika limezalisha masoko mengine mangapi? Nikiyafahamu masoko mengine yalio tokana na soko la kkoo nitatafsili kwamba limejiendesha kwa faida
 
Huyu mchoraji wa Hilo jengo, Bwana Beda Amuli alikua na makazi yake miaka ya 90 pale Kimara enzi za bar maarufu ambayo ilikua na jina la MAKONDEKO. Kama yupo hai kwa sasa atakua na umri mkubwa. Kwa anae jua habari zake atujuze kama huyu mhandisi bado yuko hai na anaendeleaje na maisha.
 
Back
Top Bottom