#Baharia, pia "mwanamaji" ni mtu anayefanya kazi kwenye chombo cha usafiri majini, hasa baharini kama vile boti, mashua, jahazi au meli. "Mwanamaji" hutumiwa mara nyingi kwa kutaja mabaharia wa kijeshi.
Kuna kazi nyingi tofauti zinazotekelezwa na mabaharia.
Mkuu wao ni nahodha au kapteni wa chombo.
Katika mashua au jahazi ndogo mabaharia wote wanafanya kazi pamoja ambapo kazi zinazoonekana ngumu zaidi hupewa kwa wale walio vijana.
Kadri meli inavyokuwa kubwa zaidi, shughuli mbalimbali za melini zinagawiwa kwa mabaharia wenye ufundi fulani.
Meli kubwa zinaweza kuwa na idara tofauti zinazohitaji mabaharia wenye fani mbalimbali.
---------
SASA WAVUTA BHANGI WA BONGO HIVI KARIBUNI WAMEAMUA KUICHAFUA TASNIA YA "UBAHARIA" KWA KUIHUSIANISHA NA WAZINZI WA KIUME,
WENYE NIA YA KUWACHEZEA NA KUWAHARIBU WANAWAKE KIHISIA PASI NA KUJALI LOLOTE KUHUSU WANAWAKE HAO.
TANBIHI:
#UBAHARIA NI TASNIA HALALI KAMA ZILIVYO ZINGINE,
NA SIO UHUNI KAMA AMBAVYO HUPOTOSHWA NA VIJANA SIKU HIZI.
Tamati:
HATA HIVYO,
LUGHA INA TABIA YA KUWA NA MISIMU INAYOSHIKA HATAMU KATIKA KIPINDI FULANI,
HIVYO "BAHARIA" LAWEZA KUTUMIKA KAMA MSIMU KATIKA MUKTADHA FULANI.
[emoji1378][emoji469][emoji469][emoji469][emoji469][emoji469]