Inawezekana familia pia inahusika,inakuaje mzazi na ndugu hawashtiki kabisa kwa unayopitia??
Sali sana hakuna linaloshindikana kwa Mungu.
Sent from my SM-A205F using
JamiiForums mobile app
Kuna Ndugu yangu (tumbo Moja ) ana pesa katika familia yangu....hanipendi hata kidogo...ananichukia sana....Huwa sielewi ananichukia kwasababu gani....nimeishawahi kumuomba anisamehe ( mara nyingi sana) kama nimewahi kumkosea kwà kujua ama kwà kutokujua lakini Huwa hataki.
Huyu Ndugu aliwahi kunipeleka mahabusu...kwà kutumia pesa na kunitoa nje kwà pesa. Hii ilikua mara yangu ya pili kwenda jela.
Mara ya KWANZA...ilikua nimemaliza Chuo....nikasema niende nyumbani kumsalimia Mama kwani nilikua nina miaka zaidi ya minne sijakanyaga nyumbani.
Nilivyofika nyumbani....baada ya siku 3 nikapata kesi kubwa sana mahakamani ambayo ilidumu kwà miaka mitano.
Source ya kesi ni :-
Pale nyumbani nilimkuta Kaka yangu ambae ndiye alikua mwenyeji. Sasa kumbe alikua na Bifu na watu wa Idara maji...walikua wakija kufunga bomba la maji Ili maji yaende kwà pressure kubwa kwà mheshimiwa diwani ambae alikua jirani yetu.
Ugomvi baina yao ukawa...why wafunge maji wakati wanayalipia bill? Wakati wanazozana huko , Mimi nilikua ndani nimetulia.
Nafikiri yule jamaa wa Idara ya maji hakupendezwa na jinsi alivyozozana na kaka yangu. Kesho yake Asubuhi akaja .....akauliza yule kaka wa jana yuko wapi? Bahati nzuri Blaza hakuepo....nilikuepo Mimi...akaambiwa hayupo....yupo mwingine. Nikaitwa...nikaulizwa mwenzako yuko wapi? Nikasema katoka.....
Nikaona jamaa katoka nje ya geti kumbe amekuja na askari pale home....nikasikia anawaambia au twendeni na huyo ...yeye akija ndio tutamuachia huyu....
Kiufupi, nilichukuliwa pale home nikapelekwa Polisi....nilipigwa sana siku hiyo ...nilivuja Damu mwili mzima....mpaka nikapoteza fahamu.
Walivyogundua nataka kufa....wakaanza kunimwagia maji usiku wa manane...
Wakaandika maelezo,...wakanishikisha dole gumbe nikapiga sahihi ya dole...
Kesho yake Asubuhi nikakimbizwa hospital....baada ya matibabu nikapelekwa mahakamani....nikapelekwa mahabusu jioni.
Nikasgitakiwa kwà makosa:-
1. Nimemzuia afisa wa Idara ya maji kufanya Kazi yake
2. Nimewazuia Polisi kufanya Kazi yao.
Hii kesi ilidumu kwà miaka mitano. Ilinitesa sana ingawa ilikua na wakili.